Kwa hili la Simba na Yanga inatosha sasa

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
Nimechoka kila mtu ili aonekane anajua mpira anaona kuiponda simba na yanga ndo kigezo kikubwa. Huu ni ukondefu wa fikra. Huwezi ukawa na akili zenye afya ukadhani soka la tanzania litakua kwa kuiponda simba na yanga au kupendekeza kuwa timu hizi zifutwe. Wewe una fikiri sawa sawa kweli?
Imekuwa ni tabia inayojijenga kwa sasa kila mtu anapokuwa amefadhaishwa na matokeo ya mpira wa simba au yanga anakuja na suluhisho la kuwa hizi timu zifutwe. Huu ni uwezo wa chini sana wa kufikiri.

Hizi timu ni historia katika nchi yetu kwa mwenye uelewa mzuri hawezi kamwe waza jambo kama hilo. Tunafaham asilimia kubwa ya wapenzi wa mpira ni wa simba na yanga theni zinakuja za mikoani ambako mtu anatokea ambako pia huko kuna kuwa kama ilivyo first language na second language. timu mama bado ni simba na yanga. Then mtu ataipenda Mbeya city, majimaji au reli ya Morogoro. Huo ni ukweli kwa kiasi kikubwa kwa wale wenye umri mkubwa kwenye michezo ukiacha watoto wa miaka hii ya 90 na 2000s.

Na kiukweli si kuwa ili uweze onesha una uwezo wa kuchambua michezo basi ni vyema ukatumia mawe timu hizi, tunajua kuna wanaolipwa kwa kuzitupia mawe timu hizi na kuzisifia timu zile au pengine za nje. Lakini kuna wengine ni kwa ulevi na ukosefu wa vitamins katika fikra wanadhani miti ya kutupia mawe ni simba na yanga tu ili waonekane nao wanaweza kurusha mawe.

Azam imekuwa kwenye soka kwa miaka kadhaa sasa. Naipongeza ina mtaji mkubwa kutokana na kumilikiwa na mtu tajiri. Lakini kimataifa tujiulize imeshiriki mara ngapi na imefanya nini ambacho simba na yanga hawajahi? mtasema uwanja. Ni kweli. Hili ni jambo zuri sana na la kupongeza lakini muelewe azam haindeshwi na wanachama. Azam kuna watu wapo kule kimaslah tu illa mioyoni mwao ni wapenzi wa simba na yanga.

Na wengine kwa sababu ya chuki na hasira ndo wanasema wao ni azam lakini kiuhalisia washabiki hasa wenye uchungu na azam hawafiki hata 1000. Huwezi ilinganisha na simba na yanga katika hili. Bado hizi zitabaki kuwa ni timu kongwe na zenye ushawishi mkubwa katika soka la Tanzania na Afrika kwa ujumla. hamjajifunza? Angalieni zanzibar baada ya kutetereka kwa small simba na jamhuri na ile nyingine nimeisahau. Ligi ya Zanzibar imekuaje? Ukiweka sababu nyingine pia ni kukosa msisimko. na ndo maana ni ngumu pia kuzifanya simba na yanga zishuke daraja.

Huo mwaka TFF wata experience mapato kidogo kuliko inavyodhaniwa. Usilinganishe ligi ya uingereza na ya Tanzania au Hispania na Tanzania. Angalia ni timu gani zinajaza uwanja wa Taifa. Hata azam ikicheza na timu nyingine ule uwanja haujai.

Tuache kuwaza fyongo kuwa simba na yanga ndo zinaua mpira wa tanzania..tujiulize lini ulikuwa hai na sasa umekufa. Tukubaliane kuna mapungufu lakini solution si kuziua/kuzivunja au kuzishusha daraja. Tuwaze kwa unene kidogo, mtu akipata jeraha kwenye kidole haimaanishi mkono wote ukatwe ....ni dakatar mvivu na mzembe anayeweza kufikiri hivyo.

NIMESEMA SASA KAMA UTAKASIRIKA KASIRIKA TU, SIWEZI UNAFIKI NA MOYO WANGU UMETULIA.
 
Dawa ni kuzivunja tu...sababu zinawafanya watanzania kama wewe upeo wako wa kufikiri uishie msimbazi na jangwani na wachezaji nao kitu cha maana sana kwao ni kuifunga simba au yanga..wala hawafikirii siku moja wawe mabingwa wa afrika...tumeona mazembe wakifika fainali hizo mara tano sasa...halafu ww unatetea timu mf simba hata uwanja wa mazoezi hawana tangu 1934
 
Simba hao ambao unawaona mafala ndio waliotengeneza njia kwa mtanzania wakwanza kutwaa tuzo ya CAF.sema tatizo ninaloona hapa ni rushwa iliyotamalaki kwa marefa.Ili simba ionekane haifai.
 
Ukiniambia Yanga inaua mpira nitakubali,kwa sababu zifuatazo.
1.Pamoja na kuiwakilisha Nchi mara zote hizi.Sijaona mafanikio yeyote.
2.Marefa wengi wameonekana dhahiri kuitengenezea matokeo but kimataifa wanaenda kutalii.
3.Wanaua vipaji bora kabisa hapa Tz.Mfano Mwashuya angekuwa simba sasa hivi,tungeongea mengine.Ni hayo tu!
 
Ukiniambia Yanga inaua mpira nitakubali,kwa sababu zifuatazo.
1.Pamoja na kuiwakilisha Nchi mara zote hizi.Sijaona mafanikio yeyote.
2.Marefa wengi wameonekana dhahiri kuitengenezea matokeo but kimataifa wanaenda kutalii.
3.Wanaua vipaji bora kabisa hapa Tz.Mfano Mwashuya angekuwa simba sasa hivi,tungeongea mengine.Ni hayo tu!
1.simba imeshiriki mara nyingi tu kombe la shirikisho na klabu bingwa ni lini imewahi kuchukua?

2.katika ligi ya Tanzania ( VPL) ni timu ya simba pekee yenye historia ya kuhonga marefa (RUSHWA) na ikafikia hatua likawa ni jambo la kawaida (HAWANA HOFU) hadi kupelekea mchezaji wa zamani wa simba ULIMBOKA kukamatwa na kitita cha pesa kwa ajili ya kuhonga marefa waziwazi.


3.simba kuna wachezaji vijana akina mwaliazi, Ndemla, Mkude, Hajibu, Isihaka nk.... wameshindwaje kuwa wachezaji wazuri na bora kiasi cha kuisadia timu yao angalau kubeba ubingwa wa VPL tangu misimu minne sasa? Kama walivyofanya vijana wenzao akina Msuva, Kaseke, Telela, Abdul, Hajiwinyi nk.
 
Dawa ni kuzivunja tu...sababu zinawafanya watanzania kama wewe upeo wako wa kufikiri uishie msimbazi na jangwani na wachezaji nao kitu cha maana sana kwao ni kuifunga simba au yanga..wala hawafikirii siku moja wawe mabingwa wa afrika...tumeona mazembe wakifika fainali hizo mara tano sasa...halafu ww unatetea timu mf simba hata uwanja wa mazoezi hawana tangu 1934
Kwani Mazembe wametwaa ubingwa wa Afrika kwa kuziua akina Vita na TK Lumpopo?
 
Sasa faida yetu simba na yanga ni nini?au ndio wa tz tumezoea kuishi ki mazoea,haya leo tena simba wamefukuza kocha...eti ndio sababu ya wao kufanya vibaya nadhani si sawa ..
 
Simba hao ambao unawaona mafala ndio waliotengeneza njia kwa mtanzania wakwanza kutwaa tuzo ya CAF.sema tatizo ninaloona hapa ni rushwa iliyotamalaki kwa marefa.Ili simba ionekane haifai.

ha ha hhaaa ha duh! aisee huu unazi ndo umetufikisha hapa... hata ukifungwa 3-0, unasema tumefungwa kwa taaabu goli 3
 
Hawa ndio wanaosadifu kauli ya mzee Mwinyi tz kichwa cha wendawazimu kazi kupiga pesa tu
 
Wanaoweza kuziua timu hizi, ni wanachama wenyewe.

Hawa wapiga kelele wengine hawana hoja za msingi. Ni watu waliojikatia tamaa na walioamua kutafuta njia za mkato.
Suluhu ya mpira wetu ni kuufanya uwe wa kibiashara. Simba na Yanga hazijazuia Mtibwa kuwa kama TP Mazembe, au Mbeya City kufikia angalau kiwango cha KCCA ya Uganda.

Tuache uvivu, tusitafute mchawi. Timu za mikoani zijipange kuondoa ufalme wa Yanga na Simba uwanjani na sio mbwembwe za mdomoni au kwenye vyombo vya habari
 
Last edited:
wewe fwaaala...hatutaki historia tunataka mpira
Kweli kabisa mkuu. Watu hawa siasa imewafanya kuwa Mazuzu. Hizo timu zake hata viwanja vyake vyenyewe vya kufanyia mazoezi havina. Je anaifahamu Cosmopolitans huyu?
 
Wanaoweza kuziua timu hizi, ni wanachama wenyewe.

Hawa wapiga kelele wengine hawana hoja za msingi. Ni watu waliojikatia tamaa na walioamua kutafuta njia za mkato.
Suluhu ya mpira wetu ni kuufanya uwe wa kibiashara. Simba na Yanga hazijazuia Mtibwa kuwa kama TP Mazembe, au Mbeya City kufikia angalau kiwango cha KCCA ya Uganda.

Tuache uvivu, tusitafute mchawi. Timu za mikoani zijipange kuondoa ufalme wa Yanga na Simba uwanjani na sio mbwembwe za mdomoni au kwenye vyombo vya habari
Mkuu. Ukweli Simba na Yanga zinabebwe na serikali, mfano bungeni kuna wabunge wa pande hizo mbili wakicheza kupunguza mafuta.
 
Ukiniambia Yanga inaua mpira nitakubali,kwa sababu zifuatazo.
1.Pamoja na kuiwakilisha Nchi mara zote hizi.Sijaona mafanikio yeyote.
2.Marefa wengi wameonekana dhahiri kuitengenezea matokeo but kimataifa wanaenda kutalii.
3.Wanaua vipaji bora kabisa hapa Tz.Mfano Mwashuya angekuwa simba sasa hivi,tungeongea mengine.Ni hayo tu!
Mbona Mwalyanzi Yuko hoi,Maguli naye alikuwa Yanga? Kiongera naye je?
 
Back
Top Bottom