Papaa Muu
JF-Expert Member
- Nov 6, 2018
- 243
- 292
Ndugu zangu naomba tukumbushane yafuatayo:
Rushwa katika siasa hujenga mfumo wa Uongozi usio wazi na usiowajibika kwa wananchi husika:
----------------------------------
1. Rushwa huondoa uhuru wa mpiga kura.
Hapa mpiga kura hukosa uhuru wa kumchagua yule anayefaa, hivyo hujikuta akimchagua yule aliyemhonga.
Kiongozi aliyepatikana kwa kutumia rushwa hudharau wapiga kura maana huamini kuwa pesa zake ndizo zimemweka madarakani
2. Wagombea wenye vipaji na uwezo wa kuwakilisha hushindwa kushiriki kugombea katika uchaguzi kwa kukosa uwezo wa fedha.
Rushwa hupotoa maneno ya wenye haki na wenye sifa stahiki
3. Rushwa huharibu dhana nzima ya uwakilishaji kwa kuwa wanaochaguliwa hawana ridhaa kamili ya mpiga kura.
Siku zote viongozi wengi wanaopatikana kwa njia ya rushwa uwezo wao wakiuongozi ni mdogo sana.
Hivyo hupelekea wananchi kukosa watetezi stahiki kwa kipindi chote cha Uongozi
4. Viongozi waliochaguliwa kwa njia ya rushwa kamwe hawawezi kusimamia mapambano dhidi ya rushwa.
Hawa Wanakuwa ni viongozi wapenda dhuluma na wasiojali kusimamia haki
5. Rushwa husababisha usimamizi wa shughuli za Maendeleo kukwama Kutokana na vitendo vya ubadhilifu wa rasilimari za umma.
Kiongozi aliyeingia Madarakani kwa kutumia rushwa, lazima atataka kurudisha gharama zote alizotumia kuhonga pindi atakapokuwa madarakani,
hivyo kamwe hawezi kuhangaikia Maendeleo ya wananchi, bali atahangaika kurudisha pesa zake kwa kufanya ubadhilifu.
________________________________
LONGA NA TAKUKURU BURE.
Piga 113
SMS 113
Bonyeza *113#
---------------------------------
Mimi na wewe tuwe mstari wa mbele kabisa kuwapinga wagombea wote watakaotaka kutumia rushwa kupata madaraka.
Toa taarifa zozote sahihi zinazohusu mianya ya rushwa ili uchunguzi uanze haraka iwezekanavyo
Imetolewa na:
Jumuiya ya wanafunzi wanaopambana na kupinga rushwa ,
UDOSOAC ,
S.L.P 259,
DODOMA.
~Kyomo, bahati
Mwenyekiti-Shirikisho
________________________________
RUSHWA HUPOFUSHA MACHO, USIKUBALI KUWA KIPOFU
---------------------------------
Rushwa katika siasa hujenga mfumo wa Uongozi usio wazi na usiowajibika kwa wananchi husika:
----------------------------------
1. Rushwa huondoa uhuru wa mpiga kura.
Hapa mpiga kura hukosa uhuru wa kumchagua yule anayefaa, hivyo hujikuta akimchagua yule aliyemhonga.
Kiongozi aliyepatikana kwa kutumia rushwa hudharau wapiga kura maana huamini kuwa pesa zake ndizo zimemweka madarakani
2. Wagombea wenye vipaji na uwezo wa kuwakilisha hushindwa kushiriki kugombea katika uchaguzi kwa kukosa uwezo wa fedha.
Rushwa hupotoa maneno ya wenye haki na wenye sifa stahiki
3. Rushwa huharibu dhana nzima ya uwakilishaji kwa kuwa wanaochaguliwa hawana ridhaa kamili ya mpiga kura.
Siku zote viongozi wengi wanaopatikana kwa njia ya rushwa uwezo wao wakiuongozi ni mdogo sana.
Hivyo hupelekea wananchi kukosa watetezi stahiki kwa kipindi chote cha Uongozi
4. Viongozi waliochaguliwa kwa njia ya rushwa kamwe hawawezi kusimamia mapambano dhidi ya rushwa.
Hawa Wanakuwa ni viongozi wapenda dhuluma na wasiojali kusimamia haki
5. Rushwa husababisha usimamizi wa shughuli za Maendeleo kukwama Kutokana na vitendo vya ubadhilifu wa rasilimari za umma.
Kiongozi aliyeingia Madarakani kwa kutumia rushwa, lazima atataka kurudisha gharama zote alizotumia kuhonga pindi atakapokuwa madarakani,
hivyo kamwe hawezi kuhangaikia Maendeleo ya wananchi, bali atahangaika kurudisha pesa zake kwa kufanya ubadhilifu.
________________________________
LONGA NA TAKUKURU BURE.

Piga 113
SMS 113
Bonyeza *113#---------------------------------
Mimi na wewe tuwe mstari wa mbele kabisa kuwapinga wagombea wote watakaotaka kutumia rushwa kupata madaraka.
Toa taarifa zozote sahihi zinazohusu mianya ya rushwa ili uchunguzi uanze haraka iwezekanavyo
Imetolewa na:
Jumuiya ya wanafunzi wanaopambana na kupinga rushwa ,
UDOSOAC ,
S.L.P 259,
DODOMA.
~Kyomo, bahati
Mwenyekiti-Shirikisho
________________________________
RUSHWA HUPOFUSHA MACHO, USIKUBALI KUWA KIPOFU
---------------------------------