nyumba kubwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 10,309
- 8,369
kwa sababu ujana ni maji ya moto
Habarini wana MMU
nimefanya analysis nimegundua vijana wa zama hizi ndoa zao ni nguvu ya soda wanaachana fasta kwanin?
Mfano. Bro wangu mmoja ni tutorial assistant pale SUA alimuoa class mate wake bonge la harusi kule kwetu mwanza waliachana baada ya miezi miwili kwa Ugomvi mkubwa sana na bro mwingine alioa mwaka jana mwezi wa 7 binti mmoja wa kidigo yani by december ndoa ikavunjika kbsaaa
sasa wenzetu mliodumu ndoani what are the mistakes tunazokosea jamani???
Tujulisheni tujifunze maana haileti picha nzuri kabisa.
Ndoa ni kwa ajili ya wanaume na wanawake na siyo kwa wavulana na wasichana. Kama hujaelewa wewe bado ni mvulana.
Soap Operas zinawadanganya sana vijana.
Ukisasa ndio unawapoteza maana wameyapokea tofauti sana.
Eti unakuta Dada Anamwambia mchumba/mumewe kuwa hawezi kuachana na facebook ila yuko tayari waachane.
Na wengine hukimbilia kuolewa ili wasiwachwe nyuma na wenzao, na sio sababu wana mapenzi ya kweli.
USHAURI.
Ukimaliza shule/chuo au ukianza kujitegemea usikimbilie ndoa au kuishi na mpenzi. Kama binadam unahitaji uhuru, tumia muda kidogo kufurahia maisha ukiridhika na kuona sasa ni kweli unahitaji mwenza fanya hivyo na hautopata shida.
Mtu katoka chini ya sheria na ulinzi wa wazazi anakimbilia ulinzi mwingine wa mke/mume. Lazima mchokane mapema muachane
....Tatizo siku hizi kila mmoja anajifanya yeye mjanja, hakuna anayejishusha. Vile vile wanawake wengi siku hizi hawataki kupelekeshwa kama wamama waliolewa zamani.....na wanaume wengi wa siku hizi maneno mengi mdomoni, nakupenda nyingi, vitendo hakuna.
Kwa hiyo ww
Uvumilivu kwenye ndoa za sasa ni zero, wanasema maisha mafupi na raha jipe mwenyeweeee!! Hivyo watu wanataka mteremko tu kwenye ndoa , wamesahau kama kuna milima na mabonde.
1. kuwa "tutorial assistant SUA "hakuvunji ndoa wala kuongeza kudumu kwa ndoa
2. ukioa "mdigo "siyo ndo ndoa yako itadumu, aidha siyo kweli kuwa ndoa yako haitadumu
3.si kweli ukiwa "tutorial assistant SUA" au ukioa msichana "mdigo" ndiyo wewe ni "kijana wa zama hizi"
aidha kutokana na ukweli kuwa hawa wote uliowataja kuwa ndoa zao hazijadumu ni "Bro" zako. inaweza ikawa ina nguvu ya kiuchunguzi ikiwa utahusisha kuvunjika kwa hizo ndoa na familia, au ukoo wenu. kuhusisha na vijana wa zama hizi haitoshi kwani hilo eneo ulilochukua sampuli zako ni jembamba mno kuwakilisha jamii ya vijana wa zama hizi
Tata amemaliza kila kitu hapo juu!
Habarini wana MMU
nimefanya analysis nimegundua vijana wa zama hizi ndoa zao ni nguvu ya soda wanaachana fasta kwanin?
Mfano. Bro wangu mmoja ni tutorial assistant pale SUA alimuoa class mate wake bonge la harusi kule kwetu mwanza waliachana baada ya miezi miwili kwa Ugomvi mkubwa sana na bro mwingine alioa mwaka jana mwezi wa 7 binti mmoja wa kidigo yani by december ndoa ikavunjika kbsaaa
sasa wenzetu mliodumu ndoani what are the mistakes tunazokosea jamani???
Tujulisheni tujifunze maana haileti picha nzuri kabisa.
uanaume unaanzia miaka mingap?
Kashengo
Ndoa za sasa hazidumu like before because people (and by that I mean women) now days have choices! Fortunately tumefunguka macho and we are no longer afraid to put ourselves and our hapiness first. Sio kama zamani mtu unakuta anavumilia crap after crap iili asiachik na kuishia kuaibika na kutokuitwa someone's missus !
Bwana mdogo karudi darasani ujifunze upya ku present point zako. halafu Huku kujidai kujua kila kitu na kubisha bisha ndiko kunakowaponza vijana kama wewe. Unataka afanye utafiti gani zaidi ya huo .Ebu acha kuleta theories za darasani ambazo humu haziwezi kamwe kufanya kazi hapa tunaongea kwa uzoefu.