Mahakama Kuu Dodoma, imefuta pingamizi la ushindi wa Ubunge wa Lissu

Makete Kwetu

JF-Expert Member
Jan 8, 2012
531
165
12417905_1417527564928324_8851612452659773904_n.png

Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, jana ilifuta kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, kushoto aliyeongozana naye ni mwalimu Samson Mkotya.


Ushindi wa ubunge wa jimbo la Singida Mashariki alioupata Tundu Lissu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hauna doa baada ya kubarikiwa na mahakama.

Mahakama Kuu kanda Maalum ya Dodoma jana imefuta pingamizi la ushindi wa Lissu lililowekwa mahakamani hapo na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, Jonathan Njau.

Jaji Berkel Sehel aliamua kufuta kesi hiyo baada ya mlalamikaji Njau kuiomba mahakama kuiondoa kesi hiyo akieleza kuwa hataki kuendelea nayo.

Katika kesi ya msingi, Njau alikuwa akipinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu na kumpa ushindi Lissu. Aliitaka mahakama kufuta matokeo hayo na kuamuru kura zihesabiwe upya.

Chanzo: Dar24

My take: Huyu jamaa ni mara ya pili anabwagwa na TL kwenye uchaguzi na anakata rufaa, ila safari hii naona kaona ni kupoteza pesa na mda wake kuendelea na kesi na mtu 'dizaini' ya Lissu guru wa sheria. TL huwa haweki wakili, anasimamia show mwenyewe
 

Attachments

  • TL.GIF
    TL.GIF
    55.8 KB · Views: 81
..huyo Njau wa kutandika viboko,anaichezea mahakama,haiwezekani akurupuke tu kufungua kesi halafu baadae aamue kuifuta..ina maana hakujiandaa.
 
View attachment 318446
Ushindi wa ubunge wa jimbo la Singida Mashariki alioupata Tundu Lissu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hauna doa baada ya kubarikiwa na mahakama.

Mahakama Kuu kanda Maalum ya Dodoma jana imefuta pingamizi la ushindi wa Lissu lililowekwa mahakamani hapo na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, Jonathan Njau.

Jaji Berkel Sehel aliamua kufuta kesi hiyo baada ya mlalamikaji Njau kuiomba mahakama kuiondoa kesi hiyo akieleza kuwa hataki kuendelea nayo.

Katika kesi ya msingi, Njau alikuwa akipinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu na kumpa ushindi Lissu. Aliitaka mahakama kufuta matokeo hayo na kuamuru kura zihesabiwe upya.

Chanzo: Dar24

My take: Huyu jamaa ni mara ya pili anabwagwa na TL kwenye uchaguzi na anakata rufaa, ila safari hii naona kaona ni kupoteza pesa na mda wake kuendelea na kesi na mtu 'dizaini' ya Lissu guru wa sheria. TL huwa haweki wakili, anasimamia show mwenyewe
Njau!!! unganisha dots.
 
Back
Top Bottom