nkyandwale
Member
- Feb 8, 2011
- 64
- 14
kusinzia ugenini !
1. Jamani nambieni,ukweli nipate jua
Ee malenga toboeni, hata kwa kusoma dua
Hapa bara hata pwani, dhana hii pembua
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini ?
2. Safari kuipigania, hata ndururu kutoa
Mwanaume kupania, kwa waridi kujitoa
Waridi kukaribia, hata siri kutoboa
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini?
3. Ua kupata mgeni ,hasa mkiki murua
Mizigo kutunzwa ndani, waridi nyama pakua
Kitanda hakitamani, ujasiri humpungua
Kusinzia ugenini , maana yake ni nini ?
4. Ujasiri hupungua, maungo kumlegea
Mbio hawezi timua, usingizi kumkolea
Hutweta kwa kupumua, waama akielea
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini?
5. Tano naweka kifungo, jibu jema nasubiri
Sitegemei magongo, na msuto wa kiburi
Akifikia ukingo, ajiona yu saburi
Kusinzia ugenini , maana yake ni nini?
Nkyandwale.
1. Jamani nambieni,ukweli nipate jua
Ee malenga toboeni, hata kwa kusoma dua
Hapa bara hata pwani, dhana hii pembua
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini ?
2. Safari kuipigania, hata ndururu kutoa
Mwanaume kupania, kwa waridi kujitoa
Waridi kukaribia, hata siri kutoboa
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini?
3. Ua kupata mgeni ,hasa mkiki murua
Mizigo kutunzwa ndani, waridi nyama pakua
Kitanda hakitamani, ujasiri humpungua
Kusinzia ugenini , maana yake ni nini ?
4. Ujasiri hupungua, maungo kumlegea
Mbio hawezi timua, usingizi kumkolea
Hutweta kwa kupumua, waama akielea
Kusinzia ugenini, maana yake ni nini?
5. Tano naweka kifungo, jibu jema nasubiri
Sitegemei magongo, na msuto wa kiburi
Akifikia ukingo, ajiona yu saburi
Kusinzia ugenini , maana yake ni nini?
Nkyandwale.