kali popote
JF-Expert Member
- May 3, 2017
- 394
- 281
Habari za asubuhi JF,
Nianze kwa kusema kwa ufupi sana. Mimi ni mwenyeji wa Arusha katika pita pita zangu nilikutana na binti kwa muonekana ni mzuri na mrembo sana nikampenda akanipenda na kuanza mahusiano ya kimapenzi.
Muda kupita nikajagundua yule binti kumbe alikuwa na mume wake na wameshazaa na mtoto mmoja ingawa la mtoto alishawahi niambia anae ila la mume hakuwahi niambia kwani alinambia mume wake aliezaa nae wameshaachana hivyo yupo single na kumbe ni muongo na ukweli ni walikuwa wakiishi pamoja.
Baada ya kuligundua hilo niliendelea kuwa nae ingawaje kwa kijihadhari sana nikajua huyu ni wakupita tuu na mwishoe kila mtu afuate yake, siku nenda rudi yule binti alipata post ya kwenda masomoni mkoa flani hapa Tanzania kwa ajili ya kujiendeleza na elimu ya ualimu. Binti tuliagana akaondoka kwenda masomoni na hapo hapo haikuchukua muda na mimi nikapangiwaga huko huko mkoa alipoenda yeye kwani nilisha omba maombi ya shahada na nilikubaliwa na kuondoka.
Baada ya kufika huko nilijiamulia mwenyewe yule binti nisimtafute na nimuache kwani asingeweza kunifaa kwanza kanidanganya ile mwanzo na pia anae mtu tayari na kuhusu umri alinipita miaka miwili mimi ninae 27 na yeye anae 29.
Hivyo niliamua kutafuta mwanamke mwingine ambae nilikuwa mkoa huo ingawa nae alikuwa ni mwanafunzi wa ngazi ya cheti cha nursing na mortuary tulianza mahusiano na muda haukupita huyu binti akashika ujauzito wangu, kiukweli niliwaza sana ukizingatia nilikuja kusoma huku lakin nilipiga moyo konde nikamuhaidi kuilea hiyo mimba mpaka atakapo jifungua.
Kimbembe ni yule binti wa mwanzo sasa baada ya kujua kuna binti nipo nae na nimempa ujauzito aliumia sana tena sana na alicho amua yule binti nikutoa msimamo wake wa dhati kwamba pamoja na yote hayo hawezi kuniacha hata kama yametoka hayo maana amenipenda sana na alikubali hata kumuacha mumeo wa kwanza aliezaa nae kisa mimi hapa hivyo ni ngumu na hawezi kuniacha na alisema bora afe kuliko anikose mimi.
Nimalize kwa kusema huyo binti niliempa mimba ameshajifungua na mtoto wa kiume na ana miezi saba sasa na ananipenda sana pia. Shida ipo kwa yule binti kwanza alienizid umri kwani nae bado ananipenda sana na hayupo tayari kuniacha amesema.
Naombeni ushauri wenu wa dhati wana JF kwani nipo katika wakati magumu sana
hata sielewi nifanyaje.
Nianze kwa kusema kwa ufupi sana. Mimi ni mwenyeji wa Arusha katika pita pita zangu nilikutana na binti kwa muonekana ni mzuri na mrembo sana nikampenda akanipenda na kuanza mahusiano ya kimapenzi.
Muda kupita nikajagundua yule binti kumbe alikuwa na mume wake na wameshazaa na mtoto mmoja ingawa la mtoto alishawahi niambia anae ila la mume hakuwahi niambia kwani alinambia mume wake aliezaa nae wameshaachana hivyo yupo single na kumbe ni muongo na ukweli ni walikuwa wakiishi pamoja.
Baada ya kuligundua hilo niliendelea kuwa nae ingawaje kwa kijihadhari sana nikajua huyu ni wakupita tuu na mwishoe kila mtu afuate yake, siku nenda rudi yule binti alipata post ya kwenda masomoni mkoa flani hapa Tanzania kwa ajili ya kujiendeleza na elimu ya ualimu. Binti tuliagana akaondoka kwenda masomoni na hapo hapo haikuchukua muda na mimi nikapangiwaga huko huko mkoa alipoenda yeye kwani nilisha omba maombi ya shahada na nilikubaliwa na kuondoka.
Baada ya kufika huko nilijiamulia mwenyewe yule binti nisimtafute na nimuache kwani asingeweza kunifaa kwanza kanidanganya ile mwanzo na pia anae mtu tayari na kuhusu umri alinipita miaka miwili mimi ninae 27 na yeye anae 29.
Hivyo niliamua kutafuta mwanamke mwingine ambae nilikuwa mkoa huo ingawa nae alikuwa ni mwanafunzi wa ngazi ya cheti cha nursing na mortuary tulianza mahusiano na muda haukupita huyu binti akashika ujauzito wangu, kiukweli niliwaza sana ukizingatia nilikuja kusoma huku lakin nilipiga moyo konde nikamuhaidi kuilea hiyo mimba mpaka atakapo jifungua.
Kimbembe ni yule binti wa mwanzo sasa baada ya kujua kuna binti nipo nae na nimempa ujauzito aliumia sana tena sana na alicho amua yule binti nikutoa msimamo wake wa dhati kwamba pamoja na yote hayo hawezi kuniacha hata kama yametoka hayo maana amenipenda sana na alikubali hata kumuacha mumeo wa kwanza aliezaa nae kisa mimi hapa hivyo ni ngumu na hawezi kuniacha na alisema bora afe kuliko anikose mimi.
Nimalize kwa kusema huyo binti niliempa mimba ameshajifungua na mtoto wa kiume na ana miezi saba sasa na ananipenda sana pia. Shida ipo kwa yule binti kwanza alienizid umri kwani nae bado ananipenda sana na hayupo tayari kuniacha amesema.
Naombeni ushauri wenu wa dhati wana JF kwani nipo katika wakati magumu sana
hata sielewi nifanyaje.