Lowassa kwenye sherehe za muungano!!!

Je sumaye Msuya warioba.... Hawakuwapo? Anyhow ninachojua anaweza kuondolewa NEC lakini bado akawa mstaafu (Kama kweli alistaafu..,, see MZee Jumbe)
 
Walitajwa officially na Msekwa tena ndani ya kikao cha NEC nakumbuka Kikwete alisema kwanini hamuwataji ndipo Msekwa akasimama na kusema wanaotajwatajwa ni Rostam Lowassa na Chenge baada ya hapo RA akasimama na kusema hizo ni tuhuma tu, Rutunga upo.
 
Jamani, kuhudhuria kwa Lowassa sio kosa kwani bado ana nafasi hadi atakapoamua kuachia madaraka au atakapotolewa.
 
Siku Lowasa akifukuzwa CCM hiyo ndiyo itakuwa mwisho wa CCM. Maana kitakacho tokea ni:

1. Mgawanyiko ndani ya chama kutokana na ukweli kuwa Lowasa anakundi kubwa sana nyuma yake na anaungwa mkono sana na
baadhi ya wana ccm ambao aliwasaidia sana ndani ya chama.

2. Mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania itachukizwa na kitendo hicho kiasi kuwa huenda wataweka kisasi ili kuwaadhibu ccm, na
ieleweke wazi kuwa mikoa ya kaskazini ina watu wengi wenye hali nzuri kiuchumi hivyo hawawezi kutishwa na ccm kwa namna
yeyote ile.

3. Kuna uwezekano Lowasa na wenzake watakao enguliwa wakatumia ushawishi wao, kumuunga mkono mgombea wa ccm
(2015) ambapo watahakikisha anaingia na kushika nchi, hili likitokea bado gamba la ccm litakuwa sio gamba bali ni jiwe.
 

Wishful thinking....Lowasa hawezi athiri chama Cha Magamba....akifukuzwa ndo mwisho wake.....
 
Siku Lowasa atakayofukuzwa ndani ya ccm nihakika patachimbika Lowasa ananguvu kubwa kwenye kila idara na siasa anaijua, ukimya wake usije ukachukuliwa kuwa ndiovyo alivyo. CCM inajaribu kutibu majeraha kwa pilipili, ninahakika hawatanawa mikono watajisahau na kujishika macho hili likitokea ni dhahiri mateso yatabaki kwao. Hata hivyo swali langu kubwa kwa ccm ni kuwa hawa wakina Lowasa na wenzake wanaeleweka na wanawafahamu vizuri, ni kwanini wasiwafikishe mahakamani ili pamoja na kuenguliwa chamani lakini waadhibiwe kwa mujibu wa sheria? huku kulindana ni kwa aina gani jamani? inamaana mhasibu akiiba pesa dawa ni kufukuzwa sio kufungwa?
 
kwa kufuatilia kwangu jana zile sherehe white hair aka EL jana kwanza alikuwa kauchubua peke yake hajafungamana na mtu yeyote then alipokuja mkuu wa kaya sidhani kama walipeana mikono sina uhakika kwani walipokuwa wameingia viongozi wengine kama mzee ruksa white hair alishuka pale alipo kuja kuwapa hi,lakini mwisho wa siku Magamba hawamuwezi huyu jamaa walishajisahau wenyewe kumuacha atambe sasa wanashindwa kumdhibiti.......:smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…