Kupata chumba NHC

Spokesperson

Member
Joined
Sep 21, 2015
Posts
19
Reaction score
7
Habarini wadau,

Mbele yenu ninahitaji kupata chumba kimoja tu cha kuishi pale Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Shekilango au hata popote pale karibu na mji.

Nimesikia kuna ukiritimba na utapeli uliokithiri pia. Sasa ninahitaji msaada wa mtu yeyote kuniwezesha (kama inawezekana) kupata chumba. Nitampoza kama dalali pindi akinifanikishia jambo hili.

Ninahitaji nihamie mwishoni mwa mwezi huu.

Ninawakilisha!
 
Mkuu utapoteza muda, kipindi wanajenga za shekilango nlienda kuuliza zitangishwa vipi nikajibiwa zimeshajaa
 
Tens ulipewa wrong info coz
Mkuu utapoteza muda, kipindi wanajenga za shekilango nlienda kuuliza zitangishwa vipi nikajibiwa zimeshajaa
Tena ulipewa wrong info zile ni za watu binafsi waliwapa nhc % Fulani ya hela kuzinunua halafu nhc wakajenga zen % iliyobaki wanalipa kidogo kidogo
 
Tens ulipewa wrong info coz

Tena ulipewa wrong info zile ni za watu binafsi waliwapa nhc % Fulani ya hela kuzinunua halafu nhc wakajenga zen % iliyobaki wanalipa kidogo kidogo
Ina maana sio za Nhc mkuu?
 
Nakushauri tafta nyumba yyte itakayokufaa kuishi. Kutafta chumba NHC ni njozi utapoteza mda wako. Mbona ayo maeneo ya Sinza nyumba zipo kibao Mkuu.
 
Nyumba za nhc ni wahindi pekee ndio wanauwezo wa kuzipata lakini mtanzani thubutu
Sasa hizo tunazoishi sisi waafrica tumepataje, au tumepangishwa na wahindi kwa mtazamo wako?
 
Kama una ngozi nyeusi utapata kwa shida sana nakushaur unywe maji mengi angalau lita 20 kwa siku then mwisho wa mwezi uende ofisi za nhc utapata chumba.

Duc in Altum
 
Labda Watanzania wenye uwezo wa kununua nyumba za NHC ni wengi kuliko wenye uwezo wa kujenga za kwao binafsi. Am just wondering!!!
Hapo wanakua sio wanunuzi ni wapangaji
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…