KERO Kusitishwa muda mrefu kwa huduma ya vyoo vya Stendi ya Mawasiliano kunasababisha kero kwa wananchi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bawabu wa pili

Senior Member
Joined
Nov 14, 2025
Posts
147
Reaction score
432
Stendi ya Mawasiliano ni eneo lenye muingiliano mkubwa wa watu kutokana na uwepo wa soko pamoja na mabanda mengi ya biashara. Licha ya umuhimu mkubwa wa eneo hilo, upatikanaji wa huduma ya choo kwa sasa ni changamoto kubwa, hali inayosababisha usumbufu kwa wafanyabiashara, wananchi wanaofika sokoni, pamoja na abiria.

Nilipofika eneo la soko, nilishuhudia baadhi ya watu wakilazimika kujisitiri haja ndogo nyuma ya jengo la choo, kwenye majani. Nilipouliza sababu ya kutotumia vyoo vilivyopo ndani, niliambiwa kuwa vyoo hivyo vimefungwa kwa zaidi ya mwezi mmoja kwa madai ya kufanyiwa marekebisho.

Baada ya kufuatilia zaidi, niliona tangazo dogo la karatasi lililobandikwa kwenye mlango wa choo likieleza kuwa vyoo hivyo vimefungwa kupisha ukarabati, na kwamba wananchi watumie vyoo vilivyopo katika stendi ya zamani.

Hata hivyo, kwa mazingira halisi, vyoo vya stendi ya zamani vipo mbali na eneo la soko, jambo linalolalamikiwa na watu wengi hususan wanawake. Hali hii inawalazimu baadhi ya wananchi kutumia maeneo yasiyo rasmi kama mbadala wa choo, jambo linalohatarisha afya na mazingira.

Kinachozidi kuwashangaza wananchi ni kwamba, licha ya madai ya ukarabati, hakuna dalili zozote za uboreshaji au kazi zinazoendelea katika eneo hilo kama jitihada za kurejesha huduma hiyo muhimu kwa jamii.

Kutokana na hali niliyoiona, kuna dalili za uzembe na kutokuwajibika kwa baadhi ya watendaji husika. Hivyo nitoe wito kwa Manispaa ya Ubungo kuhakikisha huduma za choo zinarejeshwa kwa haraka. Endapo kuna maboresho yanayohitajika kufanyika, basi jitihada za dhati na za haraka zichukuliwe ili kuondoa kero hii inayowaathiri wananchi kwa muda mrefu.



Pia soma
~
Manispaa ya Ubungo: Vyoo viwili eneo la Stendi ya Simu 2000 vimesitishwa kwa muda kutokana na changamoto ya kujaa maji mara kwa mara

~ Kero: Vyoo vya Simu 2000 ni vichafu sana
 
Ukarabati unaanza soon baada ya kuchomwa moto Oct 29

Kuhusu vyoo vinafanya kazi, Pump ilikufa nimepata taarifa imeshanunuliwa na inafanya kazi

Niliambiwa juzi na mtu wa hapo

Sasa sijui hizi taarifa za kukosekana huduma ya choo ni za lini?

Naomba niambie nipige simu muda huu nikupe taarifa ,

Mimi ni mmoja wa wahusika wa miradi ikiwepo huo wa mawasiliano
 
Zaidi ya mwezi mnatengeneza nini, na mpaka leo hakuna kitu kuna mtu kaanzisha uzi mwingine, kama unahusika you should be ashamed of yourself
 
Hii stendi ilipofunguliwa ilikuwa safi sana mpaka WI-FI ilikuwepo!
Mbeleni sasa mdg mdg ukaanza kuwa ovyo

Ova
 
Zaidi ya mwezi mnatengeneza nini, na mpaka leo hakuna kitu kuna mtu kaanzisha uzi mwingine, kama unahusika you should be ashamed of yourself
Unadhani ni rahisi tu Mzee, Kuna mifumo ya umeme,maji lazima izingatiwe ,pale Pana Hali ya maji ,mashimo yanajaa
 
Hii stendi ilipofunguliwa ilikuwa safi sana mpaka WI-FI ilikuwepo!
Mbeleni sasa mdg mdg ukaanza kuwa ovyo

Ova
Wewe ni muongo.
Stendi pekee ilowahi kuwa na public WiFi ni Makumbusho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…