Madeni yakwamisha ujenzi JNIA

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Deni la mkandarasi kwa Serikali limesababisha ujenzi wa jengo la tatu la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kusuasua huku baadhi ya vifaa vikiwa vimekwama bandarini.

Mkandarasi huyo ambaye ni Kampuni ya Bam International ya Uingereza, anadai Sh21.4 bilioni huku mkandarasi mshauri akidai Sh1.8 bilioni na Sh279.7 bilioni zinadaiwa kwa ajili ya kukamilisha mradi huo, ambazo bado hazijapatikana.

Mradi huo ambao ulianza kujengwa mwaka 2013, unatakiwa uwe umekamiliaka Desemba mwaka huu.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Salum Msangi amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 66 mpaka sasa.
Kaimu Mkurugenzi huyo alimesema hayo jana kwenye ziara ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa aliyetembelea mradi huo.

Profesa Mbarawa amesema mradi huo utagharimu Sh560 bilioni hadi kukamilika kwake.


Chanzo: Mwananchi
 
Mradi unasimama vipi wakati kila mwezi tuna matrilioni tunayakusanya TRA??

Au basi hizo figures za TRA ni uongo..!!

Maana hata Tanesco haitakiwi kuhangaika na mkopo wa USD 200Mil World Bank wakati tunakusanya matrilioni TRA kila mwezi.

Serikali iipatie Project ya JNIA na Tanesco pesa.
 
Kulikuwa na sababu gani ya kukimbilia kujenga uwanja sijui wa kimataifa chato ? Hiyo pesa si ingemalizia kujenga hiyo terminal mpya pamoja na kurekebisha miundo mbinu ya viwanja vyetu vingine

Kujua kwingi ,mbele kiza
 
pesa ya kununua ndege moja kubwa iliyolipwa ingetosha kumaliza uwanja ambao wanataka dola milioni 250 tu ...
Pesa za kujenga uwanja chato aka "GBODLITE" zingetumika kumalizia uwanja wa ndege dar au hata mwanza .....
Kupanga ni Kuchagua....
 
Kwakweli project hizi mbili kusimama hii na ya Mwanza inasikitisha nilimwona Pro anaongea nilitamani nivamie television ile
 
Inasikitisha sana.... mimi huwa naishiwa maneno haswaa nikitafakari ni kwa jinsi gani kiongozi mwenye mapenzi ya dhati na chato pekee akaiepeleka Tanzania nzima mbele

Tumerudi hatua nyingi nyuma
 
Mkuu si alisema hizo Bilioni 500 kuna ufisadi, inakuaje tena waziri anasema hela ambayo mkuu alisema ni ufisadi.
 
Back
Top Bottom