LOWASSA: Arusha pagumu!

mimi sioni UGUMU wa kujivunia kwa Arusha kama Mwenyekiti wa Jiji anatoka CCM.Hii inaonyesha madiwani wengi ni wa ccm.X
hapo ndo ujiulize madiwani wa ccm ni wengi lakini haipendwi Arusha.jibu nadhani unalo:wizi wa kura uchaguzi mkuu 2010.
 
Arusha ni pagumu kweli kubadilika kwani bado wapo wengi kwao kuvaa nguo ni mwiko
 
Moderators, naomba muwe makini aisee tunahitaji JF kama ile ya mwanzo miaka ile, hii tabia ya watu kuvuruga mada za watu naomba muiangalie kwa umakini zaidi. Yani mtu anadakia mada kwa matusi na kejeli.

Back to topic
Inapendeza kama EL anautambua ukweli namna hiyo. Kwanini hakupewa maandalizi ya kichama na EL anatambulika namna iyo?.Sitaki kuamini kama wanahujumiana wao kwa wao.


cc Pasco
 

Huu ni upu. mbavu na ni kielelezo cha kufikia ukomo wa kufikiri, kutafakari na kung'amua njia mahsusi ya kupambana na ukosefu wa ajira kwa vijana.
Mi hainiingii akilini kamwe kuzifanya pikipiki kuwa ndo mkombozi ama utatuzi wa tatizo la ajira nchini. Kila uchao ajali za bodaboda zinaongezeka na kupoteza maisha ya vijana wetu na hata wengine kubakia na ulemavu wa kudumu.......Hawa wanaopoteza maisha yao na viungo vyao ni nguvu kazi hii tunaipoteza.

Badala ya kuentertain pikipiki kuwa chombo cha kubeba abiria (naamini hairuhusiwi kisheria), kwa kuwapa pikipiki na kuwapongeza kufanya hivyo, serikali ilipaswa kuboresha sekta ya kilimo, viwanda ili vijana hao waelekezwe huko kwa manufaaa yao binafsi na taifa kwa ujumla.
BIASHARA YA BODABODA HAINA MASLAHI KWA VIJANA NA TAIFA, HAINA FUTURE!
TUACHE KUTOA MAJIBU MEPESI KWA MASWALI MAGUMU YANAYOTUSIBU KAMA TAIFA......T
BODABODA SIO JIBU SAHIHI KWA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA.
WAENDESHA BODABODA NI JESHI LINGINE TUNALITENGENEZA HILI.

 

Uuzushi huu mchana kweupe SOURCE mimi mwenyewe nipo arusha kwa sasa narudi DAR leo ijioni
 
Dhambi hii ya Ccm kutumia polisi kuua watu wasio na hatia ita wamaliza milele hadi mtakapo tubu dhambi hii hadharani.
Kama mnaua watu mnategemea kutawala nini? Hii nk siri tuu nimewapa ili mjue no kwanini hampendwi hapa Arusha.
 

Lowassa ni kinara wa kufanya Arusha iwe ngumu dhidi ya CCM baada ya 2005 kutumia pesa nyingi kuhakikisha mgombea wake (Batilda) anateuliwa na CCM na hatimaye kuwa mbunge we Arusha. Alishirikiana na Yusuf Makamba, kuna kashfa hadi za kutengeneza kadi feki za CCM ili Batilda ashinde uteuzi ndani ya Chama ndipo ilibidi kufanyike uasi na kuipata ushindi Chadema ambayo nayo imeyumba, kila mkutano inasomba watu kutoka Karatu, Hai na Arumeru kujaza uwanja. Ndiyo ukweli, hutaki unaacha lakini utashuhudia ukweli huo mwenyewe 2015.
 
Last edited by a moderator:
mimi sioni UGUMU wa kujivunia kwa Arusha kama Mwenyekiti wa Jiji anatoka CCM.Hii inaonyesha madiwani wengi ni wa ccm.X

Nipatie idadi ya madiwani wa ccm, na madiwani wa chadema arusha, kisha zile kata tano zilizowazi tunajua ni za chadema jumlisha nazo halafu ndipo uje na huu upuuzi wako hapa. Mmeogopa kuitisha uchaguzi kwasababu mnajua kuwa huyo Meya wenu wa kuchonga hatakuwepo tena kama madiwani wote watakuwepo. Wekeni mpira uwanjani muone kazi
 

Kesho tu tatasikia Lowasa anaikana hii kauli, maana ni kweli itakuwa lazima amesema ila anaogopa wakisikia wenye ccm watamjia juu, kwa hiyo lazima ataikanusha na kusema wameinukuu vibaya
 
Nasubiri thread yako kuhusu swala la filamu ya Maudodo

Mkuu mara yakwanza kuangalia filam hii ya maudodo nilijua wanaongea kiswahili real kukaa makini kumbe wamelishwa maneno bhanaaaaaa......
 
Nadhani akaandae bahasha za kutosha kwa ajili ya 2015, kuwahonga wananchi. Maana penye uzia, penyeza rupia.
 
jamaa anacheki mpango wa urais maana Mipango ingine imebuma
 

Ninakubaliana na wewe kwa asilimia 100%. Huu ndio ushahidi wa wazi (of course kwa watanzania wenye uelewa) jinsi watawala wetu (CCM) ama walivyo na uelewa mdogo (akili ndogo) au kwa makusudi wanafikiri watanzania wote ni misukule wanaweza kudanganywa kwa peremende (kumbuka ile picha ya Mhe Jk akiwa kwenye Benz ya state akimpatia mtoto wa mtaani peremende). Walianzisha shule za sekondari za kata ili kuwadanganya watu kuwa watoto wanapata elimu ya sekondari wakati hivyo ni vituo vya kukuzia vijana. Vijana hao hao wamejianzishia usafiri wa bodaboda baada ya watawala kuwa na sera madhubuti za huduma salama na za uhakika za usafiri wa umma. kwa akili zao mbovu wanataka tuwashangilie kuwa bodaboda ndio ajira ya vijana wakati sio tu jeshi lingine bali ni machinjio ya uhai wa vijana na wateja wateja wao. Walivyokuwa na akili mbovu, usishangae siku moja kusikia mmoja wa magambas akipendekeza kuwa bodaboda iimarishwe kama usafari wa wanafunzi!
 
Mie nimehoji na kuomba mtazamo wa Wana JF juu ya ukimya usio wa Kawaida wa vijana wa Lumumba hasa Ritz na @Nnape Nauye kutosema chochote juu ya sakata la sinema ya Lwakatare. Inamaanisha nini?

Mkuu mtazamo utoke wapi wakati mdudu 'METADATA' kaisha tumbukiza nyongo kwenye mchongo mzima?
 
Huyu angeenda kufuga ng'ombe na kutumbua pesa za ufisadi kabla hatujamtafuna...ni kati ya niwatamanio siku kikinuka bongo!

Wewe kweli huoni alama za nyakati, yeye anakiri kwa sababu kwanza anajiamini pili ni teyari ni baba wa wote yaani ndie President wa Tanzania 2015 hutaki hama nchi
 

Subutu! CCM ikisimamisha Lowassa na ndivyo ilivyo kwa un President 2015 ndio mwisho wa Chadema Arusha, haitapata hata kura moja achilia mbali diwani mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…