Logitech Speakers Vs Samsung TV

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,146
Reaction score
7,676
Wakuu habarini.

Majuzi nilinunua Speaker za Logitech 5.1 hizi speaker mwisho zina pins 3 (Nyeusi, Orange na Kijani) hizi Pins zina Size ya pins za PC headphones / EarPhones.

Halafu nikanunua Smart TV Samsung 65 nch 4k QLED. Hii TV hiana Sehemu ya Kuconnect Hizo Pins za Logitech Speaker kupata Sound. Hii TV ina Port 3 Nyekundu, Nyeupe na Njano zile za Kawaida ambazo hizo Pins za Logitech zina Fiti kuingia lakini hazitoi sound, Na Ina Sehemu ya HDMI.

Niliamua kununua ARC yenye HDMI kwaajiri ya Ku connect bahati mbaya hiyo ARC matundu yake zile PINS za Logitech zinakuwa Kubwa na Hizwezi kuingia.

Ni kifaa gani nikinunue ili niweze ku connect TV yangu yenye HDMI na Hizi Logitech Speakers 5.1?

Msaada Tafadhali.
 
Nunua vifaa vinavyoendana siku nyingine, achana na kachumbari.
 
Hizo hizo za Analog mkuu njano, nyeupe etc kama hujajua kucheza nazo zipo za in na out.

Anza kwenye tv ni in ama out? Kwa msaada zaidi weka model ya TV tuangalie arrangement yake, pia angalia tv kwenye box haina Extra Cable? Siku hizi kupunguza utitiri wa ports kunakuwa na Extension imekaa kama waya wa Earphone nimesahau jina lake.

Pia angalia kwenye bar headphone port nayo inaingiza ama inatoa?

Pia angalia bar haina bluetooth? Tv za kisasa zina Bluetooth.
 
Sindikiza ombi lako na kapicha basi tuone 65" inafananaje
 

Model ya Tv ni SMART TV, Samsung QLED 65 Inch. QA65Q60BAKXXA

Inatumia HDMI na Optic Cable. Lakini Speaker za Logitech Hatizumii HDMI wala OPTIC capble. Zina 3 Aux cable Mwishoni na One Port ya Aux Cable. Haina Bluetooth lakini TV ina Option Ya bluetooth

Hii ni Tv kwa Nyuma na Port zake.




Na Hii ni Speaker za Logitech


Hio hapo juu ni Speaker zote 5 za Logitech Take zikiwa Connected kwenye Base.

Hii hapa chini ni Main speaker ya Logitech (Controler)




Hii cord ndio ilipaswa kwenda Kwenye TV na Ku connect


Lakini Hamna Option Ya Kuconnect hizo Cable. Kwenye User Manual wanaonesha kuna Kifaa kinaitwa RCA extractor lakini TV ni Ina HDMI.

Hapo ndio nimekwama.

Msaada
 
Kikawaida mkuu Hdmi ni input tu, ila TV yako ni Exception ina kitu kinaitwa HDMI Earc ambayo ni tech ya kutoa Audio kupitia HDMI. Pia ina Optical hivyo hapo una njia mbili.

-HDMI (2)
-Optical

By Appearence kama sijakosea hio logitech ni speaker ya Computer, hizo waya 3 ukiangalia desktop nyingi zipo kwa Nyuma,

Hivyo hapo mkuu una TV inayotoa digital tu na Speaker zinazopokea Analog tu, adapter itakuhusu ambayo ina convert Digital kwenda analog (DAC) kitu kama hichi
Sema vina bei itabidi uandae 50k kupanda.

Alternative katafute Bluetooth za Aux, za kichina china bei rahisi tu, utumie Bluetooth sema jiandae kundowngrade quality ya sauti za Speaker.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…