Kupaua nyumba

Joined
Feb 10, 2012
Posts
14
Reaction score
3
Habari zenu wakuu....

Naomba kuuliza kwa wenye uzoefu au mafundi ujenzi gharama za kupaua nyumba ya vyumba viwili vya kawaida vya kulala,master moja,choo na bafu vya public,dinning na sebule,stoo na jiko...

Je, kwa makadirio zitahitajika bati ngapi,mbao ngapi.

Angalizo: Nataka kupaua kwa kutumia mabati ya migongo mipana gage 28 na mbao za treated.
 
nicheki mimi whatsapp nitakusaidi kupata bati pamoja mbao vyote vinapatikana dukani kwetu.
0715426668
 
Hapo kwa haraka utahitaji bati 90+ mbao 150+ nk. Kama vp nitafute nikupe BOQ hapo tufanye kazi.....hyo kazi ya siku mbili tu
 
mbao 250 bati bandari 4 za futi 8 geji 30 chapa kiboko au chapa simba misumari ya bati kilo 12 misumar ya kawaida kilo 15 mchanganyiko makoa 50. Beem wire 5 gharama ya fundi laki 4 and above
 
Andaa kama 6m mbao , bati na ufundi.
 
mbao 250 bati bandari 4 za futi 8 geji 30 chapa kiboko au chapa simba misumari ya bati kilo 12 misumar ya kawaida kilo 15 mchanganyiko makoa 50. Beem wire 5 gharama ya fundi laki 4 and above

Toa mchanganuo na bei mkuu itasaidia na wengine pia....
 
nicheki mimi whatsapp nitakusaidi kupata bati pamoja mbao vyote vinapatikana dukani kwetu.
0715426668

Mkuu toa bei ya bati na mbao na zinapatikana wapi ili iwe msaada na kwa wengine pia ndo lengo la kuleta huu uzi hapa....
 
nicheki mimi whatsapp nitakusaidi kupata bati pamoja mbao vyote vinapatikana dukani kwetu.
0715426668
mbao sh ngapi?
Bati sh ngapi?
Gharama usafiri
kushusha/kupakia
discount ipo kwa mzigo wa sh ngapi?
Je ni buguruni? Na kama ndio usalama wa fedha
na madalali/mtu kati uko vp?
 
Ungetoa vipomo vya nyumba ungepata exact amount ya bati na mbao.. Kwa makadirio hayo tegemea pia kupewa makadirio yasiyo na uchanganuzi sahihi..
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…