Mkuu figganigga this is too much. Hawa watendaji wa Magufuli naona wanaacha kufanya kwa weledi na wanaanza kufanya kazi kwa kulipiza kisasi na kukomoana. Kama hilo jengo liko bondeni na jengo la CCM pembeni yake liko angani? Na nyumba zaa serikali ambazo ziko pembeni je? na ofisi za CEDHA nyuma yake je? Kama hizo zote hazijapigwa X basi na hili jengo lisipigwe X wala lisivunjwe.
sasa kwanini nyumba zote zimewekwa X jangwani isipokuwa DART stendi ya magari ya mwendokasi je kwann wameiacha?Kama Naura imeingilia kwenye uelekeo wa mto au sehemu hisiyo stahili itabomolewa kama wanavyo bomolewa wengine na Kama jengo la Ccm limejengwa sehemu isiyo stahili basi itabomolewa...! Msihusishe hili jambo na siasa..! Watendaji wanafanya kazi kwa weledi mkubwa....
mikataba inayolinyonya taifa itabomolewa lini? Madini gesi nkBomoa tu tunataka Arusha uwe mji wa Kimataifa, na hauwezi kufikia hiyo hadhi kama kila mtu anajenga anavyotaka, nasema Bomoa yote tuanze upya kesho utambue kwamba fedha siyo kila kitu bali kuna sheria za nchi ambazo ni lazima zifwatwe!
Ukweli ni kwamba jamaa alitumia pesa nyingi kuwahonga watu na pia wengi waliumia kutokana na kupinga ujenzi huo sasa muda umefika!
mikataba inayolinyonya taiga itabomolewa lini? Madini gesi nk
Hatukatai anatumia sheria ila sheria ikipitiliza inakuwa sio sheria tena ni udicteta kwa sbb amesaidia pia Kutoa ajira. Kwa vijana wasiokuwa na ajira. Zikibomolewa hao wafanyakazi wataenda wapi.CCM ya magufuli siyo CCM ya JK,,huu ndio utawala wa haki na sheria..huyo mzee kama alitumia fedha kupindisha sheria kwenye utawala wa jk ngoja aonje joto ya jiwe!!!
Heshima yenu wakuu,
Mimi kuna Maswali yananitatiza;
Hili jengo Mahakama ndiyo ilimruhusu ajenge baada ya kushinda kesi dhidi ya Manispaa ya Arusha kumzuia Kujenga.
Eti inavunjwa kisa ipo bondeni. Mbona maji hayaingii ndani? Mto Sanawari Miaka yote upo na hili jengo halijawahi kusitisha shughuli kisa maji yameigia wala hapajawahi kutuwama maji.
View attachment 315535 View attachment 315536
Mkuu issue ya Naura Spring ni zaidi ya unavyojua, kumbukumbu zangu zinaonyesha waliopinga ujenzi wake kwa sababu sheria inakataza ujenzi wa nyumba ndani ya mita 60 kutoka mtoni walihamishwa kufuatia kubishana na wakuu wao.
Kama itavunjwa Mrema avumilie maumivu yake kama ambavyo wale viongozi walivyovumilia baada ya kuhamishwa.
Mt Meru iko umbali gani kutoka mtoni na Naura Springs iko umbali gani?Hapa ina maana na hospitali ya mount meru na BOT nazo zibomolewe
CCM ya magufuli siyo CCM ya JK,,huu ndio utawala wa haki na sheria..huyo mzee kama alitumia fedha kupindisha sheria kwenye utawala wa jk ngoja aonje joto ya jiwe!!!
Name calling does not save the hotel! Take us thru' alternative measures to conserve our ecosystem! Sio kutukana boss! Matajiri kutumia vijisente vyao kurubuni watendaji ndio tatizo!
hivi mtiririko wa maji hupungua kutokana na chanzo kupunguza kutoa maji au maji yanapopita? Unataka kutuambia kwamba hiyo Hoteli imejengwa kwenye mapito ya maji. Lakini pia kuna kitu nakijua kuhusu viongozi wetu, ni wajinga sana wanapotaka kuonesha kwamba wao wana nguvu!Naura Springs imejengwa kwenye mto Goliondoi na ukitaka kujua athari za ujenzi huo kaangalie flow ya maji ya mto Goliondoi ilivyopungua
Mt Meru iko umbali gani kutoka mtoni na Naura Springs iko umbali gani?
Ni lazima serikali iangalie faida na hasara zitakazotokana na kuvunja majengo kama hayo ambayo hata hivyo yalijengwa kwa vibali halali vya serikali.
Serikali inakusanya kodi kwenye uwekezaji huo, wafanyakazi wameajiriwa, wageni wanapata mahali pazuri pa kulala, mandhari ya jiji inapendeza.
Kwa upande wa pili serikali italipa fidia ya mabilioni kwa uvunjaji, chuki kati ya wawekezaji, wananchi na serikali itaongezeka, mapato yatapotea, wafanyakazi watarudi mitaani nk.
Nashauri watu wa mazingira wasijifanye vichaa na rais atoe tamko kwa majengo kama hayo kwani hata ya serikali hayako umbali wa mita 60 kutoka ukingo wa mto Naura. Kwa mfano TRA, Ofisi ya ya RPC Arusha na Central Police Station, CEDHA, NSSF House iliyoko eneo la zamani la Matongee n.k.