Kwenda kutambulisha mchumba nyumbani.

Kwenda kutambulisha mchumba nyumbani.

NDESSA

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2013
Posts
1,946
Reaction score
1,800
Wakuu naomba kujua kutoka kwa wenye uzoefu kwamba Mwanaume/Mvulana anapoenda na mchumba wake wa kike kumtambulisha kwao hasa mikoa ya mbali je wakifika kwao na mwanaume wakati wa kulala huyo mvulana hulala na msichana wake au vyumba tofauti?
 
We tuliza tu kipago, watakapokuonyesha ulale ndipo utalala. Kila familia ina ustaarabu wake kulingana na mazingira na utashi.
 
Nasubiri majibu maana kuna binti nnampango wa kwenda nae home, ila sehemu ya kufikia ndio shida.
 
analala tofauti na wewe. Inategemea na dini na mila na desturi. Lakini kuna familia hasa za pwani pwani umeshaoa huyo hakuna shida mnapewa chumba. But hii ni kuonyesha heshima kwa wazazi kwani huku town huwa ikoje si mpo beneti. Tabia zako nzuri au mbovu zinaonekana hapo. Inakuwaga siku 1 tu unafika jioni analala kesho safari ukikaa naye sana mashangazi wakija utasikia mara hajui kuosha vyombo, mara hajui kupika, mara anakiburi nk.
 
Ndesa umeuliza swali la muhimu sana,mm mwenyewe nilikuwa njiapanda kwa hili!
 
Nilipompelekea home, nilihakikisha anapata sehemu ya kulala tofauti na nyumbani (tuli-organize na ndugu yake mmoja anaekaa huo mkoa), home alikuja akala lunch and stayed for only 2 hrs then kumrudisha alikofikia. Akikaa tu home muda mrefu issue huwa zinaanza kuibuka achilia mbali kulala. btw kila jamii na tamaduni zake ila KULALA NAE CHUMBA KIMOJA MWIKO
 
Kila mtu na chumba chake, au atalala na wifi zake watarajiwa.

Kama ana ndugu maeneo ya jirani atalala kwa ndugu zake na nyumbani kwenu atakuja kutembea tu.
 
Back
Top Bottom