Lipa kwa M-Pesa. Anguko/sio anguko la Ajira?

Lipa kwa M-Pesa. Anguko/sio anguko la Ajira?

Tafakari yangu ni juu ya hatua hii ya Vodacom,hasa wananufaika na nini ikiwa mtumiaji wa Huduma ya Lipa kwa Mpesa hakatwi gharama yotote na wakati hivi sasa ukitumia Mpesa kuna makato ambayo mwisho wa siku mawakala wanapata commission na Vodacom wanapata commission,ipo sababu gani kukatisha Ajira za watu hawa wote pasipo kuangalia athari zake
 
Mabadiliko hayana budi kutokea ila kwa maumivu.
Nimekaa na baadhi ya Mawakala wanalalamika juu ya kupoteza wateja wao ambao sasa wanatumia Huduma ya Lipa kwa Mpesa,Mawakala wamejawa hofu juu ya hatma ya Ajira yao na anguko la biashara yao.
 
Tafakari yangu ni juu ya hatua hii ya Vodacom,hasa wananufaika na nini ikiwa mtumiaji wa Huduma ya Lipa kwa Mpesa hakatwi gharama yotote na wakati hivi sasa ukitumia Mpesa kuna makato ambayo mwisho wa siku mawakala wanapata commission na Vodacom wanapata commission,ipo sababu gani kukatisha Ajira za watu hawa wote pasipo kuangalia athari zake
Sidhani kama hilo la kutokukatwa litakuwa la kudumu, ni promotion ya muda. Sasa wasipokata chao watakuwa wananufaikaje?
 
Sidhani kama hilo la kutokukatwa litakuwa la kudumu, ni promotion ya muda. Sasa wasipokata chao watakuwa wananufaikaje?
Ni ipi sababu hasa ya wao( Vodacom) kuanzisha hii Huduma,Je wametafakari kwa kina juu ya upotevu wa Ajira za mawakala wa Mpesa kwa nchi nzima
 
Niwapongeze Vodacom kwa ubunifu. Niliwahama ila nakaribia kurudi maana uhuni wa tigo unaelekea kunishinda. Teknolojia inakua kurahisisha maisha na kupunguza gharama kwa binadamu.

Pamoja na kuwa vijana wamejiajiri kupitia uwakala hawana budi kutafuta ajira au mikakati mbadala kuendana na teknolojia. Huko duniani maroboti yanachukua nafasi za wanadamu viwandani na tayari mataifa yaliyoendelea yanatafakari hatua za kuchukua kuwakinga watu wao na athari za Maendeleo ya teknolojia.
 
Ndugu,huduma ya mawakala itaendelea kuwepo kwani lipa kwa m pesa ni kwa ajili ya kununulia na kulipia huduma tu.Hivyo kwa upande wa kutuma na kupokea pesa huduma hizi zitaendelea kuwepo tu
 
Mimi nafikiri hilo halitawahusu wafanya biashara wa kufanya transactions.....kwasababu wao wana dili na kutoa cash na kuweka pesa....lakini hiyo lipa kwa M-PESA ina husu kufanya manunuzi kwa kutumia M-PESA na wala haizuii wafanyabishara wa kuweka na kutoa pesa maana hiyo lipa kwa M-pesa ili ifanikiwe ni lazima waweke pesa kwa hiyo hakuna biashara inakufa hapo.
 
Ni ipi sababu hasa ya wao( Vodacom) kuanzisha hii Huduma,Je wametafakari kwa kina juu ya upotevu wa Ajira za mawakala wa Mpesa kwa nchi nzima
Kwanza kabisa sioni kama mawaka watapoteza kazi kwani kazi kubwa ya mawakala ni kutoa pesa hapo ndipo wanapotengeneza faida.Hii huduma kwa vodacom itakuwa na faida kwa sababu sasa watakuwa na access ya Pesa za watu na kwa hiyo hii huduma ya Lipa kwa mpesa ni njema na nafikiri ni ya kuigwa na mitandao yote ili tuhakikishe ubebaji wa cash unapungua na hivyo ile 10% serikali ya Sizonje ilikusanya itapungua na hivyo Voda watafurahi.Ova
 
Yajayo yanafurahisha!!!! Upo tayari'??
The future is exciting!!! Are you ready'??
 
Kwanza kabisa sioni kama mawaka watapoteza kazi kwani kazi kubwa ya mawakala ni kutoa pesa hapo ndipo wanapotengeneza faida.Hii huduma kwa vodacom itakuwa na faida kwa sababu sasa watakuwa na access ya Pesa za watu na kwa hiyo hii huduma ya Lipa kwa mpesa ni njema na nafikiri ni ya kuigwa na mitandao yote ili tuhakikishe ubebaji wa cash unapungua na hivyo ile 10% serikali ya Sizonje ilikusanya itapungua na hivyo Voda watafurahi.Ova
Kama utaielewa vizuri hii Huduma,ni kwamba huna haja ya kutoa pesa kwa mawakala badala Yake utakuwa unalipa direct katika duka lolote lile utakalohitaji likuhudumie,mfano nahitaji via mbili katika baa Fulani sitakiwi kwenda kwa wakala kutoa Bali ntalipa kwa Mpesa kwenda direct kwenye namba ya bar husika,Je mawakala watakuwa na kazi gani? Tafakari kwa kina
 
Kama utaielewa vizuri hii Huduma,ni kwamba huna haja ya kutoa pesa kwa mawakala badala Yake utakuwa unalipa direct katika duka lolote lile utakalohitaji likuhudumie,mfano nahitaji via mbili katika baa Fulani sitakiwi kwenda kwa wakala kutoa Bali ntalipa kwa Mpesa kwenda direct kwenye namba ya bar husika,Je mawakala watakuwa na kazi gani? Tafakari kwa kina
Nakuelewa ila nafikiri hii ni teknolojia muhimu wao wawe wanaweka tu pesana kwa wale wachache ambao bado wanatoa wakishindwa wataenda kufanya kazi viwandani
 
Ni ipi sababu hasa ya wao( Vodacom) kuanzisha hii Huduma,Je wametafakari kwa kina juu ya upotevu wa Ajira za mawakala wa Mpesa kwa nchi nzima
Sidhani kaa kutakuwa ma mtikisiko mkubwa sana wa kutisha.

Idara za/ya maji wameanzisha huduma ya kulipia kwa simu, nikajua baada ya muda hawatohitaji tena kaunta, ila hebu nenda ofisi zao uone, miaka zaidi ya miwili au mitatu baadae bado wapo wengi tu wanaendelea kulipia dirishani.
 
Makato lazima yawepo tu siku za mbeleni na hivyo kampuni itazidi kunufaika zaidi
 
Kama utaielewa vizuri hii Huduma,ni kwamba huna haja ya kutoa pesa kwa mawakala badala Yake utakuwa unalipa direct katika duka lolote lile utakalohitaji likuhudumie,mfano nahitaji via mbili katika baa Fulani sitakiwi kwenda kwa wakala kutoa Bali ntalipa kwa Mpesa kwenda direct kwenye namba ya bar husika,Je mawakala watakuwa na kazi gani? Tafakari kwa kina
Huyo mwenye bar atakavyohitaji cash kwaajili ya kununua mahitaji flani je atapata wapi? Jibu rahisi ni lazima aende kwa wakala akatoe, huyo mteja aliekwenda bar na kulipa kwa m pesa salio kapata wapi? Jibu ni kwa wakala.
 
We are moving towards cashless society

Huo ni mwanzo, the time is coming ambako utaishi mwezi mzima na kumaliza mshahara wako wote bila kushika noti
 
Back
Top Bottom