Naasa nisikiani, ya lazima mabanati
Wamekuvisha vimini, hujuwi zao shuruti
Tayari umtihanini , epukeni ma afiriti
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Kukwita mi sitochoka , ile njia mustaqima
Nabaki nahuzunika , uendako sio kwema
Na mwenzako walimzika, sio maradhi ya homa
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Mary kwa sasa tunaye , amekuwa Mariamu
Kujichuna basi yeye, hijabu haishutumu
Mazurizuri mamboye, hanaye wa kumlaumu
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Azisikiza nyingi tepu, za walewale Ansari
Kumuona raha tupu , twajionea ufahari
Karaha ya lapulapu, kutupwa kwenye bahari
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Yule Ruth mwamkumbuka?, mmbeja wake Coheni
Nikabu yu ajivika, kitabu kipo mkononi
Cohen kasitirika, tunaye majalisini
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Wamekuvisha vimini, hujuwi zao shuruti
Tayari umtihanini , epukeni ma afiriti
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Kukwita mi sitochoka , ile njia mustaqima
Nabaki nahuzunika , uendako sio kwema
Na mwenzako walimzika, sio maradhi ya homa
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Mary kwa sasa tunaye , amekuwa Mariamu
Kujichuna basi yeye, hijabu haishutumu
Mazurizuri mamboye, hanaye wa kumlaumu
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Azisikiza nyingi tepu, za walewale Ansari
Kumuona raha tupu , twajionea ufahari
Karaha ya lapulapu, kutupwa kwenye bahari
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko
Yule Ruth mwamkumbuka?, mmbeja wake Coheni
Nikabu yu ajivika, kitabu kipo mkononi
Cohen kasitirika, tunaye majalisini
Mabanati yapimeni haya yangu mi matamko