PreGE2025 Mabadiliko wanayoyataka Watanzania ni kuwa katiba ambayo italeta tume huru ya uchaguzi na Wakurugenzi wa Halmashauri kutosimamia uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
7,170
Reaction score
8,622
Alichosema Mwanasheria mkuu wa serikali juu ya No reform no election sio sahihi.

Sababu mabadiliko ya sheria za uchaguzi yaliyofanyika 2024 hayajakidhi vigezo vya kuwa na tume huru ya uchaguzi.

Tume huru ya uchaguzi ni ka ile ya Kenya ambapo mwenyekiti wake hateuliwi na rais.

Uchaguzi hauwezi kuwa huru wakati wakurugenzi walioteuliwa na rais ndio wasimamizi na wasoma matokeo.

Kwa muktadha huu ni wazi kuwa tunahitaji mabadiliko ya katiba ili chaguzi ziwe huru.

Mmesahau alichowahi kusema kada wa CCM kule Mwanza?
 
Inaonekana huwa hamsomi hata vitu mnavyovipinga.
Sheria ya sasa imekataza wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Badala yake Tume Huru ya Uchaguzi itatafuta watumishi wa umma waandamizi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
 
Inaonekana huwa hamsomi hata vitu mnavyovipinga.
Sheria ya sasa imekataza wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Badala yake Tume Huru ya Uchaguzi itatafuta watumishi wa umma waandamizi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Mkurugenzi na mtumishi wa Umma mwandamizi tofauti yake nini sasa? Huyu mmoja katauliwa na raisi na wa pili kaajiliwa na serikali ya raisi, si mtu na binamu yake hao?

Tuache kutufanyia wajinga jamani, tunataka watu huru kabisa...!
 
Inaonekana huwa hamsomi hata vitu mnavyovipinga.
Sheria ya sasa imekataza wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Badala yake Tume Huru ya Uchaguzi itatafuta watumishi wa umma waandamizi kuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Wametoa Wakurugenzi wanewaweka Maofisa Waandamizi sasa swali langu kwako kuna tofauti gani kati ya Mkurugenzi wa Halmashauri na Afisa Mwandamizi wakati wote mamlaka yao ya nidhamu ni Rais ambaye ndo Mwenyekiti wa Chama cha Siasa kinachoshiriki Uchaguzi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…