Lahaja za kiswahili zipo kama 15-20 na zote ni sahihi ( kuanzia kibarawa -somalia mapaka kikomoro)
Lahaja ilofanywa kuwa rasmi ni kiunguja mjini na ndio hii tunayosomeshwa na inayotumika kwenye vyombo vya habari......
Sifikirii kama ni sahihi kusema lahaja nyengine sio sahihi.........
kila mahali kuna lahaja yake na watu wake wanaiona sahihi...ukienda kenya watakuambia lahaja ya kimvita ilistahili zaidi kusanifishwa kuliko lahaja ya kiunguja.