Kuvua samaki Ziwa Victoria

Kuvua samaki Ziwa Victoria

amu

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2012
Posts
16,143
Reaction score
31,297
Well wadau mie ni muajiriwa kanda ya ziwa bukoba katerero moja kwa mtu binafsi ila kuchomoka dakika 2 tatu kwa siku naweza.
Simnajua tena vimshahara vya waswahili nafikiria kuzungusha hela kidogo izae kuliko kuiweka benki haizai.
Wazo lililonijia ni kukodi mtumbwi yes kukodi nimepeleleza kama 400,000 mmoja unakaa nao si mda maalum mpaka hela yako itakaporudi na kifaida kidogo.
Naombeni ushauri wenu mtu aliyenipa hilo wazo kaniambia inalipa sana.
Naomba mawazo yenu wataalam kuhusu hii biashara.
Well pesa nliyonayo cash inahang hang ni 1,000,000.
Naombeni mawazo ya kitaalamu zaidi au kama kuna biasharq nyingine huku mnishtue.
 
hapa sidhani kama utapata info za maana, ongea na wavuvi ziwani uwaskilize wanalaza sh ngapi kwa siku, pia utalazimikak upata wavuvi waaminifu au uwe na ndugu yako anaenda majini, la unaweza kupata wahuni wanauza samaki hukohuko ziwani wanakwambia leo sku mbaya kweli bosi! ongea na wavuvi peleleza.
 
Humu watu wengi wanajifanya kila Mtu katokea Dar.. Ziwa hawalijui kabisa... huko wanapaita mikoani

Mimi kama nataka kujua kitu very sensitive mfano biashara ya Hiace huwa nauliza Driver au Konda,kama ni biashara ya Kantini huwa nauliza mama ntilie humu majibu si ya kuridhisha hata kidogo utapata ushauri tu zaidi ya hali halisi yenyewe

Mfano kuna mtu alitoa ufafanuzi humu wa kilimo fulani hivi alipotoa makadirio ya Mtaji nikaweka mikono juu ni zaidi ya milioni 20 ya kuanzia Kilimo... mmmmmmmh nilipoenda kwa wakulima kabisa na tena wanatumia mbinu za kisasa hata haikufika milion 8...

Kwahiyo Nenda kwa Wahusika zaidi kuliko humu
 
hapa sidhani kama utapata info za maana, ongea na wavuvi ziwani uwaskilize wanalaza sh ngapi kwa siku, pia utalazimikak upata wavuvi waaminifu au uwe na ndugu yako anaenda majini, la unaweza kupata wahuni wanauza samaki hukohuko ziwani wanakwambia leo sku mbaya kweli bosi! ongea na wavuvi peleleza.

Ahsanteee nami ndo najiandaa leo kwenda kupeleleza huko
 
Humu watu wengi wanajifanya kila Mtu katokea Dar.. Ziwa hawalijui kabisa... huko wanapaita mikoani

Mimi kama nataka kujua kitu very sensitive mfano biashara ya Hiace huwa nauliza Driver au Konda,kama ni biashara ya Kantini huwa nauliza mama ntilie humu majibu si ya kuridhisha hata kidogo utapata ushauri tu zaidi ya hali halisi yenyewe

Mfano kuna mtu alitoa ufafanuzi humu wa kilimo fulani hivi alipotoa makadirio ya Mtaji nikaweka mikono juu ni zaidi ya milioni 20 ya kuanzia Kilimo... mmmmmmmh nilipoenda kwa wakulima kabisa na tena wanatumia mbinu za kisasa hata haikufika milion 8...

Kwahiyo Nenda kwa Wahusika zaidi kuliko humu

Ahsante umensaidia mwee
 
Hongera amu,kuwa na uthubutu thabiti,tafuta taarifa sahihi kwa wavuvi na wadau wengine wa mazao ya samaki then utakuwa katika nafasi nzuri ya kuamua. Kemondo si mbali sana,nenda hapo ukate taarifa sahihi.
 
Jamani watu humu ndani munataka kusikia noah,vitz,malteza na miandroid sijui mitablet.
Poa tu kesho ndo nawnda kemondo kuulizia zaidi
 
Hongera amu,kuwa na uthubutu thabiti,tafuta taarifa sahihi kwa wavuvi na wadau wengine wa mazao ya samaki then utakuwa katika nafasi nzuri ya kuamua. Kemondo si mbali sana,nenda hapo ukate taarifa sahihi.

Kesho ntakuwa hapo wangu nitawapa mrejesho
 
Kwa laki nne unakodi kwa muda gani ? na je huo ni mtumbwi wa injini au na makasia alafu bado haujatia nyavu .., binafsi mimi sijafanya biashara hii ila najua kununua mtumbwi na injini ni pesa ndefu kidogo na kwa hii mitumbwi ya injini sometimes mtu anakwenda kutupa nyavu anarudi na kurudisha pesa ya mafuta tu (kwahio kupata sio guarantee). Kwa ushauri wangu ili ku-taste the water na kwa mtaji wako kama wateja wapo jaribu kwanza kulangua samaki kutoka kwa wavuvi na kuziuza.., ni mengi yapo huko majini na changamoto nyingi as well as imani za ajabu ajabu
 
Kwa laki nne unakodi kwa muda gani ? na je huo ni mtumbwi wa injini au na makasia alafu bado haujatia nyavu .., binafsi mimi sijafanya biashara hii ila najua kununua mtumbwi na injini ni pesa ndefu kidogo na kwa hii mitumbwi ya injini sometimes mtu anakwenda kutupa nyavu anarudi na kurudisha pesa ya mafuta tu (kwahio kupata sio guarantee). Kwa ushauri wangu ili ku-taste the water na kwa mtaji wako kama wateja wapo jaribu kwanza kulangua samaki kutoka kwa wavuvi na kuziuza.., ni mengi yapo huko majini na changamoto nyingi as well as imani za ajabu ajabu

Ha ha mambo ya kuenda kwa babu kulala uchi?
Anyway mleta data alinipa hilo nkifika ntajua zaidi well mtumbwi hela zipo ila am not risk taker nataka nione inaendaje nimetenga hiko kiasi well ntaendelea.
Nimependa nipe data zaidi
 
Ha ha mambo ya kuenda kwa babu kulala uchi?
Anyway mleta data alinipa hilo nkifika ntajua zaidi well mtumbwi hela zipo ila am not risk taker nataka nione inaendaje nimetenga hiko kiasi well ntaendelea.
Nimependa nipe data zaidi
Ushauri wa mdau hapo juu, ni wa muhimu sana, pia ni muhimu kujua hata bei ya samaki au dagaa, inabadika sana, ndani ya masaa huwa inategemea na upatikanaji wa mazao hayo, ukiona biashara inayokimbiwa na muhindi uwe nayo makini sana
 
Ha ha mambo ya kuenda kwa babu kulala uchi?
Anyway mleta data alinipa hilo nkifika ntajua zaidi well mtumbwi hela zipo ila am not risk taker nataka nione inaendaje nimetenga hiko kiasi well ntaendelea.
Nimependa nipe data zaidi

Kama unataka sana hii biashara na upo serious na pesa ipo au una watu wa kuwaamini unaoweza kuwatuma kuvua sio vibaya pia ukaongea na VICFISH; nadhani kuna wakati walikuwa wanakupa contract na msaada kabisa wa kukuongezea boti au injini kwa mkopo unakuwa unavua na kuwapelekea uzuri wa hili ni kwamba unakuwa na uhakika wa soko; sio vibaya ukawauliza terms zao pia kama wapo mpaka Bukoba (what I know ni wapo Mwanza).

All in all ni biashara ngumu hii kwahio fanya research ya nguvu na anza kidogo kidogo upate experience
 
Ushauri wa mdau hapo juu, ni wa muhimu sana, pia ni muhimu kujua hata bei ya samaki au dagaa, inabadika sana, ndani ya masaa huwa inategemea na upatikanaji wa mazao hayo, ukiona biashara inayokimbiwa na muhindi uwe nayo makini sana

Daa ahsante kwa angalizo
 
amu unataka kuvua samaki na kuuza kwa mawakala au kuuza mwenyewe kiwandani..? kama ni kiwandani ongeza mtaji hautoshi
 
Back
Top Bottom