Jamani kuna kikao kilikaa jana usiku kuanzia saa tatu usiku pale Hyatt Hotel chini ya January Makamba, Mdogo wake January anaitwa Thuwein Makamba, Wema Sepetu, Abdulhaman Kinana na Sadik Mbarouk..
Kikao kilikua na mkakati wa kuanza kununua wasanii wanao mpa support Mh. Edward Lowassa ili waonekane wamechoka na mienendo ya Ukawa na zaidi kumchafua mgombea wake Mh. edward Lowassa.
Kampeni hiyo iliyobeba dhana ya Kung'atuka itakuwa ina dhaminiwa na tajiri maarufu anae jishughulisha na vyombo vya usafirishaji, Bwana Sadik Mbarouk aliyemwaga pesa za kutosha za kuwavuta wasaniii hao.
Mpaka jana usiku walifikia mpango wa kuwang'oa wasanii wawili, akiwemo Aunt Ezekiel na Ray Kigosi kwa dau la Million 50 kila moja. Kazi hiyo imeanza kutekelezwa leo asubuhi majira ya saa tatu na nusu, ambapo Gari aina ya Landcruiser V8 yenye namba za usajili T257CET iliyofika Nyumbani Hoteli mtaa wa posta na kuwachukua kuwapeleka uwanja wa ndege na kupanda ndege iliyo andaliwa maalum kwa ajili ya kuwashusha Dar es Salaam kwa ajili ya kusaini mkataba na kuchukua fungu lao.
Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni.. Wazungu wanasema "Every one has a price", yaani kila mtu ana bei yake, Bei ya Aunt Ezekiel na Ray Kigosi ni Millioni 50 na haaaaoooo safari imeanza ya kuvunja matumaini ya watanzania waliwo waamini.. Mwaka huu tutayaona Mengi