Kuna nini katika kinyesi cha binadamu??

Kasome sayansi ya darasa la sita juu ya mfumo wa utoaji takamwili. Kinyesi siyo takamwili bali ni mabaki ya chakula ambacho hakikumeng'enywa vyema hivyo bado kina virutubisho vinavyowafaa wanyama wengineo!
Mkuu umeongea kisayansi ila nachelea kusema kuwa mleta mada hatakuelewa maana yeye nia yake ni kuonyesha madhara ya kula nyama pendwa ya kitimoto.
 
sehem zenye njaa au vita kuna watu wanakula kinyesi chao na kunywa mkojo.
 
Kinyesi cha binadamu kwao ni chakula chenye bacteria wanaowasaidia kumengenya chakula kwenye matumbo yao...


Cc: mahondaw
 
Sio mbwa na nguruwe tu hata madaktari huhitaji kinyesi chako wakipeleke maabara kwa uchunguzi zaidi. Kinyesi cha binaadamu hubeba mambo mengi sana


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Epilepsy inaletwa na cyst wa Taenia solium, ambapo nguruwe ndo host wa minyoo hao. NB. Siyo kila nguruwe na Taenia cyst.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yah upo sahihi and mtu akila nyama ya nguruwe hata kama ana hao Taenia Solium hapati Epilepsy bali anapata Taeniasis ambao n ugonjwa unaoaffect sanasana mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na kusababisha kuharisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu; hoja yako imesheheni maswali meeengi lakini mm naona hoja ya msingi kwako (Kwa mujibu wa sentensi ya mwisho) "kuna madini lishe gani ktk kinyesi cha binadamu"?
Hapo juu #8 umeambiwa sio vyakula vyote alavyo binadamu vinakuwa digested and absorbed. Ili kufahamu kuna madini lishe gani ktk kinyesi (Mavi) ya binadamu na uweze kuthibitisha kisayansi (ukizingatia watu hutofautiana ktkt uwezo wa kusaga chakula tumboni) unahitaji kufanya Research - Digestibility studies kwa kutumia Kjedal method.
Lakini usikae utegemee watu wataacha kula nyama-pendwa ya mdudu yule kwani ile nyama inakaguliwaga na Wataalam na kupitishwa as "Fit for Human Consumption" na kugongwa muhuri wa kuthibitisha - Government Inspected Carcass. Kwa hiyo acha watu watandike kitu roho inapenda aisee.
Kwa ufupi, kinyesi cha binadamu kina kitu kinaitwa Bilirubine & biliverdine inayotokana na nyongo (Bile) na hii ndio inasababisha harufu ya mavi ya binadamu tofauti na mavi ya mnyama mwingine. Kinyesi cha binadamu, hata kabla hujakiona, utajua tu kwamba kuna mavi ya binadamu mahali hapo. Sasa wanyama mbwa na nguruwe huvutiwa na harufu hiyo ambayo kwako ww ni mbaya lakini kwao ni uturi!.(Harufu ya kuvutia).
Lakini pia umetajiwa wanyama wengine ambao nao hula kinyesi cha binadamu. Ingefaa uone kwamba kile ww unadhani ni uchafu; kwa viumbe wengine hiyo ni chakula.(samahani lakini).
 
Umejitahidi kufafanua kidogo, ila naomba niwatoe watu skepticism au steretypism ya mada yangu wakidhani mm napinga kula nguruwe. Mm lengo langu ni kupata elimu kwa kuwa jukwaa hili ni kubwa ina watu wa cadre nyingi japo na vilaza pia wapo ila poa. Labda kwa kufuta hiyo stereotypical thinking, Leo hii mida ya saa saba lunch yangu nilipata Mbeya, Ilomba ambapo nilikula NGURUWE NA NDIZI, NILI ENJOY SANA NYAMA PENDWA SANA, ILA NATAKA NIJUE HUYU MNYAMA ALIVO MTAMU NA MAISHA YAKE, NA HASA KUNA SAYANSI GANI NYUMA YA HUYU MNYAMA? IS MATTER OF curiosity TU.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanakuja mkuu kukujibu mpaka hao uliowaita vilaza ambao wamo humu..mkuu uweke pia na akiba ya maneno Usichukulie poa nyumba ni choo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…