Mkuu
Wanamkakati wa Lowassa ima ni wachanga katika fani au hawajui nini cha kufanya. Hilo ndilo limemuengua edo mapema
1 Alinza kampeni za chini chini kwa mtindo wa mtandao wa 2005 akidhani mbinu hiyo haijulikani.
2. Akaendesha kampeni kabla ya muda, na kutoa muda wa wabaya wake kutafuta mahali pa kumshika
3. Akaamini nguvu ya senti zaidi ya nguvu ya hoja. Kaacha kiporo cha Richmond bila kujua kitakuwa ni tatizo
4. Aliamini anaijua system ya CCM, akapanga CC, NEC akijua mkutano mkuu ni kumalizia. Hakujua kamati za maadili na ile ya wazee wa chama zina nguvu kiasi gani. Aliamini shinikizo kupitia NEC linatosha kumvusha. Kosa
5. Mpango wa wadhamini uliendeshwa kitoto. Team iliamini watu wengi wangezuia kukatwa jina.
Hawakujua kuwa wanachama waliotakiwa ni 450.
Mbinu ya watu wengi ilikusudia kufunika matatizo ya Richmond kwa kuonyesha anakubalika licha ya matatizo aliyo nayo.
Kosa lilomgharimu
Kwa ufupi team nzima iliongozwa na mkakati usiokuwa na uhalisia. EL alitakiwa kwanza ahakiishe anamaliza Richmond.
Yaani akabiliane nayo kiasi watu wampe benefit of doubt. Alichokifanya kiliongeza wasi wasi hata kwa aliyekuwa upande wake.
Akaajiri watu wasiojua kazi katika media na blog, badala ya kumpaisha watu hao wakwa chanzo cha kukumbusha vidonda
Tumesoma mitandaoni na JF vijana wakija na hoja tu bila kujua wanatetea nini. Hawa vijana walimuumiza sana.
Team EL ilidhani kuwa na watu kila chombo na kila blog ingesaidia sana. Hawakujua kuwa ni lazima watu hao wawe effective, hata kama ni watu 3 wawe na uwezo wa kujenga hoja na kuzitetea.
Tumeshuhudia vijana wake waliburuzwa na hilo lilikuwa doa kwa mzee. Watu walipata habari zaidi ya walizojua kupitia '' anafaa, amejenga shule, ni mfuatailiaji etc'' huku akibomelewa vibaya na wenye weledi
Angalia, Membe alikuja kupangua Libya dakika za mwisho. Alikabiliana na ukweli na ilimsaidia kimkakati
Richmond, mipango mibovu, kutotumia watu wa mkakati ndivyo vimemuangusha.
Pesa inafanya kazi ikiwa na mkono mwingine, haifanyi kazi ikigawanywa kama njugu
Pigo alilokutana nalo ni kama lile la Sitta. Wote sasa ni majeruhi wa CCM na ndio mwisho wa safari ya kisiasa.