Mbonica VJ
Member
- Sep 27, 2012
- 76
- 43
Ni karibu miezi 32 sasa, Edward Lowassa amekuwa agenda kuu ndani ya CCM na wanaccm wenyewe, si mwenyekiti wala mjumbe wote mioyo yao ni Lowasa tu, wengi wakitaka ajipambanue nakuwa nyota huru ya chama na wachache walio juu ya chama wakitaka kumpoteza kisiasa gwiji huyu wa siasa za ukwasi na fitina msonge!
Ikumbukwe kuwa doa kuu linalotajwa kuwa Lowasa ni fisadi ni Richmond, lakini nani asiyejua richmond ni nani na ilikuwaje? Pale dodoma Lowasa ameweka wazi mbele ya Mwenyekiti kuwa hakuna kilichotendeka ambacho mwenyekiti hakukijua ama kumtuma! Narudia tena UCHAFU wa LOWASSA ni RICHMOND tu!
Nauliza tena RICHMOND ni nani? Mwenyekiti alijibu nini siku ile pale Dodoma wakati Lowassa anamhoji zaidi ya kuinamisha kichwa chini hali iliyopelekea BWM kumtuliza Lowasa?
Sasa Lowassa anakitaka Chama na anataka agombee urais 2015 na ameshashinda ndani ya Chama na nusu uwanja nje ya chama, shime ccm, ili muendelee kuitwa chama cha siasa japo mtakuwa wapinzani zuieni jaribio la baadhi ya wanachama wenu la kujaribu kumzika Lowassa kisiasa angali amefanikiwa kukibeba chama!
Kuna juhudi za kitoto ndani ya CCM eti wapo kwenye harakati za kumuuandaa cijui nani kugombea Urais 2015, wanatumia raslimali za nchi kujijenga kisiasa kwa upinde wa mvua ya siasa!
Chondechonde mwenyekiti wa CCM Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, Amini Lowassa ndie chaguo la wanaccm wote hata hao wanaokusikiliza na pia wapo kila hatua ya maendeleo ya Tanzania na wewe pia na wao mioyo yao ipo kwa Lowassa!
Mwenye USHAHIDI wa wazi juu ya UFISADI wa Lowassa aulete hapa, sio stori za kulishwa vijiweni kisha mnakuja hapa kupiga ngonjera ooho Lowasa fisadi, oooho sijui nini! Leteni utetezi hapa au mfikisheni mahakamani!
Mimi nitampa kura yangu ikiwa atagombea hata kama hatoshinda, lakini atakinusuru chama kufutika kabisa duniani!
Ikumbukwe kuwa doa kuu linalotajwa kuwa Lowasa ni fisadi ni Richmond, lakini nani asiyejua richmond ni nani na ilikuwaje? Pale dodoma Lowasa ameweka wazi mbele ya Mwenyekiti kuwa hakuna kilichotendeka ambacho mwenyekiti hakukijua ama kumtuma! Narudia tena UCHAFU wa LOWASSA ni RICHMOND tu!
Nauliza tena RICHMOND ni nani? Mwenyekiti alijibu nini siku ile pale Dodoma wakati Lowassa anamhoji zaidi ya kuinamisha kichwa chini hali iliyopelekea BWM kumtuliza Lowasa?
Sasa Lowassa anakitaka Chama na anataka agombee urais 2015 na ameshashinda ndani ya Chama na nusu uwanja nje ya chama, shime ccm, ili muendelee kuitwa chama cha siasa japo mtakuwa wapinzani zuieni jaribio la baadhi ya wanachama wenu la kujaribu kumzika Lowassa kisiasa angali amefanikiwa kukibeba chama!
Kuna juhudi za kitoto ndani ya CCM eti wapo kwenye harakati za kumuuandaa cijui nani kugombea Urais 2015, wanatumia raslimali za nchi kujijenga kisiasa kwa upinde wa mvua ya siasa!
Chondechonde mwenyekiti wa CCM Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, Amini Lowassa ndie chaguo la wanaccm wote hata hao wanaokusikiliza na pia wapo kila hatua ya maendeleo ya Tanzania na wewe pia na wao mioyo yao ipo kwa Lowassa!
Mwenye USHAHIDI wa wazi juu ya UFISADI wa Lowassa aulete hapa, sio stori za kulishwa vijiweni kisha mnakuja hapa kupiga ngonjera ooho Lowasa fisadi, oooho sijui nini! Leteni utetezi hapa au mfikisheni mahakamani!
Mimi nitampa kura yangu ikiwa atagombea hata kama hatoshinda, lakini atakinusuru chama kufutika kabisa duniani!