Lawama za ukosefu wa ajira nchini; Mh Rais mfute kazi Angela Kairuki

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
Mh Rais lawama zote za kukosa ajiri nchini zinazotolewa na wahitimu mbalimbali nchini zinaelekezwa kwako, wananchi bila kujua tatizo linasababishwa na Waziri wa Utumishi, menejimenti ya umma na utawala bora, Mh Rais wananchi wamechoka na hadithi za Waziri Kairuki, Mh Rais wananchi wanakata tamaa sana kusikia matamko yasioisha na yanayojirudiarudia kutoka waziri Kairuki hakuna shaka kwamba ameshindwa kuitendea haki katika ubunifu wa Sera bora za ajira, Ajira mbadala, Mikataba na Mazingira bora ya ajira, udhibiti wa soko la ajira katika sekta binafsi katika kuweka Utanzania kwanza katika sekta ya binafsi Private Sector Employment Control Mechanism maana utakuta wageni Wahindi, Wachina, Waarabu na Wakenya wamejazana katika sekta binfasi nchini, kitu ambacho huwezi kukiona katika nchi hizo tajwa wao wanalinda soko lao la ndani la ajira nchini kwao, sasa ni wakati wa serikali kuweka mkazo ajira iwe kwa watanzania kwanza,Aidha, uthibiti wa utoaji vibali vya ajira kunakofanywa na Wizara hiyo nyeti sana katika
kukuza uchumi kupitia watumishi wa umma ndio tatizo kuu kama sio janga kuu la wazawa, watumishi wa umma na wahitimu wote wanailaumu Serikali kwa kukosa ajira kuliko vipindi vyote vilivyopita, hiyo yote inaletwa na Wizara hiyo mama sana na uti wa mgongo kwa utumishi na utawala bora nchini kwa kukosa ubunifu ili kuboresha mahusiano bora
 
Mi nijuavyo serikali yote kwa ujumla hawana njia(policy) yoyote ambayo wanayoijua wao kuweza kutengeneza ajira za kibinafsi na serikali na sijui kwa nini, ndio maana baadhi ya mawaziri wanatoa majibu mepesi ya kuwaambia vijana wajiajiri Fursa zipo nyingi kana kwamba swala la ajira nchini halihusiani na serikali kabisa, kwa hiyo huyo mama utamlaumu bure tu, vijaana waache tena kuweka matumaini kwenye hii serikali kuhusu swala la ajira wajitahidi tu kutafuta shughuli ya kufanya.
 
Back
Top Bottom