Kupanda kwa bando la Internet

uniq

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2011
Posts
5,089
Reaction score
31,085
Habari wananchi wa Tanzania.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Kumekuwa na kupanda kwa bundle za internet kwa zaidi ya mara mbili kwa bei iliyokuwepo awali.

Swali langu kuu ni kwamba gharama za uendeshaji kwenye mitandao ya simu zimepanda?? Nakama zimepanda nini kimesababisha?

Je, inamaana Mama haoini kuwa wananchi tuna umea kwa kupandishwa kwa gharama?
Mbona Mama amekaa kimya tu?

Hapa chini ni baadhi ya bei za manunuzi ya liyopo kwa sasa kutoka mtandao wa Halotel.
1. Halotel 4G
2. Halotel kifurushi cha mwezi
3. Halotel kifurushi cha wiki

 
Sisi watumuaji wa Voda tulishazoea bei hiyo tangu tamko la Ndugulule
 
Labda tozo zimewachanganya ikabidi wapunguze tu
 
Hivi hakuna mbadala wa kupata internet bila kupitia haya makampuni ya simu, kwa nini wao tu ndio wawe internet provider? Tumewachoka kila mara kupunguza mabando wakati tunaihitaji sana huduma ya internet kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo
 
Hivi hakuna mbadala wa kupata internet bila kupitia haya makampuni ya simu, kwa nini wao tu ndio wawe internet provider? Tumewachoka kila mara kupunguza mabando wakati tunaihitaji sana huduma ya internet kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo
Noted.
 
SUBIRINI mpaka KIPINDI CHA UCHAGUZI KIKIFIKA, TUTAWAPUNGUZIA KIDIGO (yaani tutafunika kombe), ILI MWANA HARAMU APITE, baada ya hapo mwendo mdundo mpaka akili iwaingie!
 
Wanahisi labda mnawasema sana katika mambo yao........punguzeni matusi mitandaoni
 
SUBIRINI mpaka KIPINDI CHA UCHAGUZI KIKIFIKA, TUTAWAPUNGUZIA KIDIGO (yaani tutafunika kombe), ILI MWANA HARAMU APITE, baada ya hapo mwendo mdundo mpaka akili iwaingie!
Mi nawashauri mkaze hivi hivi hata kipindi cha uchaguzi kazeni hivi hivi. Naamini hamtaathirika kwa lolote,mtashinda tu.

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…