Ndugu wana JF,
Nimesikitishwa sana na habari kuwa jumba la sanaa limehamishwa ili kupisha ujenzi wa gorofa ya kigogo mmoja ambaye alishawahi kuwa waziri mkuu. Jumba hili ni la muhimu sana na lipo tangia wakati wa mwalimu.
Inasikitisha kuona nchi inakwenda kishkaji kwa kufanya mambio kwa manufaa ya watu wachache. Wakati wa Mzee ruksa waliuza sana viwanja vya wazi nakumbuka hapo mnazi mmoja watu walivamia kuchukua mabati na matofali.
Tuwe shupavu pia kama serikali inauza mali ya umma kama hivi kuna siku watauza ikulu. Tungekataa na hata wakilazimisha tukavunje uzio pale. Nchi hii imefika mahali tutumie nguvu ya umma kidogo kupambana na wahuni wachache wanataka kujiuzia kila kitu.
Tanzania ipo mikononi kwetu tuilinde hata kama tutalipa gharama kidogo
Nimesikitishwa sana na habari kuwa jumba la sanaa limehamishwa ili kupisha ujenzi wa gorofa ya kigogo mmoja ambaye alishawahi kuwa waziri mkuu. Jumba hili ni la muhimu sana na lipo tangia wakati wa mwalimu.
Inasikitisha kuona nchi inakwenda kishkaji kwa kufanya mambio kwa manufaa ya watu wachache. Wakati wa Mzee ruksa waliuza sana viwanja vya wazi nakumbuka hapo mnazi mmoja watu walivamia kuchukua mabati na matofali.
Tuwe shupavu pia kama serikali inauza mali ya umma kama hivi kuna siku watauza ikulu. Tungekataa na hata wakilazimisha tukavunje uzio pale. Nchi hii imefika mahali tutumie nguvu ya umma kidogo kupambana na wahuni wachache wanataka kujiuzia kila kitu.
Tanzania ipo mikononi kwetu tuilinde hata kama tutalipa gharama kidogo