Kuondolewa Machinga Mijini

shinyangakwetu

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2015
Posts
2,487
Reaction score
2,394
Swala la machinga mijini limekuwa ni tatizo hasa kipindi cha awamu ya tano.

Tatizo hili linakua kwa kasi kwa sababu ya aina ya viongozi tulio nao.
Tanzania tuna viongozi kuanzia ngazi ya shina hadi taifa.

Sasa jiulize hawa watendaji wa mtaaa wanafanya nini.
Nashauri Mkuu wa mkoa Dar hangaika na watendaji watakaoshindwa kusimamia uondoshwaji wa machina sehemu zao.
Kesho ni 18/10 siku ambayo ni mwisho kwa machinga barabarani jijini Dar.

Kuanzia hapo pata taarifa toka kila mtendaji wa mtaa kuliko na machinga na chukua hatua
 
Tatizo ni serikali inajenga miundo mbinunisiyo rafiki kwa shughli za wananchi nchi..

Unajenga jengo kama la kisutu kisha unasema aje machinga kuuza wakati faida yake kwa siku ni ndogo kuliko ada ya pango kwa siku.

Machinga wanatakiwa kujengewa masoko sipo yanayo chukua eneo kubwa, na huduma kama za usafiri ziwepo..

Na hii inatakiwa kuwa sera kwamba kila mtaa uwe na eneo la soko na lisiwe karibu na mainroad.

Mfano ni mawasiliano, makumbusho etc.
 
Maandalizi ya utekelezaji wa zoezi hasa maeneo mbadala Kwa mwenye updates tasafali.
 
Wanatupiga sound tu.

Hivi hadi wale wa Kariakoo watawatoa?
 
Tuliipotosha maana halisi ya mmachinga.huyo ni mtu aisye na mahali pa kufanyia biashara yaani anatembeza biashara zake.sasa hiv hata mama ntilie ni mmachinga
 
Hivi wewe unajia pesa ya wamachinga wanayoingiza kwa siku pale kariakoo? Kwa taarifa yako pale kariakoo watu wanamiliki barabara wanachukua kodi kila siku
 
Kama movie vile. Zoezi lianze asubuhi mapemaaaa kabla hawajaanza kuweka makorokocho yao.
Zoezi tunalianza Leo tandika kuanzia sa 7πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hilo zoezi linahusu kariakoo na posta au huku buza tu?
 
"Wapiga kula wangu hawa waacheni". Haya maneno ndio yameleta shida yote hii. Mpaka juu ya mifereji kuna vibanda! Pedestrian walkways! Mbele ya maduka halali yanayolipa Kodi! Hakuna kitu kama hiki duniani. Wapangwe maeneo yaliyowekwa sbb kila nchi machinga wapi Ila Kuna maeneo muafaka kwa ajili yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…