Baada ya kuongea na rafiki zangu kadhaa, nimegundua kwamba ''Kuagana" imekuwa fasheni siku hizi.....Labda nawahukumu bure....
Ndoa ni kitu tukufu, misahafu ni shahidi,
Yataka moyo mkunjufu, hakuna mlio wa bundi,
Zawadi kama mikufu, tuzo njema kwa ushindi,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Zamani likuwa sifa, heshima liwekwa mbele,
Binti alifundwa vyema, katu sipige kelele,
Uwanja safi daima, watoto sipate upele,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Ndoa meingia doa, leo kuna kuagana,
Siku muhimu ya ndoa, wa zamani anapewa,
Penzi kama kukohoa, ni tabu kwa waungwana,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Kama wa zamani mzuri, kwanini hakukuoa,
Ka anukia uturi, nenda kapeleke posa,
Kwao huyu umekiri, kwa yule nataka poza,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Fungate haina mvuto, viungo vimelegea,
Ndoa sasa ni kipato, na bado utamegewa,
Ni moto pia fukuto, la upate ngekewa,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Mimi nilisema hakuna haja ya ndoa siku hizi, mkanishambulia haya sasa yaoneni haya ya mshairi wetu leo!
majuti ni mjukuu, babu yangu aliniasa
nenda wangu mjukuu, uachane na anasa
ukaweke lango kuu, ukafunge na vitasa
kama imekuwa fasheni, nani wa kulaumiwa?
vionjo unavitaka, ndoa unaitaka
wafanana na maji taka, yangu ndio mashaka
hata utoe zaka, milele una mashaka
kama hukuwa tayari, uliharakia nini?
mabadiliko ya kweli, daima huanza nasi
tusikimbilie mseli, na kubambikiana kesi
tuwe na mapenzi ya kweli, ndio twende kwa kasisi
kuagana ni batili, kamwe sifagilii
duuh..nikiwaza hii kitu pozi zinaniisha kbc
majuti ni mjukuu, babu yangu aliniasa
nenda wangu mjukuu, uachane na anasa
ukaweke lango kuu, ukafunge na vitasa
kama imekuwa fasheni, nani wa kulaumiwa?
vionjo unavitaka, ndoa unaitaka
wafanana na maji taka, yangu ndio mashaka
hata utoe zaka, milele una mashaka
kama hukuwa tayari, uliharakia nini?
mabadiliko ya kweli, daima huanza nasi
tusikimbilie mseli, na kubambikiana kesi
tuwe na mapenzi ya kweli, ndio twende kwa kasisi
kuagana ni batili, kamwe sifagilii
Magu panda jukwaani, nahitaji wako mzani,
Klorokwini sikuoni, una busara pomoni,
Okoa ndoa kinani, watupishe hayawani,
Kuagana unapotaka kufunga ndoa iwe mwiko.
Lizzy mbona sikuoni, nani kakuficha ndani,
Yakuonea makini, mchango wako ni thamani,
Hata kama we mpagani, ndoa iwe jukwaani,
Kuagana unapotaka kufunga ndoa iwe mwiko.
<br />Mimi nilisema hakuna haja ya ndoa siku hizi, mkanishambulia haya sasa yaoneni haya ya mshairi wetu leo!
uliharakia nini, bazazi nakuambiaGive me more Shantel,
U have more 2 tell,
I will buy ur idea, just waiting 4 u 2 sell!