Maaskofu mnaoleta siasa madhabahuni kumbukeni busara za mzee Makamba

Kuna watu mnamuandalia mazingira magumu sana Rais wa nchi hii na kibaya zaid na yeye ameshindwa kutegua huu mtego.
Naamini kwa kiasi kikubwa wote mnaomtetea na kutopenda aguswe wala kukosolewa mnafanya hivyo kwa ajili ya matumbo yenu tu na sio kitu kingine, nyinyi ni masalia ya Waafrika wasaliti. Ukitaka kujua nyinyi ni wanafiki kwa Rais basi rejeeni ya rafiki zenu wa Zimbabwe, hawa ndugu zenu walikuwa tayari kutoa roho ya mtu yoyote aliyethubutu kusema Mugabe ni mzee, wapo watu walifungwa huko kwa vitendo vyao vya kumuomba Mzee Mugabe aondoke au asiingoze nchi kifamilia na walipingwa na wakaitisha press kama zenu kumtetea Mugabe na hata kumuita baba wa demokrasia na mtetezi wa wanyonge kama mnavyomuita Rais Magufuli, lakini jambo la kustaajabisha siku jeshi lilipojaribu tu kumtisha Mugabe basi huwezi amini nchi nzima iliingia mitaani kumkataa Mugabe utafikri sio wale siku tatu zilizopita waliomshangilia Mugabe.
Nyinyi wote mnaokataa Rais asikosolewe kwa visingizio kuwa huyu ana mamlaka kutoka kwa Mungu hamumtakii mema na ni wasaliti wakubwa sana.
 
Si kwa povu hili...Lumumba mbona hamtulii... Na bado sindano zitawaingia tu
 
Umeandika mengi sana kudhihirisha ujinga kama siyo upumbavu wako.

1. Taasisi za dini ni mkono wa imani wa serikali kwa maana ya kuwajengea imani wananchi juu ya serikali yao. Na serikali zote msingi wake ni utaratibu unaoelekezwa na dini zote. Ndiyo maana kuna dini rasmi za serikal na watawala kuapishwa kwa imani za dini zao. Baadhi tumejiridhisha kuwa hapa kwetu dini rasmi ya serikali ya ccm ipo.

2. Kwenye biblia viongozi wa dini walitabiri anguko la serikali walipokuwa hawawatendei haki wanadamu viumbe wa Mungu. Watawala wa namna ile husababisha laana kwa nchi nzima kama hapa kwetu.

3. Kwa bahati mbaya sana nchi yetu imeshuhudia watawala wasio na hofu ya Mungu wanaodhulumu haki za raia viumbe wa Mungu kwa kukosa hekima na busara, hadi kuua au kujaribu kuua.

i. Bei za mazao kwa wakulima imekuwa kitendawili miaka yote kwenye nchi ya wakulima na wafanyakazi.

ii.Viwanda vimebaki mshangao haijulikani ilitokea nini na ifanyike nini zaidi ya kauli tata za awamu ya viwanda na uchumi wa kati.

iii. Mungu hapendi dhulma, mateso, mauaji na uonevu kwa viumbe wake kama namna tunayoshudia hivi sasa. Ni sawa kwa watumishi wote wa Mungu kuwaonya watawala ndiyo kazi yao ya kwanza.

4. Tupe takwimu za ukusanyaji wa kodi ulioongezeka. Mbona kimya hakuna taarifa?

Hoja yako haishangazi maana mafanikio ya shetani ni kuitia ganzi na upofu roho ya neema ya Mungu na kutoa ufahamu wa viongozi batili wasio na hofu ya Mungu hususan yanayofanywa na mtawala huyu.
 
Bora ziende mazabauni tu maana si asa mpaka 2020 sasa siasa ziende wapi ulitaka
 
Duh..jama
Mapovu yote haya kisa mtu kaambiwa atubu
Hahaha
Basi asitubu
Happy now?
 
Punguani mkubwa wewe, tutolee upuuzi wako hapa,jibu hoja za maaskofu kwanza, kamawaliyosema ni uongo au la?
 
Andiko refu kulimaliza nimeshindwa kwa sababu limejaa upumbavu na ujinga mwingi hebu mtoa mada nenda katubu huenda ukarudi kuandika vitu vya maana
 
we una laana huyo lowasa unahangaika nae una Evidence yoyote kwamba ni mwizi Acha kunyoosha mdomo wako kama mademu wa mipasho au wewe ni wa mipasho na udaku!?
 
Huyu jamaa amejiandaa na kuandika maneno meengi unfortunately it is rubbish like human manure!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…