scramble
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 1,593
- 257
Wengi tulikua tunahisi kuwa hatua itakayofuata ni kila nchi kumrudisha balozi wake nyumbani. Wiki iliyopita kuna habari ilizagaa kuwa Rwanda na Uganda hazitotumia tena Bandari ya Dar kuanzia Sept. 1. Habari hii ina ukweli japo Rwanda na Uganda hazikutoa tamko la mwisho la kukotumia bandari yetu. Ilikua ni tahadhari ya awali.
Mwishoni mwa wiki, Naibu Waziri wa Uchukuzi Muh. Charles Tizeba alitumwa na Serikali kwenda Rwanda kukutana na Waziri mwenzake pamoja na wafanyabiashara wanaotumia bandari ya Dar. Lengo la ziara lilikua kuweka mambo sawa ili bandari yetu iendelee kutumiwa na Rwanda.
Muh. Tizeba aliwaambia wafanyabiashara na waziri wa uchukuzi wa Rwanda kuwa alimtuma mtu kutoka wizarani ili akasafiri kwenye lori kwa lengo la kushuhudia kero za barabarani. "Yule niliemtuma alisema kuwa walisimamishwa njiani mara 107. Ni kwenye mizani na check points za polisi na TRA. Kuanzia leo tumepunguza idadi ya mizani kwa malori ya Rwanda. Lori zitapimwa Vigwaza, Singida na mpakani. Vituo vitatu tu. Watu wa TRA na POlisi nao watacheki malori kwenye hizo mizani." Jambo hili liliwafurahisha wafanyabiashara ukizingatia kuwa bandari ya dar ipo karibu na Rwanda kuliko ile ya Mombasa. Wameahidi kutumia bandari ya Dar.
Naipongeza serikali kwa kwenda Rwanda haraka iwezikanavyo. Waziri aende Uganda kwa lengo hilohilo! Kama mawaziri wote wangekua wana react immediately, tungekua mbali kimaendeleo. Hongera Mwakyembe na Tizeba!
WanaJF, hivi ni lazima vituo viwe vingi kiasi hiki!? Hamdhani kuwa suala la utitiri wa mizani na check points linahitaji mjadala wa kitaifa? Basi la kwenda Tanga kutoka Dar linapimwa Kibaha, Msata na Tanga kabla ya kuingia Stendi. Hivi pana haja ya kupima basi mara tatu au zaidi? Nawasilisha!