N'yadikwa
JF-Expert Member
- Aug 10, 2014
- 6,826
- 9,533
Kwani ni kitu gani kimewasibu TBC1 mshindwe kurusha HD kwenye chaneli zenu za TBC1 na Safari Chaneli?. Ubora wa picha ni duni sana. Hii ni chaneli ya Taifa, kutuonyesha ‘ungaunga’ kwa picha ambazo unaona kabisa zilipigwa kwa HD hamtutendei haki. Vipindi vya chaneli nyingine kama ZBC, Channel 10, UTV nk viko HD ya nguvu unapata na raha ya kutazama. Kwani nyie wenzetu mmekumbwa na nini?!!. Sitaki kuamini kwamba ni suala la Bajeti.
Kwamba Channel 10 aweze kurusha HD halafu nyie TV ya Taifa mshindwe?!, How Possible. Mbona ni kama Channel hizi hazina uongozi.
Wizara wasaidieni TBC1 waonyeshe picha zenye ubora hii ni kero kubwa. Kuna watu tunapenda kutazama Educational Programmes ambazo zinapatikana TBC ila kwa ubora huo tunaamua kuachana nayo. Badilikeni bana mnaudhi. Mheshimiwa Rais kama TBC wameshindwa tunaomba uwasaidie kubadilika. Pia, Bodi ya TBC mlioingia hivi karibuni timizeni wajibu wenu ipasavyo kuwapa wananchi matangazo ya TV yenye ubora.
Kwamba Channel 10 aweze kurusha HD halafu nyie TV ya Taifa mshindwe?!, How Possible. Mbona ni kama Channel hizi hazina uongozi.
Wizara wasaidieni TBC1 waonyeshe picha zenye ubora hii ni kero kubwa. Kuna watu tunapenda kutazama Educational Programmes ambazo zinapatikana TBC ila kwa ubora huo tunaamua kuachana nayo. Badilikeni bana mnaudhi. Mheshimiwa Rais kama TBC wameshindwa tunaomba uwasaidie kubadilika. Pia, Bodi ya TBC mlioingia hivi karibuni timizeni wajibu wenu ipasavyo kuwapa wananchi matangazo ya TV yenye ubora.