Ni kuhusu makosa Makubwa katika vitabu vya msingi Vya kufundishia.
Imegundulika kuwa Katika vitabu vya kufundishia Katika shule za msingi kuna makosa makubwa na mengi yanayo pelekea kuwalisha watoto wetu unga wa ndere uliochanganyika na matango pori badala ya unga wa rut'ba.Tatizo hili limekuwa likitokea licha Ya vitabu hivyo kupitishwa na EMAC.
Haya yamewekwa bayana na Mbunge wa kuteuliwa na rais,James Mbatia (NCCR-Mageuzi) wakati akichangia hotuba ya wizara ya Elimu Jana. Akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Elimu, Mbatia alionesha vitabu kadhaa bungeni , akitaja makosa mengi yaliyomo na kuhoji vili idhinishwaje na (EMAC).
Mbatia alisema "Serikali imetumia fedha za chenji ya Rada kusaini mikataba na kampuni zaidi ya 10 kwa ajili ya kusambaza vitabu kwenye shule zetu, lakini vitabu hivyo ni sumu kwa taifa, Alisema kuwa vitabu hivyo vimenunuliwa na fedha hizo sh bilioni 55.2 ambazo zilitengwa na serikali kwa ajili ya manunuzi ya vitabu na mihutasari.Mbatia alisema kuwa vitabu hivyo vikitumika vitalisababisha taifa kufa kielimu kwa vile watoto watajifunza mambo ambayo hayana ukweli.Alitoa mfano wa kitabu cha Jiografia cha darasa lasita kilichoidhinishwa na EMAC ambacho kimekosewa kwa kuandikwa Jografia.
Vitabu vingine ni cha Hisabati cha darasa la nne katika ukarasa wa 49, ambapo imeandikwa sifuri gawanya kwa sifuri jibu lake nisifuri wakati jibu sahihi ni haiwezekani.Pia alisema kitabu cha Hisabati kingine kinaonesha 2x7=15 na kitabu cha Uraia pia kinaeleza kuwa mtaa unaundwa na vitongoji mbalimbali na kuongozwa na wenyeviti wa vitongoji.
Mbatia alihoji; Kama Rais Kikwete hivi karibuni akiwaMbeya alikiri kuwa elimu yetu ina udhaifu, kwanini wabunge wa CCM hamtaki kukubali hili?
Kimsingi alichozungumza Mbatia ni hoja Makini inayoonesha kukosekana kwa umakini wa kutosha katika wizara yetu ya elimu..