Kupatikana au kutoonekana kwa Ben Saanane, Tunataka kipi zaidi ya hiki?

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Kwa mwenye akili timamu akimsikiliza Mh Zitto Kabwe wakati akichangia bungeni ataelewa ni wapi aliko Ben Saanane, haina haja ya kumung'unya maneno, tuukatae uonevu huu.Ben Saanane kwa mujibu wa hotuba ya Zitto sio wa kutafutia porini wala kwenye mito au madimbwi ya maji bali maelezo na hoja zake zimeshatoa jibu.


Katika hotuba yake Mh Zitto alisema kua kila zinapofuatiliwa suala hili polisi, majibu yanayopatikana ni kwamba taarifa za simu yake zinsonesha kua siku ya kupotea kwake alikua Tababta, baadae Mikicheni ambako inasemekana ilikaa muda murefu na mwisho kabisa ikawa Mburahati na kupotea moja kwa moja,Zitto alizidi kusema kua "ukifuatilia zaidi polisi haupati taarifa za kueleweka ispokua nao wanasema kua inaonekana Ben Saanane ni kama amechukuliwa na usalama wa taifa".Ama kwa hakika jibu juu ya huyo ndugu yetu liko wazi.


Pili ukisikiliza maneno ya ndugu Nape Nnauye ambaye juzi tu alikua Afisa ngazi ya juu serikalini, bado unaweza kuunganisha dots ukapata jibu.Nape kama alikua ni kiongozi wa srikali ni imani yangu kua anafahamu mengi sana juu baadhi ya mambo yanayiendelea serikalini wala asingebwatuka bure kule jimboni kwake Mtama ambapo alilalama sana kupotea kwa Ben Saanane.


Wadau,watu wa haki za binadamu ni wa kati wa kupaza sauti kwa kuzifanyia kazi taarifa za Zitto Kabwe ili huyu Binadamu Ben Saanane apatikane.Haina haja ya UTG kupiga kele sana ilihali pa kuanzia pako wazi.
 
Ben sanane aliongoza kikosi cha walisha watu sumu ambapo aliwahi kupanga mipango ya kumlisha zitto sumu..mipango hiyo iliumbuliwa na mtela mwampamba na mwenzake
 
Pia ben saanane alikuwa na mgogoro mkubwa na viongozi wengi wa chadema kwa kuwasemea uongo kwa mwenyekiti. Ndiye aliyesababisha hadi dr slaa kuiacha chadema kwa umbea wake. Mjitafute vizuri humo ndani ufipa
 
Pia ben saanane alikuwa na mgogoro mkubwa na viongozi wengi wa chadema kwa kuwasemea uongo kwa mwenyekiti. Ndiye aliyesababisha hadi dr slaa kuiacha chadema kwa umbea wake. Mjitafute vizuri humo ndani ufipa
Wewe ni mbumbu tangu lini ukayajua mambo?
 
Ben sanane aliongoza kikosi cha walisha watu sumu ambapo aliwahi kupanga mipango ya kumlisha zitto sumu..mipango hiyo iliumbuliwa na mtela mwampamba na mwenzake

Kwa sababu wewe ni Muhusika mkuu wa kumteka Ben na Roma basi umetumwa kupima Maji siyo??

Waambie yamejaa.
 
Kwa sababu wewe ni Muhusika mkuu wa kumteka Ben na Roma basi umetumwa kulima Maji siyo??

Waambie yamejaa.
Hawa vijana CCM wamechanganyikiwa, wamejawa madhambi na uchafu wa kila aina, unawapingaje kina Nape,Bashe na Msukuma CCM wenzio?
 
ungesema twende ufipa ningekuelewa. Barabara alizojenga magufuli ziache zipitishe magari

Barabara gani alizojenga Magufuli?? Magufuli anapesa za kutujengea Watanzania Barabara?

Kawadanganye Lumumba maneno hayo,mang'ombe bwana hamtumii hata Akili za kupewa tu.

Barabara zimejengwa na pesa za kodi zetu.
 
Hawa vijana CCM wamechanganyikiwa, wamejawa madhambi na uchafu wa kila aina, unawapingaje kina Nape,Bashe na Msukuma CCM wenzio?

Hawa Mkuu ndiyo wafanyaji wa kazi za kuteka na kutesa RAIA wasio na hatia.
 
Sikutegemea kama CHADEMA wangekaa kimya kwenye hili swala la Ben Saanane.

Ama kweli Tanzania kuna upinzani dhaifu sana.
 
Back
Top Bottom