Papaa Muu
JF-Expert Member
- Nov 6, 2018
- 243
- 292
Tarehe 25/5/2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Dkt.John Pombe Magufuli aliudhuria kuapishwa kwa mshindi wa ugombea urais wa South Africa.Wakati wa kuingia alipotajwa tu kuwa anayeingia ni Rais wa Tanzania umati ukaamka kushangilia kwa nguvu mpaka alipoenda kuketi,nini sababu kubwa ya kushangiliwa huko.
Tukiacha urafiki undugu umoja nk uliopo baina ya Tanzania na South Africa kuna jambo jipya limetokea toka aingie madarakani Rais Magufuli.
Ni miaka mingi waafrika wamekuwa wakishuhudia aina ya viongozi ambao wameshindwa kusimamia rasilimali za nchi zao na kushindwa kukemea ubadhirifu unaofanywa na baadhi ya viongozi ambao walipata kushika madaraka na kushindwa kukemea maovu kama rushwa nk.hili limewachosha waafrika nakuanza kuombea watu wakukemea haya yakatengemaa,sasa kwa Africa wamemshuhudia si mwingine ni Rais wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.
Waafrika wameona na wameshuhudia juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt.JPM ikifanya yale kwa miaka mingi yalikuwa yanaonekana kushindikana kufanywa mpaka ikasemekana labda waafrika watawaliwe tena ndio itafanyika,waafrika waliamini rushwa ni sehemu ya maisha kuwa lazima uitoe au upokee lakini Rais wa Tanzania amekuja akaanza vita na wala rushwa na watoa rushwa kwa vitendo kabisa mpaka ikawa nimfano wa kuigwa na nchi zingine huku wakishuhudia mialiko mfano ya uingereza ambayo ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na waziri mkuu wa Tanzania walialikwa kueleza namna Tanzania ilivyofanikiwa kupambana na rushwa.
Wengi wa waafrika waliamini itakuwa ngumu kwa nchi za Afrika kusimamia rasilimali zake zikaleta maendeleo lakini Tanzania chini ya Rais Dkt JPM imeonyesha mfano kuwa inawezekana kusimamia rasilimali na kuziongezea thamani kwa kuhakikisha nchi inapunguza kuuza malighafi kama malighafi bali inajikita katika kuuza bidhaa iliyokamilika ambayo ina thamani zaidina kuiletea nchi faida kubwa,hii mfano utaona wengi waliona ni ngumu kuzikemea kampuni kubwa za nje kwa kunyonya nchi changa malighafi hivyo Rais Dkt John PM alizuia makontena zaidi ya mia yenye mchanga wa madini na madini akatambulisha sera mpya ya madini akavunja mikataba mibovu isiyo na tija kwa nchi na kuwafanya hayo makampuni kuomba maongezi ya makubaliano na kukubali kulipa kodi waliyokuwa wanakwepa pamoja na fedha ingine kwa nchi,jambo ambalo ulimwengu mzima haukuamini kama linawezekanika kwa nchi changa kushindana ubabe na makampuni haya ambayo yalionekana yasiyogusika lakini Rais Magufuli kayagusa na yanabadilika sasa nchi inaona faida ya ilichonacho.
Waafrika walizoea kuona ili kufanikiwa lazima Rais kila wakati asafiri nje mara kwa mara lakini kwa sasa wengi wameshangazwa na Rais JPM ambaye mpaka wakati huu hajatoka nje ya bara la Afrika bali ameweza kuonyesha kwa nini nchi inakuwa na balozi(wawakilishi)nje,ameweza kufuta safari za wafanyakazi za nje ya mchi zisizo na tija kwaasilimia kubwa ukiacha zakemwenyewe ambapo mpaka sasa waafrika wameona kumbe inawezekana kabisa kwa Rais kutokutoka nje ya bara la Afrika akabana matumizi makubwa yanayofanyika kwasafari hizi za nje hivyo akawa na safari chache sana ambazo ukipiga hesabu mpaka sasa inawezekana Rais wa Tanzania akawa katoka nje ya nchi yake kwenda nchi zingine za Afrika haifikii hata mara mia ukilinganisha na marais wengine wa Afrika ambao hufikisha hata safari mia nne kwenda nje ya afrika.
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo waafrika wanayaona kwa macho yao na kuyasikia na kuthibitisha kuwa kumbe yanawezekana,kwa waafrika imekuwa ni kama Rais Magufuli anarudisha heshima ya waafrika ile yakuonekana hawawezi kujiamulia mambo yao bila kuamuliwa na nchi kubwa na kuonyesha kuwa hata waafrika wanaweza wakasimamia nchi zao vizuri naa zikaendelea.Hii imemfanya Rais Dkt John P.Magufuli kuwa ndio mfano wakuigwa kwa marais wa Afrika na waafrika wengi wangependa marais wa nchi zao wafanye haya anayoyafanya Rais Magufuli kwa nchi yake.
Nani asiyejua ukweli huu juu ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais JPM inavyofanyakazi nzuri kwa Tanzania ambapo hata wachumi ndani na nje wanaona na kukiri kuwa kama Tanzania itaendelea hivyo kwa miaka kumi basi jua baada ya muda Tanzania itakuwa iko juu kiuchumi,hili hata Waafrika wanalijua na kuliona ni zuri ndio maana wanataka liigwe,wanafahamu kuwa lazima kuna wasiopenda juhudi za hivyo ila je wapo kwa kujenga pamoja kwa kutoa mbinu B katika jambo baada yakuona mbinu A ya serikali au wapo kwa kuirudisha nchi yao nyuma kimaendeleo na kuiharibu kama vikwazo vya nje vinavyojitokeza kwa propaganda za ajabu,jibu analo atakayekuwa anakwamisha hapo,ila Waafrika wanalotaka ni kuona jambo zuri la Rais Dkt JPM liigwe na kuanza kazi kwa haraka kuondoa matatizo wanayoyapata wao nchini mwao...ndio maana kila anaposimama Rais wa Tanzania watu weengi hulipuka kwa shangwe na nderemo ukiacha vifijo visivyoisha kufikisha sauti zao kuwa anayoyafanya si madogo ni makubwa na ya maana sana ambayo yanahitajika kwa dunia ya sasa.
Ndio maana sikushangaa sana maana najua watu wa Afrika wanampima Rais wa Tanzania kwa kazi zake naye kama anavyosemaga "Sitawaangusha" na kweli wanaona "Hawaangushi" bali amezidi kufanya mazuri wayatakayo.
Hongera sana Watanzania kwa kumuunga mkono.
Hongera Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa mazuri yasiyohesabika unayoyafanya katika nchi hii nzuri ya Tanzania,unatuonyesha uzalendo wa hali ya juu,hatutakuwa nyuma yako bali tutakuwa bega kwa bega kukamilisha yote.
Acha Afrika ilipuke kwa shangwe ni heshima kubwa unaipa Afrika....Asante sana
Tukiacha urafiki undugu umoja nk uliopo baina ya Tanzania na South Africa kuna jambo jipya limetokea toka aingie madarakani Rais Magufuli.
Ni miaka mingi waafrika wamekuwa wakishuhudia aina ya viongozi ambao wameshindwa kusimamia rasilimali za nchi zao na kushindwa kukemea ubadhirifu unaofanywa na baadhi ya viongozi ambao walipata kushika madaraka na kushindwa kukemea maovu kama rushwa nk.hili limewachosha waafrika nakuanza kuombea watu wakukemea haya yakatengemaa,sasa kwa Africa wamemshuhudia si mwingine ni Rais wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.
Waafrika wameona na wameshuhudia juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt.JPM ikifanya yale kwa miaka mingi yalikuwa yanaonekana kushindikana kufanywa mpaka ikasemekana labda waafrika watawaliwe tena ndio itafanyika,waafrika waliamini rushwa ni sehemu ya maisha kuwa lazima uitoe au upokee lakini Rais wa Tanzania amekuja akaanza vita na wala rushwa na watoa rushwa kwa vitendo kabisa mpaka ikawa nimfano wa kuigwa na nchi zingine huku wakishuhudia mialiko mfano ya uingereza ambayo ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na waziri mkuu wa Tanzania walialikwa kueleza namna Tanzania ilivyofanikiwa kupambana na rushwa.
Wengi wa waafrika waliamini itakuwa ngumu kwa nchi za Afrika kusimamia rasilimali zake zikaleta maendeleo lakini Tanzania chini ya Rais Dkt JPM imeonyesha mfano kuwa inawezekana kusimamia rasilimali na kuziongezea thamani kwa kuhakikisha nchi inapunguza kuuza malighafi kama malighafi bali inajikita katika kuuza bidhaa iliyokamilika ambayo ina thamani zaidina kuiletea nchi faida kubwa,hii mfano utaona wengi waliona ni ngumu kuzikemea kampuni kubwa za nje kwa kunyonya nchi changa malighafi hivyo Rais Dkt John PM alizuia makontena zaidi ya mia yenye mchanga wa madini na madini akatambulisha sera mpya ya madini akavunja mikataba mibovu isiyo na tija kwa nchi na kuwafanya hayo makampuni kuomba maongezi ya makubaliano na kukubali kulipa kodi waliyokuwa wanakwepa pamoja na fedha ingine kwa nchi,jambo ambalo ulimwengu mzima haukuamini kama linawezekanika kwa nchi changa kushindana ubabe na makampuni haya ambayo yalionekana yasiyogusika lakini Rais Magufuli kayagusa na yanabadilika sasa nchi inaona faida ya ilichonacho.
Waafrika walizoea kuona ili kufanikiwa lazima Rais kila wakati asafiri nje mara kwa mara lakini kwa sasa wengi wameshangazwa na Rais JPM ambaye mpaka wakati huu hajatoka nje ya bara la Afrika bali ameweza kuonyesha kwa nini nchi inakuwa na balozi(wawakilishi)nje,ameweza kufuta safari za wafanyakazi za nje ya mchi zisizo na tija kwaasilimia kubwa ukiacha zakemwenyewe ambapo mpaka sasa waafrika wameona kumbe inawezekana kabisa kwa Rais kutokutoka nje ya bara la Afrika akabana matumizi makubwa yanayofanyika kwasafari hizi za nje hivyo akawa na safari chache sana ambazo ukipiga hesabu mpaka sasa inawezekana Rais wa Tanzania akawa katoka nje ya nchi yake kwenda nchi zingine za Afrika haifikii hata mara mia ukilinganisha na marais wengine wa Afrika ambao hufikisha hata safari mia nne kwenda nje ya afrika.
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo waafrika wanayaona kwa macho yao na kuyasikia na kuthibitisha kuwa kumbe yanawezekana,kwa waafrika imekuwa ni kama Rais Magufuli anarudisha heshima ya waafrika ile yakuonekana hawawezi kujiamulia mambo yao bila kuamuliwa na nchi kubwa na kuonyesha kuwa hata waafrika wanaweza wakasimamia nchi zao vizuri naa zikaendelea.Hii imemfanya Rais Dkt John P.Magufuli kuwa ndio mfano wakuigwa kwa marais wa Afrika na waafrika wengi wangependa marais wa nchi zao wafanye haya anayoyafanya Rais Magufuli kwa nchi yake.
Nani asiyejua ukweli huu juu ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais JPM inavyofanyakazi nzuri kwa Tanzania ambapo hata wachumi ndani na nje wanaona na kukiri kuwa kama Tanzania itaendelea hivyo kwa miaka kumi basi jua baada ya muda Tanzania itakuwa iko juu kiuchumi,hili hata Waafrika wanalijua na kuliona ni zuri ndio maana wanataka liigwe,wanafahamu kuwa lazima kuna wasiopenda juhudi za hivyo ila je wapo kwa kujenga pamoja kwa kutoa mbinu B katika jambo baada yakuona mbinu A ya serikali au wapo kwa kuirudisha nchi yao nyuma kimaendeleo na kuiharibu kama vikwazo vya nje vinavyojitokeza kwa propaganda za ajabu,jibu analo atakayekuwa anakwamisha hapo,ila Waafrika wanalotaka ni kuona jambo zuri la Rais Dkt JPM liigwe na kuanza kazi kwa haraka kuondoa matatizo wanayoyapata wao nchini mwao...ndio maana kila anaposimama Rais wa Tanzania watu weengi hulipuka kwa shangwe na nderemo ukiacha vifijo visivyoisha kufikisha sauti zao kuwa anayoyafanya si madogo ni makubwa na ya maana sana ambayo yanahitajika kwa dunia ya sasa.
Ndio maana sikushangaa sana maana najua watu wa Afrika wanampima Rais wa Tanzania kwa kazi zake naye kama anavyosemaga "Sitawaangusha" na kweli wanaona "Hawaangushi" bali amezidi kufanya mazuri wayatakayo.
Hongera sana Watanzania kwa kumuunga mkono.
Hongera Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa mazuri yasiyohesabika unayoyafanya katika nchi hii nzuri ya Tanzania,unatuonyesha uzalendo wa hali ya juu,hatutakuwa nyuma yako bali tutakuwa bega kwa bega kukamilisha yote.
Acha Afrika ilipuke kwa shangwe ni heshima kubwa unaipa Afrika....Asante sana