boyayoparuparu
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 343
- 82
Sasa hivi hakuna biashara ya watumwa,kinachoendelea duniani ni utumwa wa kiuchumi,tunawatumikia mabwanyenye kupitia fedha,ukitaka fedha yao moja uwe na za kwetu gunia moja,hawakubali hata kidogo wakiona nchi flani fedha yake ikaikaribia thamani ya dola,endapo nchi hiyo inataka kuikaribia fedha yao zitafanyika mbinu mbali mbali ili fedha yao ishuke thamani na utumwa wa kiuchumi uendelee.
Kinachotokea Syria,kilicho mtokea Gaddafi,Saddam nk ni moja ya mbinu zilizotumika kuhakikisha utumwa wa kiuchumi unaendelea.
Katika nchi zetu hapa tuna mifano katika nchi yetu Tanzania, Burundi, Rwanda.Burundi na Rwanda mara nyingi kunakuwa na vita za wenyewe kwa wenyewe mara tu fedha zao zinapoikaribia dola,bahati mbaya hata wasomi hawana muda wa kutafuta chanzo cha vita hizo badala yake wanaimba wimbo ulioanzishwa na vyombo vya Magharibi.
Tanzania tulipokuwa na uchumi imara tulipiganishwa na nchi ya Uganda,wakati Kikwete anashika nchi,alijaribu kutoa yale mabilioni yaliyokuwa yanaitwa ya Kikwete lakini akawa Rais wa kwanza kukutana na rais Obama,mara tu baada ya Obama kuapishwa na baada ya hapo hatukusikia tena akitoa mabilioni yale wakati alikuwa amekwishaahidi kuyatoa kila mwaka.
Sasa napenda kumwambia Magufuli, ajue kuwa anachokisema na kuahidi kukifanya ajue kuwa anahitaji tahadhari kubwa sana,kwenye kila kitu hasa kwa maisha yake,yeyote anayebisha aniambie kwanza sababu ya marais wa Iraq,Libya,Venezuela nk ni kwanini waliuawa!!
Syria ni kwanini anawindwa kama mbwa,rais yeyote anajenga urafiki, uswahiba,anayesifiwa na mabeberu,takwimu za kiuchumi zinasalia kuwa namba tu,hazina uhusiano na hali halisi kwa maisha ya mwananchi wa hali ya chini.
TUNASOMESHWA MANAMBA TU.
Kinachotokea Syria,kilicho mtokea Gaddafi,Saddam nk ni moja ya mbinu zilizotumika kuhakikisha utumwa wa kiuchumi unaendelea.
Katika nchi zetu hapa tuna mifano katika nchi yetu Tanzania, Burundi, Rwanda.Burundi na Rwanda mara nyingi kunakuwa na vita za wenyewe kwa wenyewe mara tu fedha zao zinapoikaribia dola,bahati mbaya hata wasomi hawana muda wa kutafuta chanzo cha vita hizo badala yake wanaimba wimbo ulioanzishwa na vyombo vya Magharibi.
Tanzania tulipokuwa na uchumi imara tulipiganishwa na nchi ya Uganda,wakati Kikwete anashika nchi,alijaribu kutoa yale mabilioni yaliyokuwa yanaitwa ya Kikwete lakini akawa Rais wa kwanza kukutana na rais Obama,mara tu baada ya Obama kuapishwa na baada ya hapo hatukusikia tena akitoa mabilioni yale wakati alikuwa amekwishaahidi kuyatoa kila mwaka.
Sasa napenda kumwambia Magufuli, ajue kuwa anachokisema na kuahidi kukifanya ajue kuwa anahitaji tahadhari kubwa sana,kwenye kila kitu hasa kwa maisha yake,yeyote anayebisha aniambie kwanza sababu ya marais wa Iraq,Libya,Venezuela nk ni kwanini waliuawa!!
Syria ni kwanini anawindwa kama mbwa,rais yeyote anajenga urafiki, uswahiba,anayesifiwa na mabeberu,takwimu za kiuchumi zinasalia kuwa namba tu,hazina uhusiano na hali halisi kwa maisha ya mwananchi wa hali ya chini.
TUNASOMESHWA MANAMBA TU.