Maandamano hayaepukiki kipindi hiki

Maandamano hayaepukiki kipindi hiki

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Demokrasia ina gharama zake, kuzuia maandamano katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ni sawa na kusema kuwa kuwe na mvua za masika lakini kusiwe na mbu hata mmoja.

Shuhuli za kila siku za wananchi ni lazima ziingiliane na shughuli za kidemokrasia wakati wa uchaguzi kama vile kujiandikisha kupiga kura, uhakiki wa majina, mikutano ya kampeni, na zoezi la kupiga kura. Hata misafara ya Rais inakopita huwa inasababisha pia shuhuli za kawaida za wananchi kuathirika, na hiyo ndiyo gharama ya demokrasia tuliyoichagua sisi wenyewe.

Polisi wetu wanapozuia maandamano ya vyama vya siasa sio sawa, kwasababu huu ndio msimu wenyenye wa wananchi kukusanyika kwa shuhuli za kidemokrasia. Kazi ya polisi wetu katika kipindi hiki ingekuwa kutoa maelekezo na kusimamia namna mikusanyiko hii mikubwa ya wananchi itakavyopaswa kuwa salama lakini sio kujali malalamiko ya watu wanaoingiliwa shughuli zao za maisha kwasababu ya mikusanyiko ya vyama katika kipindi hiki kifupi maalum cha uchaguzi mkuu wa kila baada ya miaka 5. Hata bila ya maandamano haya ya wafuasi wa vyama vya siasa wako watu ambao wamewahi kuchelewa usafari, matibabu, kazini, sokoni, n.k kwasababu ya kuzuiwa na misafara ya viongozi wakuu wa kisiasa inapopita na migomo ya wafanyakazi, madereva au wafanyabiashara, lakini sijawahi kusikia polisi wakisema kuanzia leo misafara mirefu ya viongozi, migomo ya wafanyakazi, wanafunzi, madereva, wafanyabiashara au maandamano kwenye makongamano mbalimbali marufuku kwakuwa vyote hivi huwa vinaingilia shuhuli za wananchi wa kawaida. Hii ndio gharama ya demokrasia bana.

Polisi inapowazuia watu wasikusanyike kwa namna wanayotaka wao inasababisha watu wajiulize maswali mengi kama vile "ni kwa manufaa ya nani?" kwababu wanaoandamana ni wananchi na kazi zinazovurugwa ni za wananchi haohao, na muda, siku, eneo na sababu za kuvurugika zinafahamika pia, sasa ni nani wamelalamika? wapi? na wako wangapi?. hata kama watu hao wapo jibu lao lingekuwa kuvumilia kipindi hiki kifupi cha uchaguzi kiishe na kazi zao zitarejea kama kawaida baada ya uchaguzi kupita, sio kuwaridhisha kwa kuzuia maandamano kama "polisi" wanavyotaka ieleweke kwa wananchi.

Kipindi kama hiki ni kipindi ambacho kinavuruga shuhuli za wananchi duniani kote, hivyo haiwezi kuwa tofauti hapa Tanzania. Duniani kote hiki ni kile kipindi ambacho likizo zote za askari zinasitishwa na askari wastaafu wote wanarudishwa kazini ili kulinda usalama wa watu na mali zao katika misafara na mikusanyiko ya watu, lakini sio kuzuia maandamano kama walivyotangaza jeshi la polisi.

Mwisho wa ubaya ni aibu. Watanzania wote tunaongea kitu kilekile "maisha bora kwa kila mtanzania" lakini kwa lugha tofauti. Wewe kuwa polisi haipaswi kukufanya usione uchungu wizi wa pesa kama zile za escrow ambazo zingeweza kusogeza maisha ya shangazi yako kule kijijini kama zingewekezwa kwenye upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwenye zahanati zetu vijijini, hupaswi kusahau kuwa ukistaafu nawe utakwenda kuishi maisha ya kawaida sehemu isiyokuwa na maji ya kufulia. Yatupasa sisi sote tuchanganye na akili zetu kwa kila jambo.
 
unaweza kujiuliza wakati tume ya uchaguzi inatangaza kuwa ni ruksa kwa wagombea kwenda na wapambe wao walitegemea nini? walijua watapita wapi? hii serikali ya kukurupuka hii
 
Tatizo sio maandamano,shida ni kwamba Lowasa kamfunika Magufuri,ili kukwepa aibu bora yasiwepo kwa wote na hii imelenga kuzuia Lowasa asiendelee kutajwa kila siku kwani hali ilivyo kila mtu mjini hadi vijijini wanataka kumwona na kumwongelea Lowasa,Makufuri katoweka kabisaa,ni mbinu za kuibeba CCM,bahati mbaya wamechelewa,LOWASA tayari ni trade mark!
 
Tatizo litakuw kubwa zaidi kwa Ccm maana wao wamekosa mwamko, kwa kuzuia maandamano ambayo pia Ccm inawapa pesa, bado ni shida kwao. Hata wale wa kununua sasa hawataonekana tena. Nashauri wapige pia marufuku kampeni tufanye uchaguzi, labda Ccm watapona
 
Nadhani we are making progress. Tulianza na kupeleka mgombea wetu kwa maandamano. Wakatokea watu watano na mgombea wetu alianza nao safari na akajitia uchizi kwa kutabasamu njia nzima na kuwapungia jamaa zake aliokuja nao toka mwanzo hadi mwisho. Akaja huyu mwingine wananchi wakajitokeza mpaka mji ukasimama, imekuwa shida!

Tukafuatia kumtambulisha mgombea wetu nchi nzima, tena kwa gharama za serikali na jasho la walipa kodi wote bila kujali vyama vyao. Sasa baada ya kuona hali, huyo mingine hapana kukusanyika! hata fomu rudisha peke yako, kimyakimya. Kwani what happened to freedom of association? Na hizi sheria zinazotumiwa na polisi ni sheria gani? maana sijaona hata sheria moja inayoruhusu polisi kuzuia mkusanyiko! Na hata kama zingetengenezwa hizo sheria, ni sheria za aina gani zinazokiuka katiba? Kwani taifa hili ni taifa la watu wa aina gani?

Sasa tumefikia hatu ya kishetani. Hata kwenye msiba usifuatane na mtu. Marehemu tutampangia idadi ya watu wa kumzika, tutampangia na watu wa kumzika! Hii ni ajabu!
 
Acha kuhangaika na chama kinajoelekea kuzimu,mimi binafsi nilishakilaani laana yenye sababu nyingi, hivyo lazima iwapate kama Bwana wangu aishivyo.
 
Aroo hayo majitu yakiandama...yaarestishe yote....
Yakireta ujeri PT
 
Nadhani we are making progress. Tulianza na kupeleka mgombea wetu kwa maandamano. Wakatokea watu watano na mgombea wetu alianza nao safari na akajitia uchizi kwa kutabasamu njia nzima na kuwapungia jamaa zake aliokuja nao toka mwanzo hadi mwisho. Akaja huyu mwingine wananchi wakajitokeza mpaka mji ukasimama, imekuwa shida!

Tukafuatia kumtambulisha mgombea wetu nchi nzima, tena kwa gharama za serikali na jasho la walipa kodi wote bila kujali vyama vyao. Sasa baada ya kuona hali, huyo mingine hapana kukusanyika! hata fomu rudisha peke yako, kimyakimya. Kwani what happened to freedom of association? Na hizi sheria zinazotumiwa na polisi ni sheria gani? maana sijaona hata sheria moja inayoruhusu polisi kuzuia mkusanyiko! Na hata kama zingetengenezwa hizo sheria, ni sheria za aina gani zinazokiuka katiba? Kwani taifa hili ni taifa la watu wa aina gani?

Sasa tumefikia hatu ya kishetani. Hata kwenye msiba usifuatane na mtu. Marehemu tutampangia idadi ya watu wa kumzika, tutampangia na watu wa kumzika! Hii ni ajabu!

Your so concious...... keep it up!!!
Kama wakiendelea kushupaza shingo watavunjika
 
Uko sahihi sana ndugu. Uppuzi huu unaona hapa bongo tu. Kwa kuwa misafara mingine ni minene sana kuliko ile ya kwetu hivyo basi njia bora ni kuzuia maandamano. Hii haikubaliki kabisa. Wote tukatae.
 
Kila Jambo Na Wakati Wake Na Wakati Ukifika Utimia Pasi Na Kikwazo
 
ccm washakuwa bongo lala , mipango yote intoka kwa Nazi nape unategemea nini hapo. nape kila siku alikuwa anamtaja Dr. Slaa, sasa zoezi kinywani limeamia kwa Lowassa.
 
kiujumla kauli ya jana ya jeshi la polis kuzuia maandamano imenishangaza sana. polis wamekwepa wajibu wao wa kikatiba kabisa. hili halikubaliki kamwe..
 
Back
Top Bottom