Kwanini wananchi wanasema tozo ni wizi?

Kwanini wananchi wanasema tozo ni wizi?

Fernando Wolle

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2022
Posts
387
Reaction score
775
Kwanza naamini hakuna Mtanzania ambaye hajui umuhimu wa kulipa kodi, kila mwananchi anatambua umuhimu wa kodi. Na hakuna serikali duniani inayoweza kuendeshwa pasipo kukusanya kodi.

๐˜’๐˜ธ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ช๐˜ฏ๐˜ช ๐˜ธ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ค๐˜ฉ๐˜ช ๐˜ธ๐˜ฆ๐˜ฏ๐˜จ๐˜ช ๐˜ธ๐˜ข๐˜ฏ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข๐˜ฎ๐˜ช๐˜ฌ๐˜ข ๐˜ฌ๐˜ถ๐˜ฉ๐˜ถ๐˜ด๐˜ถ ๐˜ต๐˜ฐ๐˜ป๐˜ฐ?
Licha ya tozo hizi zinazolalamikiwa hapa kutokuwa na ufafanuzi wa kutosha wala kutolewa Elimu ya kutosha kutoka kwa wanaotoza kwenda kwa wanaotozwa, bado zinaonekana zina mapungufu na kuna maswali mengi kuliko majibu.

๐˜›๐˜ฐ๐˜ป๐˜ฐ ๐˜ป๐˜ช๐˜ฏ๐˜ข๐˜ป๐˜ฐ๐˜ญ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข๐˜ฎ๐˜ช๐˜ฌ๐˜ช๐˜ธ๐˜ข ๐˜ฉ๐˜ข๐˜ฑ๐˜ข ๐˜ฏ๐˜ช
1. ๐˜›๐˜ฐ๐˜ป๐˜ฐ ๐˜ป๐˜ข ๐˜ฎ๐˜ช๐˜ข๐˜ฎ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข ๐˜บ๐˜ข ๐˜ด๐˜ช๐˜ฎ๐˜ถ
2. ๐˜›๐˜ฐ๐˜ป๐˜ฐ ๐˜ป๐˜ข ๐˜ฎ๐˜ช๐˜ข๐˜ฎ๐˜ข๐˜ญ๐˜ข ๐˜บ๐˜ข ๐˜ฃ๐˜ฆ๐˜ฏ๐˜ฌ๐˜ช
3. ๐˜›๐˜ฐ๐˜ป๐˜ฐ ๐˜ป๐˜ข ๐˜ท๐˜ช๐˜ฏ๐˜จ'๐˜ข๐˜ฎ๐˜ถ๐˜ป๐˜ช
Kwa ujumla ni tozo zote za Kielekroniki.

Katika hali ya kawaida ni kwamba tozo hizi zinaonekana kukatwa mara mbilimbili pasina kuwa na sababu maalum.

Mathalani, mfanyakazi/Mtumishi anayelipwa mshahara hukatwa Kodi na Serikali kwenye PAYE, pia kuna Makato mengine kama ya NSSF/PSSSF, Bima na mengine yanayofanana na hayo. Makato haya hufanyika kisha mshahara wa mfanyakazi (take home) huingizwa kwenye akaunti yake ya benki husika.

๐‘ด๐’Œ๐’‚๐’๐’ˆ๐’‚๐’๐’š๐’Š๐’Œ๐’ ๐’‰๐’–๐’– ๐’‰๐’‚๐’‘๐’‚! Mshahara huohuo ambao umeshakatwakatwa, mfanyakazi anapokwenda kuchukua haki yake anakutana na Serikali iko pale inasubiri tena kwa mara ya pili kitu kinaitwa tozo, Sasa hapa serikali inakuwa imewekeza nini? Kwasababu kwa mara hii Makato yalipaswa kuwa ya benki Pekee (๐˜ด๐˜ฆ๐˜ณ๐˜ท๐˜ช๐˜ค๐˜ฆ ๐˜ฑ๐˜ณ๐˜ฐ๐˜ท๐˜ช๐˜ฅ๐˜ฆ๐˜ณ) ambapo mteja hukatwa kulipia gharama za huduma ila hapa tuulize kiungwana kabisa Serikali yenyewe inakuwa imefanya nini mpaka kukata mara ya pili?

Mfano mwingine, mfanyabiashara analipa Kodi ya serikali moja kwa moja kwa TRA, anapambana kupata faida kidogo anaweka benki, akihitaji kuchukua pesa yake benki anaikuta Serikali tena kwa mara ya pili inasubiri tozo. Huku ni kulipishwa Kodi mara mbilimbili isipokuwa Majina ya Kodi ndio yanatofautiana. Sasa huu utitiri wa tozo una tofauti gani na Kodi za kipindi cha ukoloni? Mfano poll tax, hut tax, matiti tax, n.k.

Tukienda kwenye tozo za miamala ya simu ni kitu kilekile na tukirudi kwenye tozo za king'amuzi mambo ni yale yale ya serikali kuvuna mahali ambapo haijapanda, ili serikali isilaumiwe iende na kanuni ya kuwekeza na kuvuna na sio kuvuna bila kuwekeza tofauti na hapo ni kuua uchumi wa watu na ๐˜ง๐˜ช๐˜ฏ๐˜ข๐˜ญ๐˜ญ๐˜บ taifa litayumba kiuchumi.

๐šƒ๐šž๐š”๐šž๐š–๐š‹๐šž๐š”๐šŽ: Miaka mitano iliyopita serikali ilibuni vitambulisho vya Wamachinga japo kuna watu walipinga lakini ule angalau ulikuwa ni ubunifu wa kukusanya mapato ya serikali ambao tunaweza kusema ulikuwa ni '๐˜”๐˜ถ๐˜ต๐˜ถ๐˜ข๐˜ญ ๐˜ฃ๐˜ฆ๐˜ฏ๐˜ฆ๐˜ง๐˜ช๐˜ค๐˜ช๐˜ข๐˜ญ' . Ilikuwa Machinga akilipia elfu ishirini anaona kuna sababu kwanini amelipia. Anaruhusiwa kufanya biashara kwenye miundombinu ya serikali, hiyo ni sababu tosha kabisa kwamba serikali inakuwa imefanya kitu kwa huyu mtu anayetozwa hiyo kodi.

Uwekaji wa tozo hizi za sasa unaashiria ubunifu hafifu wa ukusanyaji mapato. Tanzania kama nchi tumebahatika sana kuwa na rasilimali nyingi zinazoweza kuingiza mapato makubwa kama kutakuwa na usimamizi madhubuti.

Rai ni kwamba viongozi wanaohusika na mikakati ya ukusanyaji mapato, wapende kuumiza vichwa kupata njia bora ya kukusanya mapato na sio kutumia njia rahisi namna hii.
WhatsApp Image 2022-08-12 at 3.33.40 PM.jpeg
 
Lipa kodi acha ulalamishi. Ulalamishi ni aina ya ukichaa. Lipa bila nongwa. CCM oyeeeee!
 
Lipa kodi acha ulalamishi. Ulalamishi ni aina ya ukichaa. Lipa bila nongwa. CCM oyeeeee!
Kuwa ccm sio kushangilia kila kitu bila kufanya reasoning. Mwalimu Nyerere ambaye ndio muasisi wa ccm na aliijua ccm kuliko wewe alisema tunahitaji vijana wadadisi, vijana wanaoweza kuipa changamoto serikali na chama, vijana jeuri. Sio vijana wa kusema ndioooo kwa kila kitu.
 
Tozo zenyewe zimekaa kiwizi wizi! Wakataji wa hizo tozo wenyewe nao wamekaa kiwizi wizi! Kwa hali hii wananchi nao lazima waingiwe na hofu.
 
Kwanza naamini hakuna Mtanzania ambaye hajui umuhimu wa kulipa kodi, kila mwananchi anatambua umuhimu wa kodi.

Licha ya kwamba Tozo zinazolalamikiwa hapa hazina ufafanuzi wa kutosha wala hazijatolewa Elimu ya kutosha kutoka kwa wanaotoza kwenda kwa wanaotozwa bado kuna mapungufu na kuna maswali mengi kuliko majibu.

Tozo zinazolalamikiwa hapa ni
1. Tozo za miamala ya simu
2. Tozo za miamala ya benki
3. Tozo za ving'amuzi

Katika hali ya kawaida ni kwamba tozo hizi zinaonekana kukatwa mara mbilimbili pasina kuwa na sababu maalum.

Mathalani, mfanyakazi/Mtumishi anayelipwa mshahara hukatwa Kodi na Serikali kwenye PAYE, pia kuna Makato mengine kama ya NSSF/PSSSF, Bima na mengine yanayofanana na hayo. Makato haya hufanyika ndipo mshahara wa mfanyakazi huingizwa kwenye akaunti yake kwenye benki husika.

Ajabu ni hii hapa, mshahara huohuo ambao umeshakatwakatwa, mfanyakazi anakwenda kuchukua haki yake anakutana na Serikali iko pale inasubiri tena kwa mara ya pili kitu kinaitwa tozo, Sasa hapa serikali inakuwa imewekeza nini? Kwasababu hapa Makato yalipaswa kuwa ya benki Pekee ambapo unakatwa kwasababu ya gharama za huduma ila Serikali yenyewe imefanya nini mpaka kukata mara ya pili?

Mfano mwingine, mfanyabiashara analipa Kodi ya serikali kwa TRA, anapambana kupata faida kidogo anaweka benki, akihitaji pesa yake anaikuta Serikali tena inasubiri tozo ambayo kimsingi ni kwa mara ya Pili. Huku ni kulipishwa Kodi mara mbilimbili isipokuwa Majina ya Kodi ndio yanatofautiana.

Tukienda kwenye tozo za miamala ya simu ni kitu kilekile na tukirudi tozo za kwenye king'amuzi mambo ni yale yale ya serikali kuvuna mahali ambapo haijapanda. Awamu ya Tano kuhusu vitambulisho vya Wamachinga japo kuna watu walipinga lakini ilikuwa ukilipia elfu ishirini unaona kuna sababu kwanini umelipia.

Sasa huu utitiri wa tozo una tofauti gani na Kodi kipindi cha ukoloni? Mfano head tax, matiti tax, n.k.

Uwekaji wa tozo hizi unaashiria ubunifu hafifu wa ukusanyaji mapato kwa kusimamia vizuri rasilimali tulizonazo. Viongozi hawataki kuumiza vichwa kupata njia bora ya kukusanya mapato.
Mama kawekwa kama tv remote wameshika wengine ko maamuzi yanayowagusa washika remote hamtayaskia kamwe.
 
Back
Top Bottom