Mkuu kumbe na wewe umemgundua. Najaribu kutafuta kigezo alichotumia kufananisha Chombo cha habari na Serikali nashindwa hata kumueka kundi gani, ni mshabiki? ni mjinga? ni chizi? au basi tu kama ulisema mkuu ,kuwa ni wale wale wakiulizwa leo ni nchi ipi ina mgogoro na Tanzania kuhusu ziwa Nyasa atajibu Zanzibar. What is Mwanahali? au kwa vile linamilikiwa na kiongozi wa CHADEMA? Kumbe unaweza kuwa mpenzi wa kitu fulani hadi ukawa kama roboti. Hawa ndiyo wanaotumiwa kutafuta mabadiliko ili baadaye nchi itumbukie shimoni, hivi mtu kama huyu leo hii kukawa na mabadiliko yanayosemwa atakuwa anajua nini maana yake ? Kazi ipo.