Lowassa, si usaidie na masikini


Mkuu, hili nalo neno!
 
Nadhani wewe mleta mada umesahau kuwa Lowasa ni mwanasiasa. Kwa wale watu wengine wa dini wangesema kuwa Lowasa hakuitwa ili afanye hayo uliyoyasema.
Yeye anatafuta namna ya kuwatumikia watu .
Na anapoombwa kuchangia basi anachangia kwa uwezo wake wote bila ubahili kama wengine wanavyotoa kibahili kwa kuwaza kwamba tusipopata kura tutapoteza.
Lowasa angeenda peke yake Zanzibar angeambiwa kuwa ameandaa lile tamasha yeye na bila shaka Dr. Shain angekua kwenye misukosuko ndani ya Chama chake toka kwa Nape akisukwa na Membe.

Lowasa leo hii akaenda kutoa msaada kwa Yatima bila kualikwa tena akiwa na wenzake kama ilivyofanyika kule Zanzibar basi ni dhahiri kuwa hicho kituo cha kukelea yatima kitafungwa kwa shinikizo la Nape na kundi lake.

Tumeona mfano watu wanaomuunga mkono kwa kujitolea damu kusaidia wagonjwa walivyopigwa marufuku kwenye hospitali za serikali.
Unataka asidie nini tena wakati akisaidia hata kwa marafiki zake kutoa damu kuwaokoa wanawake wakati wa kujifungua inakua ni vitisho kwa madaktari wakuu wa hospitali husika.

Leo hii unakuja na hoja dhaifu ya kusaidia yatima bila kuangalia kitakachotokea na vita anayopigwa mpaka kuombewa kifo na watu kushangilia wanaposikia kuwa anaumwa.

Mwacheni mzee wa watu.
Kama mnataka washaurini wanaoniliki vituo vya mayatima wajipange wawaite wanasiasa wote maarufu ikiwemo wapinzani ili wachangiwe kwa pamoja na kuondoa kelele za kina Nape na wanafiki wengine.
 
Ukitaka kujua kuwa huyu jamaa ni hana hutu nenda jimboni kwake ndio kuna ombaomba Arusha nzima na hana hata hutu angekwenda kusaidia hata wale wagonjwa wa Seriani.


swissme

hutu ndio nini mkuu?
 

Mbona Pinda et tal wametoa mil 203 umeona kawaida lakini ka milion 50 ka Lowassa kanakutoa mapovu!
 
 
Huyo mzee hana shida nakuwasaidia maskini wa TZ!shida yake ni uraisi!anasaidia either kikundi,vikundi na mtu mmoja mmoja kukamilisha ndoto yake na si vinginevyo!huyu Bwana mkubwa kashatuona wa TZ tuna price tag?anachofanya nikuona kwa pesa zake chafu ambazo kuna siku!mungu aepushilie mbali itabidi azitolee maelezo?anaamini katika kununua,hatufai hata kidogo!zaidi ya kuwafaa mafisadi wenzake na kuendekea kuuza rasilimali za nchi hii!tumuogope kama ukoma!hajawahi kusafishwa wala kujisafisha katika kashfa hata moja,hafai,hafai na hatafaa si kwa masika bali hata kiangazi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…