kkarumekenge
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 1,708
- 1,028
Yule aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, anayetamba yupo karibu sana na JK, amewatukana Wakerewe na uongozi wote wa wilaya. Wiki hii Mulongo ambaye amehamishiwa mkoani Mwanza, alikuwa Ukerewe. Akasema hajawahi kuona watu washamba kama Wakerewe na kwamba kama hali ikiendelea hivyo Ukerewe itatawaliwa kijeshi. Hakuishia hapo aliamuru diwani mmoja awekwe ndani.
Kwao Mulongo ni shamba pengine kuliko sehemu yoyote Tanzania. Anatoka Wilaya masikini kuliko zote, Bunda, sehemu iitwayo Karukekera. Shamba kabisa.Haina maji, umeme nk. Shamba kabisa.
Wakerewe walivyo "washamba" walimjibu tu "kishamba"; "umetuchokoza!" Hoja hapa si Wakerewe,bali ni kwanini viongozi wa Tanzania wameanza kutukana watu hasa hawa watokao mkoani Mara? Kwanini siku hizi kiongozi anaweza kutukana watu na kuachwa hivi hivi bila kuchukuliwa hatua?
Kwao Mulongo ni shamba pengine kuliko sehemu yoyote Tanzania. Anatoka Wilaya masikini kuliko zote, Bunda, sehemu iitwayo Karukekera. Shamba kabisa.Haina maji, umeme nk. Shamba kabisa.
Wakerewe walivyo "washamba" walimjibu tu "kishamba"; "umetuchokoza!" Hoja hapa si Wakerewe,bali ni kwanini viongozi wa Tanzania wameanza kutukana watu hasa hawa watokao mkoani Mara? Kwanini siku hizi kiongozi anaweza kutukana watu na kuachwa hivi hivi bila kuchukuliwa hatua?