LHRC kimemtaka Mwenyekiti wa ZEC Jecha kujiuzulu wadhifa huo

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
20,819
26,180
Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC kimemtaka mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Jecha Salum Jecha ajiuzulu wadhifa huo kutokana na hatua aliyochukuwa ya kufuta uchaguzi na kutangaza tarehe ya kurudiwa bila kufuata sheria hivyo kumemuondolea sifa ya kusimamia na kuongoza tume hiyo.

Tamko hilo limetolewa jijini Dar es Salaam na kaimu mkurugenzi mtendaji wa LHRC, Bi Imelda Urrio ambapo amesema ukosefu wa taarifa sahihi na rasimi za michakato ya maridhiano toka kufutwa kwa uchaguzi kunaondoa imani ya wananchi juu ya viongozi wao, tume na mchakato mzima wa chaguzi za kidemokrasia Zanzibar.

Wakati huo huo, chama cha kijamii CCK kimemsimamisha kazi na uanachama naibu katibu mkuu wake wa Zanzibar Ali Khatib Ali ambaye pia alikuwa mgombea urais wa Zanzibar kwenye uchaguzi uliotangazwa kufutwa na ZEC Oktoba 2015.

Mwenyekiti wa CCK Costantine Achitanda amesema chama kimefikia maamuzi hayo ili kupisha uchunguzi dhidi yake kufuatia uamuzi wake binafsi wa kutangazia umma kuwa CCK itashiriki uchaguzi wa marudio huko Zanzibar kinyume na taratibu za chama.


Chanzo: EATV

uploadfromtaptalk1454508093655.jpg
 
Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC kimemtaka mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Jecha Salum Jecha ajiuzulu wadhifa huo kutokana na hatua aliyochukuwa ya kufuta uchaguzi na kutangaza tarehe ya kurudiwa bila kufuata sheria hivyo kumemuondolea sifa ya kusimamia na kuongoza tume hiyo.
Tamko hilo limetolewa jijini Dar es Salaam na kaimu mkurugenzi mtendaji wa LHRC Bi Imelda Urrio ambapo amesema ukosefu wa taarifa sahihi na rasimi za michakato ya maridhiano toka kufutwa kwa uchaguzi kunaondoa imani ya wananchi juu ya viongozi wao, tume na mchakato mzima wa chaguzi za kidemokrasia Zanzibar.

Wakati huohuo chama cha kijamii CCK kimemsimamisha kazi na uanachama naibu katibu mkuu wake wa Zanzibar Ali Khatib Ali ambaye pia alikuwa mgombea urais wa Zanzibar kwenye uchaguzi uliotangazwa kufutwa na ZEC Oktoba 2015.

Mwenyekiti wa CCK Costantine Achitanda amesema chama kimefikia maamuzi hayo ili kupisha uchunguzi dhidi yake kufuatia uamuzi wake binafsi wa kutangazia umma kuwa CCK itashiriki uchaguzi wa marudio huko Zanzibar kinyume na taratibu za chama.


Chanzo :EATV

View attachment 321003
Wanamtaka au wanamshauri?
 
Jecha hapaswi kulaumiwa, mwenye kusitahili lawama ni viongozi wa Tanganyika, waliojifunika blanketi la Tanzania tena mchana wa jua kali bila kuona hata joto
 
Ningeona ana akili kama angemtaka yule mkurugenzi wao wa kudumu ajiuzulu kwa kuwa amekaa mda mrefu sana!

Yaani hii ni NGO jipu haswa!
 
Back
Top Bottom