Kwanini waziri mkuu asijiuzulu ??

Kwanini waziri mkuu asijiuzulu ??

nhassall

Senior Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
195
Reaction score
41
Ninashangaa sana tangu niliposoma GAZETI LA KULIKONI la tarehe 20/06/2014 la siku ya Ijumaa lililosema kuhusu majibu aliyojibu aliyekuwa WAZIRI WA FEDHA Hon Mustafa huku akiungwa mkono na SPIKA WA BUNGE Hon Anne Makinda kwamba ametumia busara na uvumilivu kwa miaka miwili na kuamua kujibu kwa kusema ukweli kuhusu uuzwaji wa kiwanja kwenye kitalu namba 10 Nyerere Road.
Spika alisema wazi, cha ajabu tarehe 01/07/2014 WAZIRI WA FEDHA wa hivi sasa Hon Saada Mkuya ametangaza kulifuta rasmi shirika la CHC na mali zote zinahamishiwa kwa msajili wa Hazina na baadhi ya wafanyakazi kutupiwa virago.
Nakala ya barua ya Waziri imeandikwa na kupelekwa CHC.

MASWALI.
1. Kwanini suala hili lije na kuamuliwa kufutwa rasmi kwa CHC baada ya Spika kuhoji na kuiambia serikali na wabunge kuacha tabia ya kukomoana maana Waziri Mkulo hakutajwa kuhusika katika ripoti ya CAG ?

2. Kwanini Waziri Mkuu akiwa ni mshauri wa Raisi aliomba Waziri Mkulo aondolewe akijua fika alikuwa nje ya nchi kuitafutia nchi pesa ?

3. JE WAZIRI MKUU PINDA AMEWEZA KUVAA VIATU VYA EDWARD LOWASSA ?
 
Zitto alimkomalia sana Mkulo na hoja yake ilikuwa hii,amuombe radhi ....
 
Zitto siyo aliyemuwajibisha , kumbuka WAZIRI MKUU alipaswa kutoa ufafanuzi ndani ya BUNGE kwamba mhusika yuko safari na siyo vizuri kumjadili. PIA kwanini sasa CHC ifutwe kuna agenda gani ya siri ?
 
JK alibugi big time kwa kuchelea kumuondoa PINDA eti kwa kuwa ni muumini mzuri wa kanisa! kama ilikuwa lazima wapate wa kutoka kanisani si wangemtafuta mwingine mchapakazi badala ya huyu anaeshindwa hata kumkemea Lukuvi? Fitna zote za kumchafua Mkulo leo hii iko wapi zaidi ya aibu tele? Fitna zote za kumchafua Lowassa wakati ukweli unajulikana waliopiga deal la Richmond na sasa Symbion Wanajisikiaje? Hizi double standard approach za CCM zitaendelea kuigharimu nchi yetu mpaka lini? Kuvunja CHC kunatosha bila ya kuwaadabisha wahusika?...
Ninashangaa sana tangu niliposoma GAZETI LA KULIKONI la tarehe 20/06/2014 la siku ya Ijumaa lililosema kuhusu majibu aliyojibu aliyekuwa WAZIRI WA FEDHA Hon Mustafa huku akiungwa mkono na SPIKA WA BUNGE Hon Anne Makinda kwamba ametumia busara na uvumilivu kwa miaka miwili na kuamua kujibu kwa kusema ukweli kuhusu uuzwaji wa kiwanja kwenye kitalu namba 10 Nyerere Road.
Spika alisema wazi, cha ajabu tarehe 01/07/2014 WAZIRI WA FEDHA wa hivi sasa Hon Saada Mkuya ametangaza kulifuta rasmi shirika la CHC na mali zote zinahamishiwa kwa msajili wa Hazina na baadhi ya wafanyakazi kutupiwa virago.
Nakala ya barua ya Waziri imeandikwa na kupelekwa CHC.

MASWALI.
1. Kwanini suala hili lije na kuamuliwa kufutwa rasmi kwa CHC baada ya Spika kuhoji na kuiambia serikali na wabunge kuacha tabia ya kukomoana maana Waziri Mkulo hakutajwa kuhusika katika ripoti ya CAG ?

2. Kwanini Waziri Mkuu akiwa ni mshauri wa Raisi aliomba Waziri Mkulo aondolewe akijua fika alikuwa nje ya nchi kuitafutia nchi pesa ?

3. JE WAZIRI MKUU PINDA AMEWEZA KUVAA VIATU VYA EDWARD LOWASSA ?
 
Back
Top Bottom