Kwanini maskini siku zote haeshimiwi

Unataka aheshimiwe kwa huo umasikini wake?
Ndio Kiongozi.

Kama ni kweli tunaamini Binaadam wote ni sawa, basi hata na sisi wenye Hali za chini inabidi tuheshimiwe
 
Umasikini unahusishwa na ujinga
Kwahiyo unataka kusema sisi ni wajinga?

Si mnaona wenyewe tunavyozidi kuvunjiwa Heshima na kudharaulika.

Haina maana sisi hatuna Akili ya kutafuta, haina maana sisi ni Wavivu, haina maana sisi hatuna mipangilio.

Ni mishale tu inakataa.

Mbona sie wapiganaji sana.

Jamani msitudharau
 
Point well taken
 
Ndio Kiongozi.

Kama ni kweli tunaamini Binaadam wote ni sawa, basi hata na sisi wenye Hali za chini inabidi tuheshimiwe
Dharau kwa masikini inaanzia kwenye ngazi za familia, nyumbani kaka akiwa masikini halafu mdogo wake yupo vyema basi heshima na nidhamu kubwa atapokea dogo. Matatizo mengi ya kifamilia atayapokea yeye mwenye nazo na solution atatoa yeye, wewe kaka usie na kitu utakuwa unasikia sikia tu
 
Lakini hata ukiongelea ngazi ya familia jiangalie ngazi ya taifa Tanzania mnachukuliwaje na mataifa mengine????
 
Lakini hata ukiongelea ngazi ya familia jiangalie ngazi ya taifa Tanzania mnachukuliwaje na mataifa mengine????
Masikini hana thamani popote pale iwe kitaifa au kifamilia, njia pekee ya kujiletea heshima ni kupambana kuuondoa umasikini, wenyewe wanasema umasikini au utajiri ni man made situation hivyo ni juhudi zako tu. Bill Gates pia aliwahi kusema kuzaliwa masikini sio kosa lakini kufa masikini ni kosa
 
Hapo hujaelewa mada hatujaongelea kosa la kuwa masikini umenielewa?/?


Ngoja nikuulize TZ inapochukuliwa kama nchi maskini ina maana hkuna matajiri Tz????


Pia kama kama unasema kupambana kuondoa umaskini kutokana na mada kwa nini maskini akifanya kitu cha kipesa anaonekana hakimfai???

Kwani maskini akinunua kuku si kapambana kama alkuwa anakula dagaa kapambana mpaka kapata hela ya kununua kuku.

Na unavoongelea hvyo unadhani Tanzania haina uwezo wa kujenga viwanda lakini kwa kuwa ikiweka wazo mezani linadondoshwa kutokana na kuwa inajulkana ni nchi maskini!

NB:Through heshima and support kwa maskini na yeye anaweza kupata courage ya ku struggle kutoka kwenye umaskini!
 
Swali lako ni "kwanini masikini hathaminiwi", hiyo kitaifa na kifamilia imekuja tu wakati wa kushea mawazo na hata nilipozungumzia mtazamo wa bill gates juu ya umasikini ni katika kujibu kwanini masikini hathaminiwi. Mtazamo wa wengi ni kuwa masikini ni mkosaji au failure, matajiri wengi wanaamini utajiri wao umetokana na juhudi zao hivyo ukiwa masikini ni uzembe wako tu na hapo ndipo heshima ya masikini inaposhuka, duniani heshima ni kwa winner tu hao failure hawana thamani hiyo ipo hivyo tangu enzi na enzi.
 
Sasa me ndo nataka nijue kwanini inamaana hela ina thamai kuzidi ubinadamu???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…