Ku root simu

Ku root simu

lindunduru

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2015
Posts
392
Reaction score
554
Nina tecno H5 kwa sasa ina stack hovyo hovyo. Sasa nawezaje kuiroot ili niingize Os mpya. Msaada wenu tafadhali.
 
Jinsi ya ku ‘root’ simu yako ya Android.

Utangulizi:
Simu zetu za Android zimekua sehemu ya Maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia katika Mawasiliano, Kuhifadhi kumbukumbu za muhimu, burudani, biashara, nk. Haya yote hufanywa na Program ambazo huwekwa kwenye mfumo wa simu (Operating System). Programu hizo hubeba maaginzo maalum (Set of instructions) ambazo humwezesha mtumiaji kufanyia mambo mbalimbali kutegemea program hio. Mfano wa program muhimu kwenye simu ni kama vile Opera Mini (humwezesha mtumiaji kufungua kurasa mbalimbali za Intaneti), Calculator, nk.
Program hizo huwekwa sio tu kwenye simu, bali hata vifaa vingine kama vile Computer. Mtumiaji wa Simu au Computer ndie anaeamua program ya kuweka kutegemeana na matumizi yake. Katika miongo michache iliopita zimetengenezwa program nyingi mpya na zenye maboresho makubwa na ya kisasa. Ubunifu uliopo katika program mbalimbali unaleta ukuaji katika Nyanja mbalimbali katika maisha yetu ya kila siku. Program hizi pia zimeleta urahisi na ufanisi. Mfano Calculator, Saa, Vitabu Vitakatifu (Biblia na Kuran), Kamusi, Camera, nk.. vyote vimetengenezewa PROGRAM na kuwa rahisi kuvitumia katika simu muda wowote, mahali popote.
SASA TUJE KWENYE MADA;
Android ni Mfumo wa simu (Operating System) ambao unaboreshwa siku hadi siku. Mfumo huu una majina tofauti kutegeana na toleo lake. Haya ni Matoleo (Versions) mbalimbali ya Android kuanzia ya kwanza mpaka ya mwisho;
1. Cupcake (1.5)
2. Donut (1.6)
3. Éclair (2.0 – 2.1)
4. Froyo (2.2 – 2.2.3)
5. Gingerread (2.3 – 2.3.7)
6. Honeycomb (3.0 – 3.2.6)
7. Ice Cream Sandwich (4.0 – 4.0.4)
8. Jelly Bean (4.1 – 4.3.1)
9. KitKat (4.4 – 4.4.4)
10. Lollipop (5.0 – 5.1.1)
Matoleo haya huboreshwa kadri yanavyozidi kutolewa. Kujua toleo la simu yako nenda Settings – About phone – Android Version. Ukikuta Jelly Bean, KitKat au Lollipop hongeara! kwani unatumia matoleo ya mwisho yalioboreshwa!!
Mfumo huu wa Android unafaa kufanyiwa settings mbalimbali na kuwekewa Program mbalimbali ili kumfanya mtumiaji aifurahie simu yake kwa asilimia 100, lakini shida huja kwamba sio kila PROGRAM inayowekwa katika mfumo huu wa Android inakubali kufanya kazi!! Wapo watengenezaji wengi wa program (Software Designers) ulimwenguni. Sasa watengenezaji wa mfumo huu wa Android wamezuia Program ambazo hazijatoka kwao zisifanye kazi kwenye mfumo huo kwa sababu za kimaslahi.
HAPA SASA TUTAPATA KUELEWA MAANA YA KU ‘ROOT’ kua ni kuifanya simu ikubali Program zilizozuiwa na watengenezaji wa Android (Android Developers). Ukishai ‘root’ simu yako sasa utakua na uwezo wa kuweka program zinazohitaji ‘root permission’ kwenye simu yako.
JINSI YA KU ‘ROOT’ SIMU YAKO.
Kuna aina za simu ni rahisi sana ku root, lakini nyingine zinahitaji utafiti wa kina na muda wa kutosha. Zipo program nyingi sana zinazoweza kutusaidia zoezi hili. Mojawapo ya Program ambazo zinajulikana sana kwa ku root simu ni kama vile KingRoot, Vroot, Kingoapp Root, SRSRoot, Framaroot, Root Master, z4root, Universal root, Easy root, nk.. Baadhi ya Program hizi zitahitaji Computer, nyingine hazihitaji.
Katika Makala hii tutaelekeza kwa kutumia Program iitwayi KingRoot ambayo inakubali kufanikisha zoezi hili kwenye asilimia kubwa ya simu za Android. Program hii haihitaji Computer. Kuipata nenda Google kisha I isearch na kui download. Kwa msaada uliza……

Maandalizi:
(i) Charge Simu yako, angalao ijae kwa 50%
(ii) Wezesha ‘’Developer Options” kwenye simu yako. Menu hii imefichwa kwa watumiaji wa kawaida. Sisi tunataka kutumia simu zetu kwa 100%. Sasa kuifichua nenda Settings>About phone>Build number. Baadhi ya simu (LG na HTC) nenda Settings>About phone>Software information>Build number. Ukishafika kwenye Build number gusa hapo mara saba (tap 7 times)…mpaka uambiwe “You are now a Developer”
(iii) Sasa nenda Settings>Developer options>USB debugging. Weka tiki hapo (kama haipo)
(iv) Nenda settings>Security>Unknown Sources. Weka tiki hapo (Kama haipo).
Hapo maandalizi yatakua ni tayari. Sasa download KingRoot 4.0 (in MB 6.34) kwa kui search kwenye Google kisha Install kwenye simu yako. Baada ya ku install gusa ‘Open’. Baada ya hapo KingRoot itafunguka na itaitambua simu yako automatically—Model ya Simu na Toleo lake. (Mf. Model: H6 Android 4.4.2). Kama simu yako haijawahi kuwa rooted utaona ‘Root access is unavailable’. Chini gusa ‘START ROOT’. Hapo KingRoot itakua inakomboa simu yako kutoka kwenye kifungo cha maisha…kuwa na subira zoezi hilo litachukua muda kidogo (sio Zaidi ya dak 6)…mpaka utakapoona ‘ROOT SUCCSSFULLT’ DONE!!!!! YOU ARE NOW A SUPERUSER…!!!!!

--

Ili kuhakikisha kama simu yako imeshakuwa rooted, nenda PlayStore kisha download Root Checker. Ukishai Install na kuifungua gusa ‘VERIFY ROOT’. Ukiona ‘’Congratulations! Root access is properly installed on this Device” HAPO KILA KITU TAYARI!!!!!

FAIDA ZA KU ROOT SIMU:
1. Utaweza ku update toleo la mfumo wa simu yako (Kuflash). Mfano kama unatomia Android 4.4.2 (KitKat) unaweza kui update kwenda Android 5.0 (Lollipop) Simu ya Android haiwezi kuflashiwa bila kuwa rooted!
2. Hua inatokea simu kuibiwa. Wewe unaesoma Makala hii usiibe simu ya Android siku hizi (ukiokota mtafute mwenye nayo). Nitafute nikupe story!! Sasa zipo program nyingi za ku track simu yako wakati imeibiwa lakini nyingi huondoka kwenye System ya simu yako baada ya kufanyiwa ‘Factory reset’ au kuflashiwa. Kama ume root simu yako, zipo Program za kuitafuta simu yako ambazo hata mtuhumiwa aiflash au aireset….BADO ITAKUWEPO TU! Mfano wa Program hizo ni Cerberus.
3. Utakua na uwezo wa kuweka Program nyingi na nzuri za kuifanya simu yako iwe fasta na kuboresha muonekano (performance and appearance). Pia kuna program za kutunzia chaji, Kuzuia matangazo kutoka Google (mf. AdAway), n.k…. ambazo hazitafanya kazi bila root

ZINGATIA:
Rooting inaweza kuharibu kabisa kuharibu simu yako na kuifanya isiwake tena!! (Mimi hapa sitahusika kwa lolote) Usiogope, hii huwatokea wale wanaokurupuka na kutofuata maelekezo. Mimi binafsi nishairoot simu yangu na za Marafiki zangu zisizopungua 20 bila madhara yoyote kutokea. Fanya utafiti kwanza ni program gani sahihi ku root simu yako, omba ushauri,…..
Pia Rooting inaharibu Warranty ya simu yako. Kama ulipewa Warranty uliponunua simu yako na ukaikuta na tatizo, ukiirudisha haitakubalika. Aidha, inawezekana pia ku’unroot’

HITIMISHO:
Kwa yeyote ambae ni mdadisi na mtafiti, anaependa kusaidiwa na Technologia, kuna ulazima wa kuroot simu yake. Baada ya Makala hii, wale woote ambao tutaenda sambamba tutaanza kupitia Programs nyingi ambazo zinahitaji ‘Root Permission’. Mie natumia Tecno H6, baada ya kui root nimeifanyia Settings nyingi sana na ninaitumia katika mambo mengi sana!! ROOTING imeniwezesha hata kubadilisha muonekano wa maandishi system nzima!!
 
Mkuuu shukrani... nimeelewaa vizuri sanaaa SALOK
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimefuta hatua zote ila ikiaanza kuroot ikifika kwenye 54% inashindwa kuendelea na kuandika failed.nifanyeje ilinifanikiwe aisee?
 
Nina tecno H5 kwa sasa Ina stack hovyohovyo.sasa nawezaje kuiroot ili niingize Os mpya.msaada wenu rafadhali.

katika simu za tecno ambazo ni kimeo basi H5 ndio namba 1. nakushauri uza ununue hata p5 auY3 au Y4 . hiyo H5 itakusumbua sana utakuwa unareset kila mara na kuStack ndio kawaida yake.
 

Attachments

  • 1439666294343.jpg
    1439666294343.jpg
    27.9 KB · Views: 536
Salok,vp kuhusu swali langu hapo juu?msaada tafadhari
 
Mkuu Nina Tecno Phantom A+ Nitumie Program Gani Ya Kuroot Simu Nisije Yakoroga Simu Ikazima
 
thanks mkuu kwa uzi wako huu nimefanikiwa ku root simu yangu aina ya samsung galaxy gt 7392
 
Nimefanikiwa Ku Root Simu Yangu Tecno Phantom Na Sasa Nahitaji Kuweka Os Mpya Je Inawezekana Na Kama Ndio Nifanyeje.
 
Ahsante sana Mkuu SALOK kwa ufafanuzi wako; hatimaye nimefanikiwa kuiroot simu yangu.
 
Last edited by a moderator:
"Baada ya Makala hii, wale woote ambao tutaenda sambamba tutaanza kupitia Programs nyingi ambazo zinahitaji ‘Root Permission" Mkuu SALOK nimenukuu hiki kipande nadhani ni muda muafaka sasa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu salok vipi kwa huawei y300 inakubali
 
Ahsante sana Mkuu SALOK kwa ufafanuzi wako; hatimaye nimefanikiwa kuiroot simu yangu.

"Baada ya Makala hii, wale woote ambao tutaenda sambamba tutaanza kupitia Programs nyingi ambazo zinahitaji ‘Root Permission" Mkuu SALOK nimenukuu hiki kipande nadhani ni muda muafaka sasa.

shukrani mkuu. programs ziko nyingi ila nitazitaja kwa uchache.....
 
Last edited by a moderator:
mfano wa program hizo ni IFONT. hii inakuwezesha kubadilisha mfumo wote wa maandishi ktk simu yako..!!
 
Back
Top Bottom