Leo naomba niongee na vijana wote ambao ndio wanaingia au wako kwenye mahusiano

Eddy Love

JF-Expert Member
Jul 25, 2011
13,652
8,539
Kwanza unatakiwa kujua hakuna mapenzi ambayo ni matamu kama mapenzi ambayo yana maendeleo na yenye maisha mazuri. Hata siku mkiwa mko kwenye show zenu huku mna uhakika wa maisha huwaga zile show zinakuwa amazing sana mana zinakuwa hazina stress.

Sasa leo kuna vijana wengi wanakomaa kwenye mahusiano ambayo kwanza hayana furaha japo wanalazimishia furaha. Kwanza kijana unatakiwa kupiga mahesabu kuwa toka umeanza mahusiano na mpenzi wako maisha yanaenda mbele au yanarudi nyuma.

Ukiona maisha yanarudi nyuma basi jinasue kwenye hayo mahusiano. Kwanza siku hizi vijana wanakomaa kuingia kwenye mahusiano na mabinti wadogo na wazuri kwa ajili ya kufurahisha matamanio yao ya sex tu.

Sasa shida ya vibinti hivyo unakuta havijui chochote kuhusu maisha yani hajui kuna kupata au kukosa siku akipiga kizinga huna ananuna. Uko kwenye mahusiano na binti ambaye anajua majina yote ya club mpaka club zingine anaingia bure kwa sababu ashazoeleka wewe bado unakomaa naye.

Tena vijana wengine unakuta anajinyima kabisa yeye anampa mwanamke yani anapigwa kizinga anatoa huku anatukana moyoni eti kinachofanya ajitoe muhanga anaogopa
akimnyima wengine watampa.

Sikia nikuambie kitu, hawa mabinti wa siku hizi ambao hawayajui maisha jinyime weeh siku umeishiwa kabisa usifikiri atabadilika ndio kwanza atakuacha. Sasa wengine unakuta wanakutana na mwanamke ambaye amemzidi umri anampenda lakini anaona noma masela watamcheka.

Acha nikuambie hata mwanaume kuna muda anahitaji kuwa na mwanamke wa kumuongoza ukikuta umepata mwanamke amekuzidi umri ila anayajua maisha usiogope maneno ya watu kuwa naye ukiwa hasa unajua malengo yako na kile ambacho unapata.

Tambua kabisa kuwa na mahusiano na binti ambaye hajawahi kuwaza maisha zaidi ya starehe ni kutengeneza cancer ambayo itakuja kukumaliza mbeleni.

SASA ENDELEA KUJITOA MUHANGA KUVIRIDHISHA HIVYO VIBINTI UNAFIKIRI UKIISHIWA ATAKUONEA HURUMA WAKATI NDIO KWANZA ATAENDA KUCHUKUA KIBABU KAMA BABA YAKO ILI AENDELEE KULA STAREHE.
 
Kwanza unatakiwa kujua hakuna mapenzi
ambayo ni matamu kama mapenzi ambayo yana
maendeleo na yenye maisha mazuri.Hata siku
mkiwa mko kwenye show zenu huku mna uhakika
wa maisha huwaga zile show zinakuwa amazing
sana mana zinakuwa hazina stress.Sasa leo kuna
vijana wengi wanakomaa kwenye mahusiano
ambayo kwanza hayana furaha japo
wanalazimishia furaha.Kwanza kijana unatakiwa
kupiga mahesabu kuwa toka umeanza mahusiano
na mpenzi wako maisha yanaenda mbele au
yanarudi nyuma.Ukiona maisha yanarudi nyuma
basi jinasue kwenye hayo mahusiano.
Kwanza siku hizi vijana wanakomaa kuingia
kwenye mahusiano na mabinti wadogo na wazuri
kwa ajili ya kufurahisha matamanio yao ya sex
tu.Sasa shida ya vibinti hivyo unakuta havijui
chochote kuhusu maisha yani hajui kuna kupata
au kukosa siku akipiga kizinga huna ananuna.Uko
kwenye mahusiano na binti ambaye anajua
majina yote ya club mpaka club zingine anaingia
bure kwa sababu ashazoeleka wewe bado
unakomaa naye.Tena vijana wengine unakuta
anajinyima kabisa yeye anampa mwanamke yani
anapigwa kizinga anatoa huku anatukana moyoni
eti kinachofanya ajitoe muhanga anaogopa
akimnyima wengine watampa.Sikia ni kuambie
kitu hawa mabinti wa siku hizi ambao hawayajui
maisha jinyime weeh siku umeishiwa kabisa
usifikiri atabadilika ndio kwanza atakuacha.
Sasa wengine unakuta wanakutana na
mwanamke ambaye amemzidi umri anampenda
lakini anaona noma masela watamcheka.Acha
nikuambie hata mwanaume kuna muda anahitaji
kuwa na mwanamke wa kumuongoza ukikuta
umepata mwanamke amekuzidi umri ila anayajua
maisha usiogope maneno ya watu kuwa naye
ukiwa hasa unajua malengo yako na kile
ambacho unapata.
Tambua kabisa kuwa na mahusiano na binti
ambaye hajawahi kuwaza maisha zaidi ya
starehe ni kutengeneza cancer ambayo itakuja
kukumaliza mbeleni.
SASA ENDELEA KUJITOA MUHANGA
KUVIRIDHISHA HIVYO VI BINTI UNAFIKIRI
UKIISHIWA ATAKUONEA HURUMA WAKATI NDIO
KWANZA ATAENDA KUCHUKUA KIBABU KAMA
BABA YAKO ILI AENDELEE KULA STAREHE.
Salute kwako mkuuu naona umeshawahi dawati la mbele kabisa..
 
Unatetea mapenzi ya mwanaune kuzidiwa umri na mwanamke!! Hatudanganyiki na mawivu yako acha tutoke na vichenchede vyenye kujua club zote na tujinyime kwani ww inakuuma nn?
 
Kwanza unatakiwa kujua hakuna mapenzi
ambayo ni matamu kama mapenzi ambayo yana
maendeleo na yenye maisha mazuri.Hata siku
mkiwa mko kwenye show zenu huku mna uhakika
wa maisha huwaga zile show zinakuwa amazing
sana mana zinakuwa hazina stress.Sasa leo kuna
vijana wengi wanakomaa kwenye mahusiano
ambayo kwanza hayana furaha japo
wanalazimishia furaha.Kwanza kijana unatakiwa
kupiga mahesabu kuwa toka umeanza mahusiano
na mpenzi wako maisha yanaenda mbele au
yanarudi nyuma.Ukiona maisha yanarudi nyuma
basi jinasue kwenye hayo mahusiano.
Kwanza siku hizi vijana wanakomaa kuingia
kwenye mahusiano na mabinti wadogo na wazuri
kwa ajili ya kufurahisha matamanio yao ya sex
tu.Sasa shida ya vibinti hivyo unakuta havijui
chochote kuhusu maisha yani hajui kuna kupata
au kukosa siku akipiga kizinga huna ananuna.Uko
kwenye mahusiano na binti ambaye anajua
majina yote ya club mpaka club zingine anaingia
bure kwa sababu ashazoeleka wewe bado
unakomaa naye.Tena vijana wengine unakuta
anajinyima kabisa yeye anampa mwanamke yani
anapigwa kizinga anatoa huku anatukana moyoni
eti kinachofanya ajitoe muhanga anaogopa
akimnyima wengine watampa.Sikia ni kuambie
kitu hawa mabinti wa siku hizi ambao hawayajui
maisha jinyime weeh siku umeishiwa kabisa
usifikiri atabadilika ndio kwanza atakuacha.
Sasa wengine unakuta wanakutana na
mwanamke ambaye amemzidi umri anampenda
lakini anaona noma masela watamcheka.Acha
nikuambie hata mwanaume kuna muda anahitaji
kuwa na mwanamke wa kumuongoza ukikuta
umepata mwanamke amekuzidi umri ila anayajua
maisha usiogope maneno ya watu kuwa naye
ukiwa hasa unajua malengo yako na kile
ambacho unapata.
Tambua kabisa kuwa na mahusiano na binti
ambaye hajawahi kuwaza maisha zaidi ya
starehe ni kutengeneza cancer ambayo itakuja
kukumaliza mbeleni.
SASA ENDELEA KUJITOA MUHANGA
KUVIRIDHISHA HIVYO VI BINTI UNAFIKIRI
UKIISHIWA ATAKUONEA HURUMA WAKATI NDIO
KWANZA ATAENDA KUCHUKUA KIBABU KAMA
BABA YAKO ILI AENDELEE KULA STAREHE.
Pesa=Mwanamke. Hapo tuu utauafurahia mapenzi hizo theory nyingine mbwembwe tuu.
 

Similar Discussions

17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom