Kutoka Wanamtandao mpaka mapacha 3(RACHEL)!Hakika malipo ni hapahapa duniani.

Jasho la Damu

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
956
120
Mwanzoni mwa Mwaka 2005 kulishamiri kundi moja la watu maarufu hapa TZ liloitwa Wanamtandao. kundi hili lilianza rasmi mwaka 1995 ambalo vision na mission yake ni kuongoza Serikali ya JMT(URT). mwaka 1995 walishindwa kutimiza ndoto yao baada ya Late Mwl JK Nyerere kuwastukia hasa pale walipomkodishia ndege kada wao kwenda Dodoma ili akachukue fomu za kugombea Urais kupitia CCM na kisha nyerere kuhoji ikiwa leo wanatumia ndege kuchukulia fomu wakifika ikulu itakuwaje?
 
Kwa bahati ya mtende mwaka 2005 miaka 6 baada ya kifo cha Nyerere kundi hili liliweza kujijenga tena na kutumia kila aina mbinu kuwaaminisha CCM na watz kuwa wao ndio wanapaswa kukamata dola bila tatizo lolote walifanikiwa kwa kiasi kikubwa tena kwa moyo mkunjufu wa watz karibia wote.
Ikumbukwe ya kwamba ni kundi lililotuaminisha kuwa Salim A Salim ni mwarabu pia Mwandosya si mtu safi na kutengeneza makundi ya kikabila ndani ya jiji la mbeya.
leo tunaona kundi limegawanyika na kubaki mapacha 3 tu.
 
Back
Top Bottom