maajabu ya tuzo za mwanaspoti

maajabu ya tuzo za mwanaspoti

Jospina

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2013
Posts
2,421
Reaction score
1,395
pamoja na lengo zuri walilonalo bado mwanaspoti wameonyesha mapungufu makubwa sana katika utoaji wa tuzo zao, haya ni baadhi ya mapungufu

1. mpaka sasa hakuna vigezo maalumu vilivyotumika kumpa Niyonzima uchezaji bora na kuwazidi Themi, Kiemba N.K.Niyonzima hakuwa mfungaji bora, hakuwa ni mtu aliyetoa assist nyingi, hakuwa ndo mchezaji mwenye nidhamu, hakuna kitu chochote special/ viable unachoweza kukitetea hadharani kwanini Niyonzima ni mchezaji bora

2. Mchezaji Joseph Kimwaga kapewa tuzo ya mchezaji bora chipukizi wakati msimu uliopita hakucheza mechi yeyote ya ushindani?? Sasa inakuwaje leo Joseph Kimwaga anakuwa mchezaji Bora Chipukizi??
Je alicheza michezo mingapi ya ligi na ya kiushindani??

Au wameangalia alipoifunga #Yanga tu basi ndio bora wakati wapo wengi tu waliocheza mcmu uliopita.
Ila bora kwang kwa upande wa Chipukizi ni Ramadhan Singano a.k.a Messi.

3.Kimechaguliwa Kikosi bora cha wachezaji 11 wa Ligi Kuu ya Vodacom(VPL) msimu uliopita lakini wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Congo wamejumuishwa ndani yake. hawa jamaa msimu uliopita walicheza timu gani ya Tanzania??

ushauri wangu: wanapochagua wachezaji bora wa ligi kuu, waache kutupumbaza na sms, kutegemea sms wachezaji kama Themi, Mwagane yeye itakuwa ngumu sana kwao kuchukua tuzo kwasababu wao hawapo simba au yanga zenye mashabiki wengi! jopo la makocha wa timu wanaoshiriki ligi kuu, wahariri wa magazeti ya michezo ndio washiriki katika kuchagua na viable criteria ziwe wazi kabisa

am sorry
 
Kwa upande wa Niyonzima naweza nikawatetea kidogo, uyu jamaa alikuwa na msimu mzuri kama nakumbuka alifunga magoli muhimu kueleke mechi za kuamua bingwa, alicheza mechi nyingi kama mchezaji tegemeo, ata kiemba pia alikuwa na msimu mzuri sema kwasababu timu ilimaliza vibaya ndo maana kakosa. Kwa kimwaga na 11 bora nadhani wamechemka
 
Kwani Canavaro wa Italy alikuwa michezaji bora wa dunia 2006.Naye alikuwa mfungaji bora?ndiyo unashangaa kwa Niyonzima (Fabregas)?
 
[h=5] kaseja copy.png ndio bongo hii...[/h]
 
hapo kwa Samata na Ulimwengu ndio pameniumiza kichwa
 
Niyo ni sawa, but nakubaliana na wewe na vipengele vyote vingine
 
Mwanaspoti wanaweza wasiwe sahihi kwenye uteuzi wao kwa sababu zilizotajwa. Lakini sisi wananchi ndio wenye kasoro zaidi kwa kutuma sms bila ya kuhoji hayo mwanzoni, na tulioona hayo yakifanyika bila ya kutuma sms wala kuikosoa Mwanaspoti mpaka baada ya uteuzi. Tafsiri ya karibu ni kwamba tuliziona kasoro hizo, lakini tukajiingiza kutuma sms kwa imani kwamba wachezaji tuliowapenda ndio wangeshinda; sasa hawakushinda ndio tunalalamika. Tulipaswa kuhoji vigezo kwanza kabla ya kushiriki kupiga kura.
 
Mwanaspoti wanaweza wasiwe sahihi kwenye uteuzi wao kwa sababu zilizotajwa. Lakini sisi wananchi ndio wenye kasoro zaidi kwa kutuma sms bila ya kuhoji hayo mwanzoni, na tulioona hayo yakifanyika bila ya kutuma sms wala kuikosoa Mwanaspoti mpaka baada ya uteuzi. Tafsiri ya karibu ni kwamba tuliziona kasoro hizo, lakini tukajiingiza kutuma sms kwa imani kwamba wachezaji tuliowapenda ndio wangeshinda; sasa hawakushinda ndio tunalalamika. Tulipaswa kuhoji vigezo kwanza kabla ya kushiriki kupiga kura.

unachosema ni sahihi watu wengi wamepiga kura kwa mapenzi na si kwa kuangalia vigezo
 
Back
Top Bottom