Kuna future hapa?

PLL

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2013
Posts
882
Reaction score
400
Habari zenu wanajamvi...nashindwa kumuelewa huyu mpenz wangu ni yule mtu ambaye ikitokea mmekorofishana atakuongelea maneno machafu sana yan hauamin kama yametoka katk kinywa chake,ivi karibuni umetokea ugomvi kidogo amenitamkia maneno ambayo kila nikimuona napatwa na hasira sana anajidai kuomba msamaha,je huyu n mtu naeweza kuishi nae kwa amani pindi tutakapofunga ndoa?
 
achana nae bwana....mapenzi raha sasa maneno machafu ya nini tena
 
Kaka huyo mwanamke anaonekana hana heshima kabisa yaani bf wake afu anakutukana as if kama mmeokotana bar au disco, my friend think twice about it... over!
 
ukitaka kujua rafiki yako/mpenzi wako/mume/mke wako anakuheshimu kiasi gani, mkasirishe hapo atatoa yale yote ambayo anakuwa ameyaficha juu yako, ukiona hivyo jiepushe mapema . hivyo nakushauri achana na huyo mpenzi anaetoa maneno machafu pindi akiksirika,
 
wakati wa uchumba huwa ni kawaida kwa wapenzi kuficha uhalisia wao....unayoyaona leo hutokea maranyingi baada ya ndoa...ni neema kuwa huyo mpenzi wako kakuonesha mapema vile alivyo...tafakari, chukua hatua.
 
Mchokoze mara kama tatu akikutukana mara zote mwache aende zake .
 

Mosi, Uliwahi kumwuliza hilo swali? Alijibu nini?
Pili, una bahati haya yamewatokea hamjafunga ndoa...sepa...
 
Wewe ni ke au me?
Nikuambie ukweli bila kukufariji; utaweza kuishi nae ktk ndoa ila hutamfurahia, utakuwa mtu wa kumvumilia tu kwa huo mdomo wake usio na break. Swali - utaweza kumvumilia kwa kiasi hicho, bila kikomo, yaani maisha yako yote? Jibu lako obvious ni hapana maana tayari hapo amekutibua sana hadi ukimwona unapata hasira, hivyo ni wazi huwezi kumvumilia huyo.

Ushauri mchungu hapo ni kuwa huwezi kuishi naye ktk ndoa ukapata furaha haijalishi hata kama anayo mazuri mengi sana anayokufanyia, kwa hii thread yako umeonyesha hilo huwezi kulivumilia, amua mapema uepuke kujitafutia stress for the rest of your life. Wapo watu wanaweza kuvumilia maneno machafu lakini naona sio wewe! Shukuru huyo hajaweza kukuficha, amejionesha waziwazi, ungekuwa tayari kwenye ndoa ingekuwa balaa!
 
Kaka huyo mwanamke anaonekana hana heshima kabisa yaani bf wake afu anakutukana as if kama mmeokotana bar au disco, my friend think twice about it... over!
Thanx kwa ushauri ila hapo kwenye KAKA weka DADA na hapo kwenye MWANAMKE weka MWANAMME
 
Mimi ni KE
kwel uvumilivu wangu ktk hlo n mdogo kila nkimuona nataman kulia na furaha yote hupotea
 
Mosi, Uliwahi kumwuliza hilo swali? Alijibu nini?
Pili, una bahati haya yamewatokea hamjafunga ndoa...sepa...
Anadai kuna future na anakua akinielezea pale nakosea ili kunirekebsha kwasababu ananipenda,binafsi najiuliza mbona ye ananiudhi ila cjawah hata cku moja kumtamkia maneno machafu anadai n hasira,nkamwambia hasira zimemfanya atoe yale aliyonayo moyon kwa cku nyng
 
wakati wa uchumba huwa ni kawaida kwa wapenzi kuficha uhalisia wao....unayoyaona leo hutokea maranyingi baada ya ndoa...ni neema kuwa huyo mpenzi wako kakuonesha mapema vile alivyo...tafakari, chukua hatua.
Kwakweli ni jambo la kushukuru
 
Kuhitilafiana katika mapenzi na hata kupandisha jazba si jambo la ajabu lakini ni vizuri kuwa waangalifu ili kujua ni maneno gani yanayostahili kutotamkwa ili usije kutamka matusi ya nguoni yakasababisha penzi kuingia dosari kubwa na hata kuvunjika. Kama mwenzio ana tabia ya kutoa maneno machafu/matusi ya nguoni nawe huwezi kuyastahamili basi kama hatakuwa tayari kubadilika na kuachana na lugha chafu ni vizuri kufanya maamuzi magumu haraka.
 
PLL, future ipo kabisa!! Kuna tamthilia moja imeanza hivi karibuni Star TV(kama upo TZ) inaitwa MariaClara! Kwahiyo ndoa itawepo na itakuwa kama ya Gerry na Suzan....kama upo TZ, nakushauri fuatilia hiyo tamthilia ili ikupe maamuzi sahihi....weekend saa 3 usiku; ijumaa na jnne ni saa 3.30 usiku.
 
Nashukuru kwa ushaur umenena vyema
 
Khaaa!
 
achana naye asikupotezee mda atakuzesha mapema huyo mapenzi kufurahi yahe mwanamke kauzu wa nn?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…