Kuinyima kura CCM wakati naipenda

Kuinyima kura CCM wakati naipenda

kalcha

Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
79
Reaction score
12
Katika kipindi cha hivi karibuni, tumeshuhudia mengi yanafanyika kujaribu kuwaaminisha watu kuwa fulami mbaya, mchafu, mwizi na hafai kusimamia utekelezwaji wa majukumu ya nchi. Katika vita hii, inaoneka chama tawala ambacho kimekaa madarakani kwa miaka takriban28 + 16 ndicho kinaonekana kumchafua mgombea wa chama chenye nguvu ya mpambano. Kwa muono wangu huu ni UDHAIFU MKUBWA SANA.

Binafsi sikubaliani nao na naomba kutumia fursa hii kuwaomba wanaoengineer mpango huu waache maana unazidi kupoteza nguvu zao. Kipindi kilichokuwa madarakani, kingeweza kutosha kabisa kuwafanya wananchi waamini kuwa hakuna mwingine anayeweza kufanya mambo mazuri zaidi.

Huwezi kupata maneno ya busara kuwaambia watu kwa mifano hai ya ulichotekeleza mpaka utafute mbinu za kumchafua mpinzani wako!! Cha ajabu halafu hata mpinzani wetu haonyeshi hasira, wala kuhangaika na hoja zetu. Tuache tunakimbiza wanachama wenye uwezo wa kufikiri. Tutabaki na mambumbumbu mpaka lini!! Mnatukera sana mpaka na sie tunaona bora tuu muadhibiwe! Maana hata kama unampenda sana mtoto, akikosea unamuadhibu huku unaumia.

Kabaki tuu Magufuli anahubiri atafanya nini, ukimuuliza chama chetu kimefanya nini anaweka mipango ya kuwaadhibu waliomteua. Nina wasiwasi nae anaweza siku akasema kama Bashe ubunge mpeni huyu... urais mpeni LWS!! Inasikisha sana.
 
Acha unafiki utaipendaje na kuichukia usijue wa kumpa kura? Mpe unayemtaka kura siri yako acha kuuliza maswali yasiyo na kichwa wala mguu.
 
Rofa siku zote ni rofa tu. Unajifanya mwana CCM wakati wewe ni UKIWA hebu tupishe hapa.
 
Siyo Rofa ni Lofa jamani. Hivi kwa hali hii ya kampeni kupigwa na foreigners kuna mabadiliko kweli hapa?
 
kuinyima ccm kura ndio upendo wa dhati kabisa. Na ihi wanaccm wengine watuunge mkono.

Maana kwa miaka 50 wameshindwa kabisa kuondoa maadui wa 3
1 - ujinga
2 - maradhi
3 - umaskini

sasa mwenye mapenzi ya dhati kwa ccm ni lazima akipigie kura ya HAPANA ili kikae pembeni kwanza.

Ili ulevi wa kukaa madarakani kwa muda mrefu uwaishe. Na kujua nini maana ya kuongoza kwa ufanisi.

Unajua dereva anaye endesha gari hawezi kuona kama anaendesha vizuri kwa sababu yeye yupo kwenye msikano.

Lakini aliye pembeni ndio anajua dreva yupo vizuri au vibaya na huyu wa pembeni anaona hatari na mambo kuliko dereve maana dereva uaga focas na kuendesha.

Hivyo huyu wa pembeni akipewa gari ameshajua dereva alikua anakosea wapi.

Kubalini2 ccm mkae angalau miaka 10 nje ya ulingo wa serikali mjifunze. Mtakuwa wazuri sana.
 
Kuichagua ccm utakuwa zezeta, mtumwa wa mawazo, mtanzania amka, miaka 54 leo hii hakuna maji safi na salama mijini!! je vijijini utasemaje? Wake zetu,Mama zetu, dada zetu, watoto wetu wanalazwa chini wakati wanatuzalia viongozi wa Taifa la kesho. Mabadiliko muhimu
 
Dr Slaa ni msema kweli, kawaminya pabaya ukawa na fisadi wao anaegombea uraisi. Tunamtaka mgombea wa ukawa fisadi aje hadharani akanushe kama yy ni msafi. Slaa toa dozi ingine hii inaonekana imewalewesha tu bado wanayumbayumba. Watabeba sana watu na mabasi kuwasombelea kutoka Moshi, Arusha ili wajaze mafuriko mikoa mingine.
 
Back
Top Bottom